AZAM IMETINGA NUSU FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO.

Klabu ya Azam FC imetinga fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho nchini Tanzania baada ya kuifunga Mwadui kwa mikwaju ya penati 5 kwa 3.
Azam imefikia hatua hiyo baada ya dakika 120 kumalizika kwa timu hizo kufungana mabao 2-2.

Penati za Azam zimefungwa na Waziri Salum, Allan Wanga, Himid Mao, John Bocco na Agrey Moris huku Kelvin Sabato akikosa penati ya 4 kwa upande wa Mwadui.

KENYA NA TANZANIA ZAKAMATA GARI TATU ZA WIZI.

Polisi wa Kenya na wale wa Tanzania wamepata magari matatu ambayo yalikuwa yameibiwa nchini Kenya na kupelekwa mjini Moshi.Polisi kwenye kaunti ya Taita Taveta wanasema mojawepo wa magari hayo ni ya kampuni ya China inayojenga reli nchini Kenya ya Zong Miang Engineering Company .
Magari hayo matatu yalipatikana yametelekezwa bila mtu kwenye mji huo wa Moshi nchini Tanzania.

USAWA WA BAHARI HUKO NEW ZEALAND UTAINUKA KWA MM 30 KATIKA KARNE HII.

Usawa wa bahari kando ya New Zealand utainuka kwa milimita 30 hata mita moja ndani ya karne hii

Ripoti iliyotolewa na taasisi ya New Zealand inaonesha kuwa, kama utoaji wa hewa inayosababisha kuongezeka kwa joto duniani hakutapungua kwa kiasi kikubwa, joto litaendelea kuongezeka, na usawa wa bahari kando ya New Zealand utainuka kwa milimita 30 hata mita moja ndani ya karne hii.

Kuinuka kwa usawa wa bahari kutasababisha maji ya bahari kuingia kwenye fukwe nchini humo, na hivyo mafuriko yatatokea mara kwa mara wakati wa mvua kubwa. Hivi sasa watu wengi wanaishi pwani, na theluthi mbili ya watu wanaishi katika maeneo yaliyo kwenye hatari zaidi ya kukumbwa na mafuriko.

Mfano pwani ya Otago iliyoko kisiwa cha kusini cha nchi hiyo, tofauti kati ya urefu wa mawimbi yanayosababishwa na tufani yanayotokea kila baada ya miaka miwili na mawimbi makubwa yanayotokea kila miaka mia moja ni milimita 32 tu, hii inamaanisha kuwa kama usawa wa bahari ukiinuka kwa milimita 30, maafa ya mafuriko yaliyotokea kila miaka mia moja huenda yatatokea kila mwaka.

Licha ya hayo, wakati joto linapoendelea kuongezeka, mvua itapungua, kazi za ujenzi, uzalishaji viwandani na utoaji wa maji baridi zitakabiliwa na shinikizo kubwa. Wanyama na mimea ambayo sasa iko hatarini huenda vitatoweka.

Ingawa kuongezeka kwa joto duniani kutasababisha kupanda kwa bei ya bidhaa duniani, na kunufaisha maendeleo ya kilimo nchini humo, lakini pia kutaleta athari nyingi mbaya, na kuhatarisha usalama wa chakula.

TFDA YANASA VIPODOZI HARAMU TANI 15.

Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini TFDA imenasa vipodozi vya magendo tani 15 vyenye thamani ya shilingi milioni 400 mjini Dar es Salaam.
Bidhaa hizo  zilikuwa zimehifadhiwa kwenye ghorofa mbili zilizoko eneo la Karioakoo mjini humo.

Meneja wa TFDA Emmanuel Alphone amesema vipodozi hivyo vimeingizwa bila ya idhidi ya mamlaka husika.
Watu wanane wamekamatwa na kuhojiwa kuhusiana na bidhaa hizo na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

SOMALIA NA AU WAJIPANGA KUPAMBANA NA UGAIDI.

Somalia na Umoja wa Afrika wanapanga kuwa na mikakati mipya ya usalama ili kuzuia matishio ya ugaidi nchini Somalia.

Mwakilishi maalum wa mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Afrika nchini Somalia Bw Francisco Madeira amefanya mazungumzo na naibu waziri mkuu wa Somalia Bw Mohamed Omar Arte kuhusu mambo muhimu ya operesheni za usalama.

Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Africa imesema, kwenye mkutano huo, maofisa hao wawili walijadili kuhusu jinsi majeshi ya serikali ya Somalia na tume ya Umoja wa Afrika nchini humo AMISOM yanavyoweza kuratibu na kushirikiana kulishinda kundi la Al Shabaab.

RIYAD MAHREZ AWA MWAFRIKA WA KWANZA KUSHINDA TUZO YA PFA.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Algeria anayeichezea klabu ya Leicester City ya Uingereza Riyad Mahrez ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya PFA 2015/2016 (Professional Footballers Association).

Riyad Mahrez ametangazwa kushinda tuzo hiyo mbele ya wachezaji kama Mesut Ozil wa Arsenal, Jamie Vardy wa Leicester City, Harry Kane wa Totenham Hot Spurs, N’golo Kante wa Leicester City na Dimitri Payet wa West Ham United.
PFA ni tuzo za wachezaji bora wa kulipwa.

CRYSGAL PALACE IYAKUTANA NA MANCHESTER KOMBE LA FA.

Crystal Palace itakutana na Manchester United katika fainali ya kombe la FA mwaka 2016, kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Watford City.

Yannick Bolasie aliongoza Palace kabla ya Troy Deeney kusawazisha kunako dakika ya 55, lakini Conor Wickham alifunga bao la pili na la ushindi kwenye dakika ya 61.

WABUNGE TISA WAPEWA SIKU 30 KUICHUNGUZA LUGUMI.


















WABUNGE TISA WAPEWA SIKU 30 KUICHUNGUZA LUGUMI.

Akizungumza na waandishi wa habari hapo jana mjini Dodoma baada ya kikao cha kamati hiyo, Kaimu Mwenyekiti wa PAC Mh.Aeshy Hilary amesema uamuzi wa kuundwa kamati hiyo umekuja kufuatia kutoridhishwa na ripoti hiyo pamoja na kuwepo kwa changamoto katika taarifa ya utekelezaji wa mradi huo iliyowasilishwa na Jeshi la Polisi.

Mh. Hilary alisema kuwa majukumu ya kamati hiyo yatakayoongozwa na Mwenyekiti wake Mh. Josephat Asunga ni k...uwa kamati hiyo ndogo itafanya uchunguzi kwa muda wa siku 30 sambamba na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Ameongeza kuwa uchunguzi huo utafanywa kwa mtindo wa kikachero na ule wa kushtukiza, ili kukwepa hali ya kuandaliwa kwa mazingira ya kuficha ukweli.

GAIDI MWANDAMIZI WA AHRAR AL SHAM AUAWA HUKO SYRIA.











GAIDI MWANDAMIZI WA AHRAR AL SHAM AUAWA HUKO SYRIA.

Kamanda mwandamizi wa kundi la kigaidi la Ahrar al-Sham lenye mafungamano na mtandao wa kimataifa wa al-Qaeda ameuawa katika hujuma ya bomu iliyolenga ngome za kundi hilo katika mkoa wa Idlib, kaskazini magharibi mwa Syria.
Majid Hussein al-Sadeq pamoja na magaidi wengine watatu waliuawa katika shambulio la jana Jumamosi dhidi ya mji wa Binnish, unaohesabiwa kuwa moja ya ngome za magaidi hao, yapata kilomita 10 kaskazini mashariki mwa mkoa wa Idlib.
Julai mwaka jana, kamanda mwingine mkuu wa kundi la kigaidi la Ahrar al-Sham kwa jina Abu Abdu Rahman Salqin aliuawa katika shambulio jingine la bomu katika eneo la Abu Talha, mkoani Idlib.
Kwa muda mrefu sasa serikali ya Syria imekuwa ikisisitiza kuwa magaidi nchini humo wanapata misaada ya fedha na silaha kutoka nchi za Magharibi hasa Marekani na waitifaki wake katika eneo hili ambao ni Saudi Arabia, Qatar, Uturuki na utawala haramu wa Israel. Karibu watu nusu milioni wameshapoteza maisha tokea magaidi waanzishe kampeni ya kumuondoa madarakani Rais Bashar al Assad wa Syria mwaka 2011.
Hii ni katika hali ambayo, Steffan de Mistura, Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria amesema watu wapatao laki nne wamepoteza maisha kutokana na vita vya zaidi ya miaka mitano vilivyoikumba nchi hiyo ya Kiarabu.

