KAMA PARIS INAULIWA NA MIZIMU YA SYRIA, WACHA IFE, SITALIA!

KAMA PARIS INAULIWA NA MIZIMU YA SYRIA, WACHA IFE, SITALIA!
Hakika nimeumia sana kwa yaliyotokea Paris, watu waso na hatia wakifa bure bila sababu yoyote au kwa makosa yalo fanywa na wanasiasa.
Hata hivyo, ni dhahiri kuwa haya yote ni matukio ya kigaidi, ni mwendelezo tu ya matukio mengi ya kigaidi yanayo endelea kutokea duniani.                     


Pamoja na kulaani hili la Paris na mengi yenye kufanana na hili, naomba tujiulize hivi zile silaha za maangamizi ambazo Saddam Hussen alituhumiwa nazo hata akavimiwa kijeshi NATO ziko wapi? Iweje hadi leo pasionekane dalili yoyote ya nchi ya Iraq kumiliki silaha zile?
Dhahiri kuwa NATO walizusha hili la silaha za maangamizi ili wapate uhalali wa kuivamia Iraq, baada ya vita ile hadi leo hii Iraq hakuna salama ukilinganisha na enzi za Saddam.
Wairaq 165,000 ambao si wapiganaji walikufa wakati vita, wengi wao wanawake na watoto, na baada ya vita na hata sasa wairaq wasiopungua milioni moja wamekufa kutokana na kutotengamaa kwa hali ya usalama tangu uangushwe utawala wa Saddam.
Ukiniambia nani aliyewaua wairaq hawa wasio kuwa na hatia, jibu langu ni NATO na washirika wake, sababu wairaq hawa hawakuuliwa na silaha za maangamizi za Saddam bali waliuliwa na silaha za NATO na washirika wake, pia kwakuwa Saddam hakukutwa na silaha za maangamizi, kwa vyovyote vile ule uvamizi ulosababisha vifo hivi hakuwa halali na ulishinikizwa zaidi na mgongano wa kisiasa kati Baghadad na Washington.
Walioshiriki kufanya mauaji Iraq, dunia haioni kama walikosea, na kwa hivyo hakuna shinikizo lolote la kutaka wahusika wachukuliwe hatua za kisheria hata haki ya waliopoteza maisha ipatikane. Linaloonekana ni kupongezwa kwa watu hao.
Kwa vyovyote vile waliopoteza wapendwa wao wanatafuta haki za ndugu zao kwa namna nyingine, na ninaweza kusema Paris, London, Washington, nk imevamiwa na mizimu(ghost) ya watu walikufa bila hatia katika ardhi ya Iraq, nami nasema kama ni mizimu ya wafu wa kivita, wacha iwatafune wao na vizazi vyao!
Baada ya kuanguka utawala Saddam, ndipo yalipo zuka makundi ya kigaidi kama vile ISLAMIC STATE, makundi ambayo yasingezuka kama kungekuwa na usalama nchini Iraq, na kwa vyovyote vile yalianzishwa ili kulipiza kisasi kwa kile kilichotokea Iraq au makundi haya yana ajenda yao ya siri sema wanajipatia uhalali kwa watu waliopoteza wapendwa wao kwa jina la "kisasi dhidi ya madhalimu wa kimagharibi."
Rais Bush hakupelekwa ICC kwa kile alichokifanya Iraq, sababu Marekani si mwanachama ICC, lakini ajabu Marekani hiyo inaishinikiza mahakama hiyo kuwashughulika bila ajizi viongozi wa Afrika kwa uhalifu wa kivita. Hapo ndipo inapo ibuka shaka. Uovu wa NATO dhidi ya binadamu unaitwa vita dhidi ya ugaidi, na wale wanaolipiza kisasi kwa uovu wa NATO wanaitwa magaidi.
Kuku na yai kipi kilianza? Uovu magharibi(NATO) dhidi ya ubinadamu na ugaidi, si swali la kuku na yai hata tusijue kipi kilianza. NATO ndio iliyoanza kufanya dhuluma kwa binaadamu kwa tamaa za malighafi, ndipo ukafuata ugaidi ambao lengo lake ni kupigania haki iliyoporwa kutokana na uovu wa NATO.
Mathalani, Ulaya ilivamia Afrika na kujigawia kama mali yao, watawala wa jadi waliopinga hili walionekana magaidi kama magaidi wa sasa, chini ya sheria zao na mahakama zao walinyongwa. Alichofanyiwa Saddam Hussen akina tafauti na alichofanyiwa Kinjetile Ngwale.
Kinachotokea sasa duniani ni ukoloni uliovaa joho jipya, ni mwendelezo wa ULAYA chini ya NATO kuendelea kutaka kupora malighafi katika nchi za Afrika na za kiarabu, ni mwendelezo wa kutafuta masoko ya silaha zao kwa lazima kwa kuzusha vita au kuvuruga utulivu na usalama. Vurugu zote za ULAYA zinafanyika mbali na Ulaya kwaajili ya usalama wa watu wao, sasa wanastuka watu 153 kufa wakati hadi sasa wairaq waso pungua milioni moja wamekufa sababu ya UVAMIZI WA NATO.
