NDESAMBURO ATOA MASHARTI MAGUMU CHADEMA.

































NDESAMBURO ATOA MASHARTI MAGUMU CHADEMA.
Mdhamini mkubwa wa CHADEMA mh. Ndesamburo atoa masharti magumu kwa chadema baada ya Binti yake Lucy Owenya kukosa Ubunge wa viti maalum.

Mpashaji wetu ameieleza Kisima kuwa Ndesamburo alimwita Mbowe Moshi na kumpa masharti makali kuwa kama Binti yake Lucy Owenya hatapata Ubunge atasitisha misaada na kuipeleka kwa kwa chama cha ACT wazalendo kumuongezea nguvu Zitto Kabwe, na kutangaza rasmi Vita na chadema.

Hata hivyo Mbowe aliomba radhi na akamwambia mchakato wa viti maalum haufanywi na mtu mmoja, bali kuna taratibu ndani ya chama na NEC pia. Hata hivyo inaonekana nia ya Mbowe ilikuwa kuwatupia zigo Tume ya Uchaguzi, jambo ambalo sio kweli.

Baada ya mazungumzo yote walihitimisha kwa kukubaliana. Mbowe aliomba radhi na kukubali kuyatekeleza masharti, kwa kuanza kumtoa Lucy Owenya nafasi ya 39 na kumshusha hadi nafasi ya 37 ya orodha ya mpangilio wao wa viti maalum . Nafasi ya 37 inamfanya Lucy kuwa mtu wa Kwanza katika viti maalum vipya watakavopata chadema baada ya kumalizika uchaguzi huu unaoendelea desemba 20. Kama tutakumbuka tume ya Uchaguzi walibakiza viti vitatu kutovigawa ndio hivyo ambavyo wanategemea kimoja wampe Lucy endapo wataongeza asilimia za kura za kupata sifa kupata viti maalum hivyo.

Pamoja na hayo inasemekana sababu iliyo sababisha Lucy Owenya akose nafasi ya kiti maalum ni ukaribu wake na mwanasiasa machachari Zitto Kabwe, hongera yake Lucy Owenya kwa kupewa matumaini na poleni madada wa CHADEMA ambao mlikuwa nafasi ya 37 na 38. Lucy Owenya kachukua nafasi yenu, midhali ni maamuzi ya chama, hamna budi ya kuyakubali na kuongeza juhudi zenu katika ujenzi wa chama.

Kisima Cha Jangwani.