ALIYEMTUSI MTUME MUHAMMAD(S.A.W) AUHUKUMIWA KIFO MAURITANIA.


Mahakama ya Rufaa ya Mauritania imepasisha hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi aliyemvunjia heshima Mtume Muhammad (saw).

Shirika la Habari la Kimataifa la Qur'ani (IQNA) limeripoti kuwa, Mahakama ya Rufaa ya mji wa Nawadibo huko kaskazini magharibi mwa Mauritania imepasisha hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi Muhammad Sheikh Ould Amkhtir wa nchi hiyo kwa sababu ya kuandika makala iliyomvunjia heshima na kumtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad (saw) hapo mwaka 2014.

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mauritania ambaye aliomba kutolewe hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi huyo amesema kuwa kunyongwa kwake kutakuwa somo kwa wale wote wanaothubutu kumvunjia heshima Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Kuchapishwa kwa makala ya mandishi Muhammad Sheikh Ould Amkhtir hapo mwaka 2014 kulisababisha maandamano makubwa kote Mauritania ambayo hayakutulia ila baada ya kutolewa hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi huyo.

UMOJA WA ULAYA HAUTAMBUI UMILIKI WA ISRAELI KWA MIINUKO YA GOLAN.


Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, umoja huo hauutambui rasmi umiliki na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa miinuko ya Golan ya Syria.

Federica Mogherini amesisitiza kuwa, Umoja wea Ulaya hautambui ukaliaji mabavu wa Israel dhidi ya ardhi za Palestina baada ya vita vya mwaka 1967 na kuongeza kuwa, huu ni msimamo wa Umoja wa Ulaya na nchi wanachama wa umoja huo.

Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema hayo siku chache baada ya utawala wa Kizayuni wa Israel kudai kwamba, miinuko ya Golan ya Syria ni sehemu ya ardhi ya utawala huo.

Waziri Mkuu wa utawala huo, Benjamin Netanyahu alinukuliwa hivi karibuni akidai kwamba, miinuko hiyo ya Golan daima itakuwa sehemu isiyotenganishika na utawala huo.

Utawala ghasibu wa Israel uliikalia kwa mabavu sehemu ya miinuko ya Golan ya Syria mwaka 1967 katika vita vyake na Waarabu. Mwaka 1981, utawala huo wa kimabavu uliiunganisha sehemu hiyo na ardhi unazozikalia kwa mabavu, hatua ambayo hakuna wakati ilitambuliwa rasmi na jamii ya kimataifa.

WATU 13 WAFA CONGO DRC KWA MAPIGANO KATI YA SERIKALI NA WAASI.


Watu wasiopungua 13 wamepoteza maisha katika mapigano baina ya jeshi la serikali na kundi la wanamgambo eneo la mashariki mwa nchi hiyo.

Duru za usalama nchini humo zimeripoti kuwa, katika mapigano hayo watu 12 waliouawa ni wanamgambo, na mwingine mmoja ni askari wa serikali. Aidha jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limeongeza kuwa, mbali na idadi hiyo kuuawa, wengine kadhaa wamejeruhiwa.

Kwa mujibu wa ripoti, mapigano hayo yamejiri katika eneo la Biakato, mashariki mwa nchi hiyo na kwamba wanamgambo hao ni wanachama wa kundi la Mai-Mai. Mwishoni mwa mapigano hayo askari wa serikali walifanikiwa kudhibiti silaha za wanamgambo hao waliokimbia na kuacha silaha zao hizo. Jeshi la serikali pia limetangaza kuhitimisha shughuli za wanamgambo wa waasi katika eneo hilo la Biakato.

Ni miaka 20 sasa tokea eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo lianze kushuhudia hujuma za wanamgambo wanaoipinga serikali ya Kinshasa, huku wahanga wakuu wakiwa ni raia wa kawaida.

DAESH WATUMIA SILAHA ZA SUMU HUKO IRAQ.


Wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh, wametumia silaha za kemikali katika maeneo ya raia kaskazini wa Iraq.

Shambulizi hilo limefanywa katika eneo la Abu Shit wanapoishi idadi kubwa ya Wakurdi katika viunga vya mji wa Mosul, kaskazini mwa Iraq ambapo magaidi hao wametumia maguruneti yenye silaha hizo zilizopigwa marufuku. Kwa mara kadhaa sasa wanachama wa kundi hilo la kitakfiri wamekuwa wakitumia silaha zenye gesi ya sumu katika maeneo ya raia wa kawaida na kuua idadi kubwa ya watu. Katika hatua nyingine, Abdul-Muhsin al-Abbasi, mmoja wa makamanda wa jeshi la Iraq ametangaza kuwa, askari wa nchi hiyo kwa kushirikiana na wapiganaji wa kujitolea, wamefanikiwa kukomboa vijiji kadhaa vya mkoa wa al-Anbar, magharibi mwa nchi.

Katika operesheni hizo, jeshi la Iraq limemuua kiongozi wa ngazi za juu kabisa wa kundi la Daesh aliyekuwa akiitwa Yassin al-Khalifawi, maarufu kwa jina la Da'fasah, akiwa pamoja na viongozi wengine wa genge hilo la kigaidi. Aidha askari wa Iraq pia wamedhibiti silaha na zana kadhaa za kijeshi zilizokuwa zikitumiwa na matakfiri hao maarufu kwa kutenda jinai dhidi ya binaadamu.

Hayo yanajiri katika hali ambayo, ndege za kijeshi za Uturuki kwa mara nyingine tena zimefanya mashambulizi kadhaa ndani ya ardhi ya Iraq katika maeneo ya wapiganaji wa Kundi la PKK ambao wamekuwa wakipambana na wapiganaji wa Daesh nchini humo. Hii si mara ya kwanza kwa ndege za Uturuki kuvuka mipaka yake na kutekeleza hujuma zake nje ya nchi hiyo, suala ambalo limekuwa likilaaniwa na serikali kuu ya Baghdad.

MAHAKAMA KENYA YAFUTA KIFUNGU CHA MATUSI KATIKA SHERIA YA MTANDAO YA NCHI HIYO.


Mahakama Kuu jijini Nairobi imeamua kwamba Kifungu cha Sheria ambacho kimekuwa kikitumiwa kuwafungulia mashtaka watu kuhusiana na ujumbe kwenye simu na mitandao ya kijamii Kenya ni haramu.
Jaji wa Mumbi Ngugi alisema kifungu hicho, cha kutumia vibaya kifaa cha mawasiliano, kinakiuka katiba.
Kifungu hicho nambari 29 katika Sheria ya Habari na Mawasiliano Kenya Nambari 3 ya 1998 hupendekeza faini ya Sh50,000 au kifungo cha miezi mitatu jela, au adhabu zote mbili, kwa mtu anayepatikana na hatia.
Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) na Mwanasheria Mkuu walikuwa wametetea sheria hiyo wakisema ililenga kulinda sifa za wengine.
Jaji Ngugi alisema maelezo ya kifungu hicho ni mapana sana na pia baadhi ya makosa yanayolengwa kwenye kifungu hicho yameangaziwa katika sheria nyingine.
Aidha, alisema hakijatimiza matakwa ya Kipengele 24 cha Sheria ambacho kinaeleza ni katika hali gani ambapo haki za kimsingi zinaweza kubanwa. Aidha, alisema kifungu hicho kinakiuka Kipengele nambari 33 cha Katiba.
“Iwapo lengo ni kulinda sifa za watu wengine, basi hilo limeangaziwa kwenye sheria ya kuwaharibia sifa watu wengine,” Jaji Ngugi alisema kwenye uamuzi wake.
Jaji huyo alitaja mfano wa kesi tofauti dhidi ya mwanablogu mmoja ambaye aliamriwa kulipa Sh5 milioni na mahakama baada ya kushtakiwa chini ya sheria za kuwaharibia watu sifa.
Jaji Ngugi alikuwa akitoa uamuzi katika ombi la mwanablogu Geoffrey Andare aliyekamatwa Aprili 2015 na kufunguliwa mashtaka ya kutumia vibaya kifaa cha mawasiliano kutokana na ujumbe alioandika kwenye mitandao ya kijamii.
Mlalamishi alipinga mashtaka hayo akisema sheria hiyo inabana uhuru wa kujieleza mtandaoni.
Jaji alisema DPP hawezi kuendelea na kesi hiyo kwa msingi wa sheria hiyo.
Wakenya mtandaoni wamefurahia hatua hiyo ya Jaji Ngugi na tangu jana jioni jina lake limekuwa likivuma kwenye Twitter.
Kuna wanaomsifu kwa kutetea uhuru wa wananchi kujieleza lakini wengine wanahisi kwamba amekuwa akiharamisha vifungu vingi sana vya sheria.
Mfano ni Stephen Wambua anayesema uamuzi wa jaji huyo unafaa kuwekwa kwenye kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness Book of World Records.