Mkwawa aliyedhulumiwa, kama huko aliko anasikia kilichotokea Paris, atahuzunika kidogo sababu walokufa si ng'ombe, lakini kwa vyovyote vile atasema "afadhali na waendelee kuuliwa huenda watajua machungu ya kuondokewa na wapendwa wao hata waache kuzusha vita katika mataifa ya wenzao"
Kama ukiketi na kujiuliza, utagundua asilimia kubwa ya kile kinachoitwa ugaidi kimetokana na dhuluma, dhuluma ambayo haina njia ya kuidai mahakamani. Kwa kukosekana hilo, mdhulumiwa hubaki na fundo rohoni, fundo ambalo humlazimisha kufanya lolote ili mradi tu yule aliyemdhulumu alipe na ajue ni kwa kiwango gani ameumia. Washirika wa NATO wanajua nini walikifanya au wanaendelea kukifanya mashariki, kwa kugundua hilo ndio maana kimenuka Paris, lakini Obama, Cameron na Angela Mack wametaharuki uku wakijipanga kwa lolote ambalo laweza tokea katika nchi zao.
Kama ukiketi na ukichunguza, utagundua kila sehemu ambayo ina Civil war kwa namna moja ama nyingine kuna mkono wa nchi za magharibi.
SYRIA, UWANJA WA VITA KATI YA NATO NA URUS.
Huyo mtoto aliyeliyesukumwa maji katika fukwe amekufa maji baada ya kukimbia vita ya Syria kwa njia ya bahari, na huyo mtoto mwingine ni mhanga toka katika uwanja wa mapambano. Watu wengi wamekufa katika uwanja wa kivita na wengi wamekufa maji katika bahari meditarania.
Kinachotokea Syria sasa ni vita ya WAKUBWA WA DUNIA wakigombea rasilima za Syria, Vita Syria ni vita kati NATO(Ufaransa na USA) kwa upande mmoja na URUSI kwa upande mwingine chini ya mwavuli wa civil war inayoendelea sasa Syria.
NATO inawafadhili waasi dhidi ya serikali.
URUSI inaifadhili serikali ya Assad.
Makundi yote haya, NATO na Urusi wanachofikiria mafuta ya tu! Kushindwa kwa waasi ndio kushindwa kwa NATO na kushindwa kwa Assad ndio kushindwa kwa Urusi, vita itaisha endapo NATO na Urusi wakiamua iishe! Makundi yote haya mawili yanataka ipatikane serikali thabiti ya Syria ambayo wataweza kuiendesha watakavyo, na kila kundi halikubali kushindwa hadi pale hiyo serikali itakapo patukana!
Ufaransa na Marekani wanajua wanachokifanya Syria kimesababisha vifo vya watu wasiopungua mil 1, na mimi na wewe pia tunajua, alafu watu 153 waliokufa Ufaransa wasabaishe nami nilie?? nina wazimu? hao 153 waliokufa nitahuzunika sababu si ng'ombe lakini siwezi kuwalilia na kuomboleza ikiwa wao wamesabisha mamilioni ya watu kufa katika maeneo tafauti duniani, heri nao waonje machungu huenda watajifunza utu na sio utu wa bandia wanao tuonesha.
Wengi tumeshangaa Facebook kuanzisha utaratibu wa kuweka kivuli cha bendera ya Ufaransa juu ya profile picha kama njia ya kuoneaha kuguswa na msiba wa Paris, lakini hakufanya hivyo siku mbili kabla ya Paris pale lilipofanyika shambulio la kigaidi Beiruti, ukiuliza kwanini? Hawakufanya hivyo lilipotokea Wastegate na Garrisa? Washatoa jibu la kisiasa, lakini ukweli utabaki kuwa hayo mengine hakukufanyika Ulaya.
Kwanini mshituko wa Magharibi juu ya Paris ni mkubwa zaidi ukilinganisha wa China au Urusi? jibu ni jepesi, Dola ovu zimeshuhudia mwovu mwenzao akishughulikiwa kiasi na wao wajipange sababu uovu wao ni mkubwa kuliko hata wa Paris.
Pamoja na kwamba ushiriki wa Ufaransa katika vita ya Iraq haukuwa na madhara kwa wairaq, lakini hakuondoi ukweli kuwa Ufaransa ilishiriki Afghanstan, na sasa inashiriki katika vita vya Syria, na haiondoi ukweli kuwa huwezi kuitenganisha na NATO na Ufaransa.
Poleni wairaq na ulimwengu wa kiarabu kwa kile kilichotokea Iraq na Syria, poleni wafaransa kwa yalotokea Paris, lakini pia naomba mjue vita ilo sababishwa na uvamizi wa NATO Iraq bado haijaisha, vita imenzia kupiganwa Iraq lakini imekwisha sambaa, sasa imefika Paris, poleni wahanga, vita haina macho.
NINI KIFANYIKE
MOSI.
NATO na dunia chini ya UN iombe radhi kwa kilichotokea Iraq naSyria, lakini isiishie kuomba radhi tu lakini pia isijaribu tena kufanya uovu kama ule.
PILI.
NATO na dunia isidhani demokrasia ndio mwarobaini wa matatizo ya watu, hususani waafrika na waraabu. Zipo nchi nyingi za kidemokrasia lakini zina matatizo mengi kuliko hata Libya ya Ghadafi. Watu waachwe waishi kwa utaratibu wao waliouzoea, kabda kwa hiyari wao waamue kubadilika.
TATU.
Wasililazimshe kufanya biashara na nchi ambayo haitaki kufanya biashara nao juu ya malighafi fulani. Sababu hadi sasa imeshakuwa dhahiri, kilicho mgharimu Ghadaf na Saddam ni utajiri wa mafuta katika nchi zao.
Kinyume na hivyo, tutaendelea kushuhudia matukio ya kigaidi katika nchi za NATO na mimi binafsi siwezi kuwa na huruma zaidi juu mamia ya watu dhidi ya maelfu ya watu watakao kufa kwa chokochoko za NATO.
Njano5
0784845394