MAJASUSI WA ISRAELI WAUAWA GAZA.


Majasusi watano wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamehukumiwa adhabu ya kifo katika Ukanda wa Gaza.

Afisa mmoja wa mahakama ya Palestina amesema kuwa Mahakama Kuu ya Kijeshi ya Ukanda wa Gaza imewahukumu kifo wakazi watatu wa eneo hilo na wengine wawili wa kambi ya al Nasirati baada ya kupatikana na hatia ya kufanya ujasusi kwa maslahi ya Israel.

Hukumu hiyo imetolewa siku chache baada ya majasusi wengine kadhaa wa Israel kunyongwa katika eneo hilo la Ukanda wa Gaza.

Kabla ya shambulizi lolote dhidi ya watu wa Gaza, Israel imekuwa ikipokea habari za kijasusi kuhusu maeneo ya wapigania ukombozi wa Kipalestina kutoka kwa vibaraka wake katika eneo hilo na baadaye kushambulia eneo hilo linalozingirwa.

Vilevile ripoti zinasema kuwa, magari yanayotolewa kama zawadi au msaada na baadhi ya nchi za Kiarabu kwa maafisa wa makundi ya mapambano ya Palestina yamegundulika kuwa na zana makhsusi za kufuatilia nyendo zao na kwamba Israel inatumia zana hizo kuwaua kigaidi viongozi na wanaharakati wa Palestina.

WANA NDOA WENYE SARATAN HUISHI MAISHA MAREFU ZAIDI KULIKO WASIO NA NDOA.

Utafiti wa Marekani waonesha ndoa inasaidia kurefusha wagonjwa wa saratani

Utafiti uliotolewa katika jarida la Saratani la Marekani umeonesha kuwa wagonjwa wa saratani waliofunga ndoa wanaweza kuishi maisha marefu zaidi kuliko wale wasiofunga ndoa.
Watafiti kutoka taasisi ya kinga ya saratani ya jimbo la California ya Marekani na chuo kikuu cha California walitafiti watu wazima laki 8 hivi waliothibitishwa kupata saratani kutoka mwaka 2000 hadi 2009, na kufuatilia hali zao hadi kufikia mwaka 2012.
Matokeo yameonesha kuwa kiwango cha vifo cha wagonjwa wasiofunga ndoa ni juu kuliko waliofunga ndoa. Kati ya wagonjwa wa kiume, kiwango cha vifo cha wagonjwa wasiofunga ndoa ni asilimia 127 ya kile cha waliofunga ndoa; kwa upande wa wagonjwa wa kike, ni aislimia 119 ya kile cha waliofunga ndoa.

Watafiti wamesema, chanzo cha tofauti hiyo hakiwezi kuelezwa kwa hali ya kiuchumi ya wagonjwa, kama vile kama amenunua bima ya kiafya ama anaishi katika sehemu yenye hali nzuri ya kiuchumi.

Pia wamesema, uungaji mkono wa kijamii ni nguvu muhimu ya kurefusha maisha ya wagonjwa wa saratani. Hivyo ndoa inaleta athari nzuri kwa afya za wagonjwa hao. Watafiti wanashauri kuwa madaktari wanapowatibu wagonjwa wasiofunga ndoa, wanatakiwa kuuliza katika mtandao wao wa kijamii kama kuna mtu anayeweza kutoa msaada katika afya na saikolojia au la.

WAISLAMU UFARANSA WAZIDI KUBAGULIWA.


Utafiti mpya unaonesha kuwa, Waislamu nchini Ufaransa, wanazidi kubaguliwa kiasi kwamba wana nafasi ndogo sana ya kupata kazi ikilinganishwa na raia wengine wa nchi hiyo ya Ulaya.

Taasisi ya utafiti ya Montaigne imeripoti kuwa, fursa ya Waislamu ya kuweza kupata kazi wakati wa mahojiano ni ndogo sana ikilinganishwa na raia wa dini nyinginezo wa Ufaransa.

Serikali ya Ufaransa ambayo hadi hivi sasa imeshindwa kupambana na wimbi la fikra na misimamo mikali dhidi ya jamii ya Waislamu, imeanzisha kampeni maalumu inayojulikana kwa jina la "Uwezo Kwanza" ili kukabiliana na ubaguzi hasa katika sekta ya kuajiri watumishi wa umma. Kampeni hiyo inayoanza leo Jumanne inatarajiwa kudumu kwa muda wa siku 15.

Waziri wa Kazi wa Ufaransa, Myriam El Khomri amesema, ubaguzi wanaofanyiwa Waislamu nchini Ufaransa hauna uhusiano wa moja kwa moja na siasa za uajiri za serikali, lakini baadhi ya wakati kunachukuliwa misimamo nchini humo ambayo inawaathiri Waislamu.

Taasisi ya Montaigne ilianzishwa mwaka 2000 mjini Paris na wajumbe wa taasisi hiyo ni viongozi wa ngazi za juu wa mashirika, vyuo vikuu na wajumbe wa jamii ya kimataifa. Taasisi hiyo ya utafiti inafanya kazi ya kutathmini siasa za serikali ya Ufaransa, masuala ya kiuchumi pamoja na mifungamano ya kijamii.

Ufaransa ina karibu Waislamu milioni tano ikiwa ndiyo nchi yenye idadi kubwa ya Waislamu barani Ulaya.

WAKRISTO WAJIFUNZA UISLAMU KATIKA MAKANISA HUKO MAREKANI.


Licha ya kuongezeka vitendo vya chuki dhidi ya Waislamu nchini Marekani, baadhi ya makanisa ya nchi hiyo yameamua kuitisha vikao mbalimbali vya kujifunza na kuutambua vizuri Uislamu.
Shirika la habari la RASA liliripoti jana Jumatatu kwamba, makanisa ya mji wa Albuquerque katika jimbo la New Mexico huko Marekani, wameandaa ratiba maalumu za kuutambulishwa Uislamu kwa wafuasi wa dini nyinginezo hususan Wakristo.

Ratiba hizo ambazo zimepata umaarufu wa jina la Hotuba za Wanawake Waislamu, wanawake wa tamaduni na dini tofauti wameamua kukusanyika katika makanisa na kujifunza, kuuliza maswali na kujadiliana mambo mbalimbali kuhusu Uislamu ikiwa ni pamoja na kuhusiana na maisha ya Waislamu hususan wanawake Waislamu wa Marekani.

Imepangwa kuwa, ratiba kama hizo zifanyike pia katika makanisa mengine matatu ya jimbo hilo.

Chuki dhidi ya Uislamu zimeongezeka sana huko Marekani, suala ambalo limewafanya wafuasi wa dini nyinginezo hasa Wakristo wadadisi na wapate hamu ya kuujua zaidi Uislamu kutoka kwa Waislamu wenyewe.

WATU 38 WAFA KWA MAFURIKO HUKO AFGHANISTAN.


Watu wasiopungua 38 wamefariki dunia kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kali iliyonyesha maeneo ya kaskazini mwa Afghanistan.

Maafisa wa serikali ya Afghanistan wamesema vifo hivyo vimeripotiwa katika mikoa ya kaskazini ya Takhar, Badghis na Samangan katika mafuriko yaliyoanza Jumapili usiku.

Mkurugenzi wa majanga ya kimaumbile katika mkoa wa Takhar, Abdul Razaq Zinda, amesema watu 13 wakiwemo watoto walifariki katika wilaya za Kalafgan na Bangi.

Aidha amesema, nyumba kadhaa hasa zile zilizojengwa kwa matofali ya udongo ziliharibiwa na mvua kali.

Msemaji wa polisi ya mkoa wa Badghis amesema watu 19 walifariki wilayani Muqur.

Mafuriko yameua pia watu wengine sita ambao ni wanawake watatu na watoto watatu mkoani Samangan na kubomoa nyumba zipatazo 20 na ekari zisizopungua tano za kilimo.

Mvua kali zimeukumba mji mkuu wa Afghanistan, Kabul lakini hakuna maafa makubwa yaliyoripotiwa.

ISRAELI YATETEA KITENDO CHAKE CHA KUKALIA MIUNUKO YA GOLAN YA SYRIA.


Licha ya kuweko upinzani wa jamii ya kimataifa dhidi ya umiliki wa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa eneo la miinuko ya Golan ya Syria unayoikalia kwa mabavu, lakini Waziri Mkuu wa utawala huo, Benjamin Netanyahu amedai kuwa, miinuko hiyo ya Golan daima itakuwa sehemu isiyotenganishika na utawala huo.

Akizungumza siku ya Jumapili katika kikao cha baraza la mawaziri kilichofanyika kwa mara ya kwanza katika eneo la miinuko ya Golan, Benjamin Netanyahu sanjari na kusisitiza juu ya mamlaka ya utawala huo kwa eneo hilo la Syria amesema kuwa, katu Israel haitasalimu amri mbele ya mashinikizo ya kimataifa.

Akiendelea na matamshi yake ya kichochezi kuhusiana na miinuko ya Golan inayokaliwa kwa mabavu na Israel Netanyahu ameitaka jamii ya kimataifa iutambue rasmi umiliki wa Israel kwa miinuko hiyo.

Utawala ghasibu wa Israel uliikalia kwa mabavu sehemu ya miinuko ya Golan ya Syria mwaka 1967 katika vita vyake na Waarabu. Mwaka 1981, utawala huo wa kimabavu uliiunganisha sehemu hiyo na ardhi unazozikalia kwa mabavu, hatua ambayo hakuna wakati ilitambuliwa rasmi na jamii ya kimataifa.

Matamshi hayo ya Netanyahu anayatoa katika hali ambayo, hivi karibuni vyombo vya habari vya Israel vimeripoti mara kadhaa kuhusiana na kihoro na wasiwasi wa viongozi wa utawala huo juu ya kurejea eneo hilo katika milki ya Syria.

Sambamba na duru mpya ya njama za Israel za kutaka kujitanua na kuzikalia kwa mabavu ardhi za Mashariki ya Kati, Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Syria imemwandikia barua Katibu

ROBOTI LENYE HISIA ZA KIBINADAMU LATENGENEZWA CHINA.


Je unaweza tambua roboti kati ya hawa watu kwa hizi picha ? Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia ya China katika mji mkuu wa Hefei, mashariki mwa China  kimezindua roboti kwa jina "Jiajia" ambayo ina uwezo wa mwingiliano na binadamu.

Jiajia ni huyo mwenye mwanamke mwenye nguo nyekundu, anaweza kila kitu ambacho mwanamke anaweza kasoro kubeba mimba tu, lakini hisia za kupenda na kuchukia, hisia za kulala na mwanaume na mengi kama hayo.

Roboti hizo zinauwezo wa kutongoza au kutongozeka, zinaweza kukataa au kukubali inategemea na uwezo wako wa kushawishi.

Bado bei yake haijapangwa, na yapo yanayotengenezwa maalum kwaajili ya Afrika, je yakija Tanzania utanunua?? yakiume pia yatatengenezwa kwaajili ya kazi mbalimbali kama kulima nk.

Watu watabisha lakini mbona wanakula mayai kizungu, kuku za kizungu, sasa kuna ubaya gani mkila na nyapu/zakari za kichina? Au wachina hamuwaamini?

TANZANIA NI YA PILI KWA UZALISHAJI BANGI KWA WINGI AFRIKA.


Polisi nchini Tanzania wameendeleza oparesheni dhidi ya ukuzaji wa bangi pamoja na biashara yake kwenye eneo la Arusha.

Oparesheni hiyo inaendelezwa huku ripoti ya Umoja wa Mataifa ikionyesha kuwa Tanzania ndio mzalishaji mkuu wa pili wa bangi barani Afrika.

Kamanda wa polisi kwenye eneo la Arusha Charlse Mkumbo amesema oparesheni hiyo italenga biashara na ukuzaji wa bangi na miraa.

TETEMEKO LINGINE LIMETOKEA JAPANI.

TETEMEKO LINGINE LIMETOKEA JAPANI.

Tetemeko lignine la ardhi lenye nguvu ya 7.3 kwenye vipimo vya Richter limetokea nchini Japan na kuuwa watu 19 na kusababisha uharibifu mkubwa hayo ni kwa mujibu wa mamlaka nchini humo.  

Tetemeko hilo  lilikukumba kisiwa cha Kyushu ndani ya siku mbili, na kusa sababisha kuporomoka kwa majengo, barabara, mifumo ya maji na umeme.
Wanajeshi 20,000 wametumwa kusaidia juhudi za uokoaji lakini jitihada za uokoaji zimetatizwa na mitetemeko mingine midogo midogo.

Hivi majuzi lilitokea tetemeko Kumamoto hukohuko Japan na kuleta uharibufu na kuua watu, hili sasa lingine, nchi ya Japan inakumbwa na majanga haya kwa mara na kupelekea nchi hiyo kuwa na sheria kali za ujenzi.

GAVANA HUKO MAREKANI ALIGIZA HELKOPTA KUBEBA WALLETI YAKE.


Helikopta ya polisi ilitumwa kuchukua pochi ya gavana wa jimbo moja nchini Marekani, safari iliyogharimu $4,000 (£2,800), uchunguzi umebaini.

Kisa hicho kilitokea mwishoni mwa 2014.
Gavana wa Alabama Robert Bentley aliondoka Tuscaloosa kuelekea kwenye nyumba yake ya ufukweni, mwendo wa saa tano hivi ukitumia gari, lakini akasahau pochi yake.

Aliwataka maafisa wake wa usalama kwenda kuchukua pochi hiyo. Maafisa hao walitumia helikopta hiyo ya polisi, rekodi za safari za ndege zimeonesha.
Bw Bentley anakabiliwa na shinikizo za kumtaka ajiuzulu kutokana na sakata ya unyanyasaji wa kingono.

Lakini anasema hakuagiza ndege itumiwe kwenda kuchukua pochi.
"Niliwaomba tu waende wakachukue pochi yangu, sikuwaambia watumie njia gani,” gavana huyo ameambia mtandao wa AL.com.

„Sikuwaambia watumie helikopta. Ni lazima uwe na pochi yako kwa sababu za kiusalama. Mimi ni gavana. Na ni lazima niwe na pesa. Ni lazima ningenunua kitu cha kula. Na nilihitaji vitambulisho vyangu.”

Tovuti ya AL.com inasema safari hiyo ya helikopta iligharimu mlipa kodi takriban $4,000 (£2,800).

IRAN YAJITAMBA KUWA NA JESHI IMARA NA LENYE NGUVU.

IRAN YAJITAMBA KUWA NA JESHI IMARA NA LENYE NGUVU.

Luteni Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu la Iran amesema kuwa, jeshi hilo liko imara katika kuyalinda Mapinduzi ya Kiislamu na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
Shirika la habari la IRNA limemnukuu Brigedia Jenerali Kiumars Heidari akisema hayo wakati huu wa kukaribia Siku ya Jeshi nchini Iran.

Ameongeza kuwa, jeshi la Iran halizembea hata sekunde moja kuulinda Uislamu na Mapinduzi ya Kiislamu na kwamba kusimama kwake huko imara kunathibitishwa na jinsi jeshi hilo lilivyo na fakhari ya kutoa mashahidi 48 elfu katika njia ya haki.

Brigedia Jenerali Kiumars Heidari ameongeza kuwa, jeshi la Iran lina tofauti kubwa na majeshi ya nchi nyingine duniani na kusisitiza kuwa, leo hii jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limekuwa mtetezi mkubwa wa wanyonge na watu wanaodhulumiwa duniani na limesimama imara kukabiliana na waistikbari na mabeberu na ndio maana linapendwa na linakubalika.

Ikumbukwe kuwa kesho Jumapili inayosadifiana na tarehe 17 Aprili ni siku ya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka kwa ratiba tofauti.

MALALAMIKO YA WAZIMBABWE KWA SIASA ZA MUGABE.


Wananchi wa Zimbabwe wamefanya maandamano kulalamikia siasa za Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo.
Karibu wafuasi elfu mbili wa chama cha upinzani cha MDC cha Morgan Tsvangirai wamefanya maandamano mjini Harare kulalamikia siasa za Rais Robert Mugabe. Akizungumza mbele ya wafuasi wake Tsvangirai amesisitiza kuwa, Mugabe ameshindwa kutatua mgogoro wa nchi hiyo na kwamba wananchi wa Zimbabwe wanaamini kuwa, serikali yake haina njia nyingine ila kuporomoka tu.

Robert Mugabe ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 92, amekuwa rais wa Zimbabwe tangu mwaka 1980. Hali yake tete ya kiafya imepelekea kuzuka maneno mengi kuhusu mtu wa kurithi kiti chake. Kumekuwa na dhana kuwa, Mugabe anafanya mpango wa kumrithisha kiti hicho mkewe, Grace Mugabe. Hata hivyo mwanzoni mwa mwezi uliopita wa Machi, Mugabe alikanusha uvumi huo na kusisitiza kuwa, rais ajaye wa Zimbabwe lazima achaguliwe kwa njia za kidemokrasia.

Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, matamshi hayo ya Mugabe yanaashiria azma yake ya kuendelea kuwa rais wa Zimbabwe hadi mwisho wa maisha yake. Katika hali ambayo duru za kisiasa za nchi hiyo zinafuatilia kwa karibu sana hali ya kiafya ya Mugabe, baadhi ya duru hizo zinaamini kuwa, hatua ya Mugabe ya kushindwa kuainisha mrithi wake itazidi kuitumbukiza katika mgogoro nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.

Hivi sasa hali ya kiuchumi ya Zimbabwe ni ya mgogoro kiasi kwamba baadhi ya ripoti zinaonesha kuwa Zimbabwe ndiyo nchi maskini zai

MAKUMI YA RAIA WAMETIWA MBARONI KWA MAANDAMANO KUMPINGA RAIS WA GAMBIA.


Makumi ya raia wametiwa mbaroni nchini Gambia katika maandamano yaliyofanyika jana ya kumpinga Rais Yahya Jammeh wa nchi hiyo.
Jana maelfu ya wananchi wa Gambia walifanya maandamano wakimpinga Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh.

Maandamano hahayo yalikandamizwa na vikosi vya usalama huku makumi ya waandamanaji wakitiwa mbaroni. Habari kutoka Gambia zinasema kuwa, maandamano hayo ni makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini humo.

Waandamanaji wakiwa wamebeba mabango na maberamu walipiga nara wakipinga sera za Rais huyo na kutoa wito wa kufanyika mageuzi ya kisiasa.

"Wananchi wa Gambia Wanataka Mageuzi ya Kisiasa" ni moja ya maandishi yaliyoonekana katika maberamu yaliyokuwa yamebebwa na waandamanaji hao. Baadhi ya waandamanaji hao wamesema kuwa, Rais jammeh ndio sababu ya hali mbaya ya kiuchumi inayoikabili nchi hiyo.

Baadhi ya waandamaji waliotiwa mbaroni wanaripotiwa kupigwa na kuteswa na vikosi vya usalama baada ya kutiwa mbaroni.

Baadhi ya ripoti zinasema kuwa, Rais Yahya Jammeh aliyekuwa nchini Uturuki kushiriki mkutano wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC amekatisha safari yake yake hiyo na kurejea Gambia.

Rais Jammeh amekuwa akiongoza Gambia kwa mkono wa chuma tangu mwaka 1994.

UNICEF: BOKOHARAM INAWATUMIA KINGONO WASICHANA WA CHIBOK

Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, anayehusika na masuala ya magharibi na katikati mwa Afrika amesema kuwa, wasichana wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haram wanabakwa na kudhalilishwa kijinsia na wanamgambo wa kundi hilo.

Manuel Fontaine amesema hayo leo na kuongeza kuwa, wanawake na wasichana wanaotoroka kutoka mikononi mwa kundi hilo maarufu kwa kutenda jinai dhidi ya binaadamu, wameelezea namna wanachama wa kundi hilo walivyokuwa wakiwabaka na kuwalazimisha kutenda vitendo vya ngono bila ya wao kupenda. Kwa mujibu wa wasichana hao, makamanda wa genge hilo walikuwa pia wakiwapatia mafunzo ya kujiripua kwa mabomu. Hii ni katika hali ambayo, ripoti zilizotolewa mwezi Mei mwaka jana zilieleza kuwa, robo tatu ya mashambulio yaliyofanywa na kundi la Boko Haram kuanzia mwaka 2014, yalifanywa na watoto wadogo waliopatiwa mafunzo na magaidi hao.

Ni miaka miwili sasa imepita tangu magaidi hao walipowateka nyara wasichana wa shule moja ya serikali katika mji wa Chibok, kaskazini mashariki mwa Nigeria, huku jamii ya kimataifa ikitaka kuachiliwa huru mara moja wasichana hao.

WAPELISTINA WAANDAMANA KUPINGA UKATILI WA ISRAELI.


Wapalestina wa maeneo tofauti ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan wamefanya maandamano makubwa ya kulaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.

Mwandishi wa shirika la habari la IRIB ameripoti kuwa, jana Ijumaa mamia ya wananchi wa Palestina walifanya maandamano katika maeneo tofauti ya Ukingo wa Magharibi wakiutaka utawala wa Kizayuni wa Israel ukomeshe mara moja ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi wanazoporwa Wapalestina.

Waandamanaji hao walipiga nara dhidi ya ya Israel na wametangaza uungaji mkono wao kwa muqawama na Intifadha ya kupambana na utawala wa Kizayuni.

Wanajeshi wa Israel waliwavamia na kuwashambulia kwa risasi waandamanaji hao na kujeruhi Wapalestina kadhaa.

Wakati huo huo mamia ya Wapalestina wamekusanyika mbele ya jengo la Shirika la Msalaba Mwekundu katika Ukanda wa Ghaza wakitaka kuachiliwa huru Wapalestina wenzao wanaoshikiliwa mateka na utawala wa Kizayuni.

Hivi sasa kuna karibu Wapalestina elfu saba wanaoshikiliwa mateka na utawala wa Kizayuni wa Israel katika jela za kuogofya za utawala huo dhalimu.

MISRI: MAANDAMANO YA WANANCHI TISHIO KWA SERIKALI.


Wizara ya Mambo ya Ndani nchini Misri imetaka polisi kuchukua hatua za dharura kwa ajili ya kuzima kwa njia yoyote ile, maandamano ya wananchi wanaopinga hatua ya Rais Abdel Fattah el-Sisi kumpa visiwa viwili vya nchi hiyo Mfalme Salman wa Saudi Arabia.

Afisa mmoja wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Misri ambaye hakutaka kutaja jina lake, amesema kuwa, kufuatia amri hiyo, polisi wameimarisha doria katika kila kona na barabara kubwa, kwa lengo la kuzuia maandamano hayo ya wananchi. Hii ni katika hali ambayo siku chache zilizopita, Wizara hiyo ya Mambo ya ndani ya Misri ilionya juu ya kuendelezwa maandamano hayo ya kupinga kitendo cha rais wa nchi hiyo cha kuipa Saudia visiwa viwili vya Sanafir na Tiran vilivyoko katika Ghuba ya Aqaba.

Jana pia maandamano makubwa yalifanyika katika maeneo tofauti ya Misri, ambapo polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji. Inafaa kuashiria hapa kwamba, hivi karibuni serikali ya majenerali wa kijeshi ya Misri imeipa serikali ya Saudia visiwa hivyo viwili vya Bahari Nyekundu kwa madai kuwa, upimaji mipaka uliofanywa umeonyesha kuwa, tangu awali visiwa hivyo vilikuwa katika maji ya Saudia, suala ambalo limetajwa na Wamisri kuwa ni usaliti. Tayari vyama na harakati za kisiasa nchini Misri kwa pamoja vimelaani vikali udhaifu wa Rais Abdel Fattah el-Sisi mbele ya Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud wa Saudia.

UISLAMU NA UKRISTO UMEWATIA UJINGA WAAFRIKA.


Pamoja na uislamu wangu, lakini sitaweza kubeza au kudharau mila na desturi yangu ya kiafrika.

Kuna watu wana mawazo kitumwa, kikoloni, na kijinga, kwao wao uafrika na mila zake ni ushenzi na dalili ya kutokusoma na kustaharabika.

Mtu anabeza na kumdharau na kumuona mshenzi au shirikina mvaa hirizi, lakini anamuona mstaharabu na mwenye maana sana mtembea na bible au quran kwapani. Hivi anayekwenda kuomba kanisani apate kazi ana tafauti gani na yule anayekwenda mzimuni kufanya hivyo pia?

Hivi mchungaji anaposema na kutabiri juu ya kesho au anapoona mambo yako ya rohoni ana tafauti gani babu au bibi yangu wa mzimuni anayetabiri kwa mizimu? Kwanini utabiri wa mzimuni uitwe ramli na ushetani lakini utabiri wa kanisani uitwe maono na utukufu? Kwanini?

Alikadhalika yule mwenye kutambika katika mizimu ama miungu ya kwao anaonekana ni mtu wa kizamani au mtu anaye ishi maisha ya kijima, maisha kale, lakini yule anayekesha msikitini au kanisani ndio mjanja na mtu aliyestaharibika. Eeh Afrika yangu, nalia uafria wangu, hivi kuna tafauti gani kati ya kukesha msikitini na kukesha mzimuni?

Kuna tafauti gani ya kwaya na mapambio ya kumsifu Yesu na madogori au lewa za kwetu? Hivi nini hasa tafauti? Kama tafauti ni moja, hizi kwaajili ya Yesu na zile kwaajili ya Mizimu, lakini lengo na matarajio ni yaleyale. Anayekwenda mzumuni kuomba baraka hana tafauti na mwenda kanisani kuomba baraka. Kama tafauti ni moja kanisani anaombwa Yesu na mzimuni anaombwa mzimu, lakini matarajio ni yaleyale.

Kwa jinsi waafrika tunavyo zipamba, na kuzipigania dini za kigeni imepita kiasi wenye dini zao watuone wajinga, wapumbavu, na watu tusio kuwa na asili wala kwetu. Waafrika wa nchi ya AFRIKA YA KATI wameuana kisa uislamu na ukristo, huko Nigeria hakuna salama kisa uislamu na ukristo, hivi ninyi waafrika ni wapi wazungu wanapigana vikumbo sababu ya uafrika? kwanini sisi tuwe tunajipendekeza kwao kwa kiwango hiki?

Sema msemavyo, lakini hakuna anayepinga hapa kuwa ukristo ni utamaduni wa kizungu, Yesu katiwa mle tu ili watu wengi wavutike, pia uislamu utamaduni wa kiarabu na uyaudi wenyewe wayaudi. Kama Afrika tungetawaliwa na mchina au mhindu, sasa hivi tungekuwa mabudha au wahindu, yaani, ni bendera fuata upepo, ng'ombe ambaye kitoweo kwetu angekuwa Mungu wetu na tungejitoa muhanga kupambana na wala ng'ombe, sisi tunafuata matakwa ya wanao tutawala.

Wewe huna utamaduni wako kiasi ukubali kujitoa mhanga kisa dini? kiasi udharau uafrika wako na utamaduni wako? Nilisikitika sana Mzee Kingunge alivyokwenda kuwakilisha dini za jadi bunge la katiba watu katika mitandao walimdhihaki kwa maneno ya hovyo kabisa, lakini wakati huohuo katika bunge hilo kulikuwa na mashekhe na mapadri walio wakalisha dini zao na hakuna yeyote aliyethubutu kuwasumbua, tena watanzania wa dini hizi mbili walitamani bunge la katiba lijae mashekhe na mapadri kama vile tunaenda kuandika MSETO WA QURAN NA BIBLIA.

Pia naomba mjue hakuna uhusiano wowote kati ya mauaji ya vikongwe, albino na mambo ya kufananayo na dini za asili au tambiko za mzimuni. Hiyo ni sawa na Padri au Shekhe kuwa shoga kisa ukauhukumu uislamu au ukristo wote kwa kosa moja la ushoga. Na hata ukichunguza dini za uslamu na ukristo zimepoteza maisha ya watu wengi sana hadi kukufikia wewe, wapo waliotolewa sadaka na Mungu wa kikristo ili ukristo ukufikie, kwa hivyo utagundua dini zote zina historia mbaya ya kutoa kafara za ajabu na kutoa adhabu za kuua, kafara na adhabu ambazo kwa wakati wetu huu ni kinyume cha utu na ubinadamu.

Acheni dharau, acheni ujinga, acheni ulimbukeni, acheni upumbavu!

WAAFRIKA TUNA MAMBO.                                           
1.
Mwajua mimi sijambo, namshukuru manani,
Nimeamka kitambo, shafika kibaruani,
Ila kuna kubwa jambo, kuuliza natamani,
Hivi nyie hamjambo? Mliopo kisimani.
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
2.
Mambo yakiwa si mambo, siweke fundo moyoni,
Kubwa sicheke utumbo, kwa maini ya jirani,
Sitaki ule makombo, kwa hamu ya biriani,
Bure taitwa mtambo, mwenye wazimu rasini.
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
3.
Kuna mambo ya mkumbo, kuyafuata acheni,
Mambo mengine urimbo, mchunge siwanaseni,
Kijana kimbie ng'ambo, nchini abaki nani?
Mwisho apigwe taimbo, kwa bata za ghaibuni.
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
4.
Memkumbuka Setembo, babu yangu wa moyoni,
Aliniusia mambo, kuwa'mbia natamani,
Rijali haumwi tumbo, wala chango kinenani,
Hakika hafanyi tambo, bila vitendo jueni,
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
5.
Nawasema wa kiambo, hata wale wa mjini.
Mlioamkia tembo, mloiota ndotoni,
Hamkuogeshwa jimbo, wakati wa utotoni,
Sawa mfanye utumbo, subuhi mko hewani,
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
6.
Twasisitiza kimombo, kiswahili taabani,
Vizuri kuiga mambo, si kila kitu jamani,
Sawa kuacha kiyombo, kwa suti za Marekani,
Kukiabudu kimombo, ni wazimu jueni.
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
7.
Kanisani kuna mambo, pia na msikitini,
Tuna itukana gombo, nalia utamaduni,
Miungu kutoka ng'ambo, Ulaya na Arabuni,
Imetupiga kikumbo, jadi haina thamani,
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
8.
Tufani yapiga sambo, istizai yafaani,
Mjue twaenda kombo, naomba zindukeni,
Sote tumelewa tembo, kutoka ughaibuni,
Sasa ni wana wa kambo, baba wa kijerumani
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
9.
Nimesema kimafumbo, hilo kwanza lijueni,
Maneno haya si shombo, ukutani andikeni,
Msiyafiche kwa rambo, hadharani yawekeni,
Jeuri ataka fimbo, awekwe sawa jamani,
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.
10.
Nimeliza la mgambo, lengo mtoke shimoni,
Ninawaita kwa wimbo, wahafidhina njooni,
Mwanagenzi nina mambo, majagina nifunzeni,
Naomba nifunge gombo, nilosema yashikeni,
Nawambia si utani. waafrika tuna mambo.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5.)
Mzalendo.njano5@gmail.com
0622845394/0762845394
Morogoro Tanzania.

KOREA KASKAZINI YASHINDWA KUFYATUA MAKOMBORA YAKE YA MASAFA YA WASTANI.


Jaribio la Korea Kaskazini kufyatua kombora la masafa ya wastani kwa jina “Musudan” katika pwani yake ya mashariki, limeshindwa, hayo ni kulingana na, maafisa wa Marekani na Korea Kusini

Shughuli hiyo ilikuwa ikifanyika siku ambayo ni ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa taifa la Korea Kaskazini Kim Il-sung.

Shirika la habari la Korea Kusini Yonhap, likinukuu duru za serikali, limesema kombora hilo lilikuwa aina ya kombora la Musudan, ambalo kitaalamu hujulikana kama BM-25.

Makombora hayo yanaweza kufika umbali wa kilomita 3,000 na kufikia kambi ya majeshi ya Marekani iliyopo kisiwa cha Guam katika bahari ya Pasifiki. Hata hivyo hayawezi kufika Marekani bara.

Hayo ni makombora ya masafa ya wastani, makombora yake ya masafa marefu yanaweza kufika Marekani, hii ina maanisha Korea Kaskazini inaweza kumchapa Mmarekani bila kuhitaji msaada wa uwanja au bahari ya nchi yeyote na Marekani.

Kama mtakumbuka, Marekani ilipigana vita Iraq kwa msaada wa nchi kama Jordan ambazo zilitoa anga na viwanja kwaajili ya matumizi ya kijeshi kwa wamarekani, kama si msaada huo vita ya Iraq isingekuwa nyepesi kwa Marekani.

Marekani na Korea Kusini ndio wanasema hilo Jaribio la Kaskazini limefeli, lakini huwez jua, bado hatuna taarifa kutoka kaskazini, sababu hii huenda ni propaganda tu za Marekani Korea Kusini.

Tusubiri Tuone.


AFIKISHWA KIZIMBANI KWA KUMTUKANA RAIS MAGUFULI FACEBOOK.




KUMAMOTO HALI BADO MBAYA.

KUMAMOTO HALI BADO MBAYA.

Watu tisa wamefariki baada ya tetemeko kubwa la ardhi kuukumba mkoa wa Kumamoto kusini magharibi mwa Japan, huku zaidi ya watu 400 wakiwa wamekimbizwa hospitalini.

Tetemeko hilo lilikuwa na kipimo cha 6.4 katika vipimo vya Richter. Habari zinasema takriban watu 23,000 walitafuta hifadhi kwenye maeneo 350 mkoani humo.

NIGERIA YASISITIZA UDHARULA WA KUPAMBANA NA UGAIDI.

NIGERIA YASISITIZA UDHARULA WA KUPAMBANA NA UGAIDI.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Nigeria imesisitiza udharura wa kuzidishwa ushirikiano unaohitajika kati ya nchi za eneo la magharibi mwa Afrika kwa ajili ya kupambana na kundi la Boko Haram.
Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema kuwa, kundi la Boko Haram katika kipindi cha miezi iliyopita limepata pigo kubwa kutoka vikosi vya majeshi ya nchi za eneo la magharibi mwa Afrika lakini inasikitisha kuona kuwa, kundi hilo lingali linaendeleza hujuma za kigaidi.

Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Nigeria imeongeza kuwa, maafisa usalama wa Nigeria, Chad na Niger hadi sasa wameshindwa kuratibu oparesheni za majeshi ya nchi hizo dhidi ya Boko Haram katika eneo hilo na hivyo kundi hilo limetumia vibaya nukta hiyo ya udhaifu.

Maafisa usalama wa nchi hizo tatu walikutana mwaka jana huko Abuja, Nigeria kwa lengo la kutathmini oparesheni zao za pamoja dhidi ya kundi la Boko Haram. Japokuwa kituo kikuu cha kundi la Boko Haram kiko huko kaskazini mashariki mwa Nigeria lakini kundi hilo limekuwa pia likifanya mashambulizi ya kigaidi katika nchi jirani.

Baadhi wa wachambuzi wa mambo wanasema kuwa, mapigano na mivutano ya ndani katika baadhi ya nchi za magharibi mwa Afrika kwa upande mmoja, na kutokuwepo uratibu baina ya nchi za eneo hilo kwa ajili ya kupambana kwa pamoja na magaidi hao ni miongoni mwa sababu za kutofanikiwa mapambano ya kuliangamiza kundi hilo.

Sisitizo la Nigeria juu ya udharura wa kuzidishwa ushirikiano baina ya nchi za magharibi mwa Afrika limetolewa huku kundi la Boko Haram likizidisha mashambulizi ya kigaidi katika nchi za eneo hilo licha ya jitihada zinazofanywa na najeshi ya nchi hizo za kukabiliana na wahalifu hao.

Katika kampeni zake za uchaguzi, Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria aliahidi kuwa atakomesha uasi wa kundi la Boko Haram. Hata hivyo hadi sasa jeshi la Nigeria halijapata mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya kundi hilo la kigaidi. Ni kutokana na hali hiyo ndipo weledi wa mambo wanaposisitiza kuwa, kuna udharura wa kuwepo ushirikiano na uratibu wa pamoja kati ya nchi zote za magharibi mwa Afrika kwa ajili ya kung'oa mzizi wa kundi hilo la kigaidi.

Kundi la Boko Haram linaendelea kuwashikia mateka mamia ya wasichana wa shule waliochukuliwa na kundi hilo miaka miwili iliyopita. Jana Jumatano wataalamu wa Umoja wa Mataifa na wataalamu wa haki za binadamu wa Afrika walitoa taarifa ya pamoja wakiashiria suala na kusema kuwa:

Imepita miaka miwili sasa ambapo wapiganaji wa kundi la Boko Haram wanaendelea kuwashikilia mateka wanafunzi wa kike wa shule ya Chibok na hadi sasa hakuna maendeleo ya aina yoyote ya kuweka wazi hali ya wanafunzi hao. Wataalamu hao wameitaka serikali ya Nigeria kuzidisha juhudi za kukomboa wasichana hao.

Kuongezeka kwa mashambulizi ya kigaidi katika maeneo mbalimbali ya dunia na kuimarika na kupanuka zaidi harakati za makundi ya kigaidi hususan katika bara la Afrika lenye utajiri wa maliasili, maeneo ya kistratijia na hitilafu nyingi za kikabila na kikaumu kumeyafanya mataifa na nchi hizo zikabiliwe na tishio kubwa la makundi kama Boko Haram na al Shabab.

Ukweli ni kwamba makundi ya kigaidi yanatishia usalama wa kimataifa na si bara la Afrika pekee, kwa msingi huo kuna udharura wa kuchukuliwa hatua za kimataifa za kukabiliana na janga hilo lisilojua mipaka ya nchi au bara makhsusi.

HUKO BURUNDI AFISA WA CNDD-FDD AUAWA

HUKO BURUNDI AFISA WA CNDD-FDD AUAWA

Afisa wa chama tawala nchini Burundi ameuawa kwa kupigwa risasi, katika kile kinachoonekana ni wimbi la makabiliano ya kulipiza kisasi dhidi ya serikali.

Damien Barindambi, mshirikishi wa wilaya katika eneo la Mutimbuza amesema Phocas Bakaza, mwanachama wa chama tawala CNDD-FDD aliuawa kwa kufyatuliwa risasi jana jioni viungani mwa mji mkuu Bujumbura. Amesema kuwa, watu wawili wamekamatwa kutokana na hujuma hizo zinazoaminika ni za kulipiza kisasi.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 400 wamekwishauawa hadi sasa, tokea Burundi itumbukie kwenye mgorogoro wa wenye kwa wenyewe Aprili mwaka jana. Wizara ya Usalama wa Umma nchini Burundi imetangaza kuendelea machafuko katika maeneo tofauti ya nchi, ambapo watu 46 wameuawa tokea mwanzoni mwa mwaka huu wa 2016 pekee.

Mwaka mmoja umetimia tangu Burundi itumbukie katika hali ya mchafukoge mwezi Aprili mwaka jana, kufuatia hatua ya chama tawala cha CNDD-FDD kumuidhinisha Rais Pierre Nkurunziza kugombea tena urais katika uchaguzi uliopita nchini humo.

MAREKANI NA NCHI ZINAZO MILIKI SILAHA ZA NYUKULIA WAPOKONYWE KUKIDHI TAKWA LA KILIMWENGU.

MAREKANI NA NCHI ZINAZO MILIKI SILAHA ZA NYUKULIA WAPOKONYWE KUKIDHI TAKWA LA KILIMWENGU.

Kupokonywa silaha za nyuklia Marekani na nchi nyingine zinazomiliki sialha hizo ni takwa na hitajio kuu la fikra za waliowengi ulimwenguni.

Gazeti la Resalat linalochapishwa mjini Tehran limeandika leo katika uchambuzi wake kuwa, kupokonywa silaha za nyuklia ni takwa ambalo nchi zinazomiliki silaha za aina hiyo, zikiongozwa na Marekani; zina hofu kubwa kuhusiana na mpango wa kutaka kutekelezwa hatua hiyo.

Gazeti la Resalat limeandika kuwa, kuwepo mamia ya vichwa vya nyuklia ni hatari kwa maisha ya mamilioni ya watu duniani na kwamba suala la kupokonya silaha za nyuklia linapasa kuwekwa katika ajenda ya kazi ya nchi mbalimbali duniani ili kudhamini usalama wa kimataifa.

Gazeti hilo linalochapishwa hapa Tehran limeendelea kuandika kuwa, nchi zinazomiliki silaha haribifu na zilizopigwa marufuku katika hatua yao inayokinzana waziwazi katika kikao cha hivi karibuni cha G-7 huko Hiroshima Japan, zimetaka kuwepo dunia pasina na silaha za nyuklia, katika hali ambayo nchi hizo hazistahiki kuzungumzia suala la kupokonywa silaha za nyuklia ulimwenguni.

Gazeti la Resalat limeongeza kuwa, hatua ya madola yanayomiliki silaha za nyuklia ya kutekelezwa miamala ya kindumakuwili kwa kupuuza maghala ya silaha za nyuklia yanayomilikiwa na utawala wa Kizayuni wa Israel, imeutia kiburi utawala huo na hivyo kutoheshimu taasisi yoyote ya kimataifa ukiwemo Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).

WAASI WA UGANDA WASHAMBULIA MASHARIKI YA DRC.

WAASI WA UGANDA WASHAMBULIA MASHARIKI YA DRC.

Watu kadhaa wameuawa na kujeruhiwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya waasi wa Uganda kufanya mashambulizi kwenye maeneo hayo.

Mtandao wa habari wa Africa Time umezinukuu duru za kijeshi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zikitangaza kuwa, wanajeshi wawili wa nchi hiyo waliuawa jana Jumanne baada ya waasi wa ADF wa Uganda kufanya mashambulizi katika mji wa Opita, kaskazini mwa mkoa wa Kivu Kaskazini, mashariki mwa Kongo na wanajeshi wengine wanne wamejeruhiwa. Hata hivyo duru hizo hazikusema chochote kuhusu hasara walizopata waasi katika mapigano hayo.

Waasi wa Uganda wanaoipinga serikali ya Rais Yoweri Museveni wako mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo tangu mwaka 1995 hadi hivi sasa. Askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Kongo pamoja na serikali ya nchi hiyo wanaamini kuwa waasi hao wa Uganda wamefanya mauaji ya raia 550 katika eneo la Beni huko Kivu Kaskazini tangu mwezi Oktoba 2014 hadi hivi sasa.

Eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetumbukia kwenye machafuko na mashambulio ya waasi kwa miaka 20 sasa. Jeshi la Kongo pamoja na askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa hadi sasa wameshindwa kudhibiti vitendo hivyo vya waasi na kuwaletea amani na usalama wakazi wa maeneo hayo.

KABURI LA PAMOJA LA WATU 350 LAGUNDULIKA KASKAZIN MWA NIGERIA.

KABURI LA PAMOJA LA WATU 350 LAGUNDULIKA KASKAZIN MWA NIGERIA.

Karibu miili 350 ya Waislamu imepatikana ikiwa imezikwa kwa siri katika kaburi la umati kaskazini mwa Nigeria.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Kano, Muhammad Namadi Musa, Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Wafuasi wa Dini Mbalimbali amesema kugunduliwa kaburi hili la umati ni ushahidi wa wazi kuwa mamia ya Waislamu waliuawa Desemba mwaka jana wakati jeshi la Nigeria lilipowashambulia Waislamu wafuasi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria katika jimbo la Zaria.

Katika tukio hilo, jeshi la Nigeria liliwafyatulia risasa wafuasi wa harakati hiyo inayoongozwa na Sheikh Ibrahim Zakzaky ambaye sasa anashikiliwa na jeshi la nchi hiyo akiwa na majeraha na risasi mwilini.

Siku ya Jumatatu mwanaharakati mmoja maarufu wa nchini Uingereza alikosoa vikali ukimya wa jamii ya kimataifa juu ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu nchini Nigeria.

Masoud Shajareh mkuu wa Tume ya Kiislamu ya Haki za Binadamu (IHRC) yenye makao yake London amesema ni miezi kadhaa sasa imepita tangu kujiri mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu nchini Nigeria ambapo hadi sasa ukatili huo haujachunguzwa.

IRAN YASEMA UWEZO WAKE MKUBWA WA KIJESHI SIO TISHIO, BALI WA KIJIHAMI NA FYOKOFYOKO ZA AINA YOYOTE.

IRAN YASEMA UWEZO WAKE MKUBWA WA KIJESHI SIO TISHIO, BALI WA KIJIHAMI NA FYOKOFYOKO ZA AINA YOYOTE.

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) linaendelea na mazoezi makubwa ya kijeshi katika eneo la kusini mashariki mwa nchi.

Luteka hiyo iliyopewa jina la Mtume Mtukufu SAW imeanza Jumanne katika mkoa wa Sistan na Baluchestan ambapo pia kumezinduliwa ndege mpya isiyo na rubani au drone ilioyotengenezwa hapa nchini na yenye uwezo mkubwa.

Drone hiyo ijulikanayo kama Hamasa inatumika kwa mara ya kwanza katika mazoezi ya jeshi baada ya uundwaji wake kutangazwa miaka miwili iliyopita. Drone hiyo ina uwezo mkubwa wa kazi za upelelezi na kurusha makombora mbali na kuwa na uwezo wa kuruka juu sana. Drone zingine zilizotengenezwa nchini Iran zinazotumika katika luteka hiyo ni pamoja na Mohajer, Ababil na Shahed.

Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha IRGC Brigedia Jenerali Mohammad Pakpour amesema mazoezi hayo ya siku tatu yatafanyika pia katika mikoa ya Kerman, Khorasan Kusini na Hormozgan.

Hivi karibuni pia vikosi vya ulinzi vya Iran vilifanya mazoezi na kufanyia majaribio zana za kisasa za kujihami. Machi 9 IRGC ilifanyia majaribio yaliyofana makombora mawili ya balistiki ya Qader-H na Qader-F. Machi nane pia Iran ilifanya majaribio yaliyofana ya kombora la Qiam.

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasisitiza kuwa uwezo wake mkubwa wa kijeshi si tishio kwa nchi yoyote bali ni kwa ajili ya kujihami.

RUSSIA YASEMA UVAMIZI WA MAREKANI HUKO LIBYA NDIO CHANZO CHA KUVURUGIKA NCHI HIYO YA AFRIKA.

RUSSIA YASEMA UVAMIZI WA MAREKANI HUKO LIBYA NDIO CHANZO CHA KUVURUGIKA NCHI HIYO YA AFRIKA.

Serikali ya Russia imesema kuwa uvamizi wa kijeshi wa Marekani huko Libya ni hatua iliyovuruga uthabiti wa nchi hiyo.
Serikali ya Russia imesema kuwa hatua ya Marekani na waitifaki wake ya kuivamia kijeshi Libya na kupelekea kung'olewa madarakani kiongozi wa nchi hiyo Muammar Gaddafi, imesababisha kugawanyika Libya.

Serikali ya Russia imeutaja uvamizi wa kijeshi wa Marekani huko Libya, kuwa ni pigo kubwa kwa nchi hiyo.

Rais Vladimir Putin wa Russia mara kadhaa alishawahi kutahadharisha kuhusu athari za kuvamiwa kijeshi Libya na kile kinachoshuhudiwa hivi sasa nchini humo.

Akizungumza kwenye mahojiano na televisheni ya Fox News ya Marekani, Rais Barack Obama wa nchi hiyo juzi Jumapili alisema kuwa athari za kuishambulia kijeshi Libya, zilikuwa ni kosa lake kubwa, japokuwa wakati huo alikuwa akidhani kwamba uvamizi huo ulikuwa sahihi. Rais Obama aliyatamka hayo wakati alipoulizwa swali kuhusu kosa kubwa zaidi alilowahi kufanya katika kipindi cha utawala wake.

Baada ya mapinduzi ya wananchi wa Libya na kung'olewa madarakani kiongozi wa nchi hiyo Kanali Muammar Gaddafi, baadhi ya nchi ziliyaunga mkono makundi ya kigaidi nchini humo, na kuzuia kuingia madarakani utawala wa kidemokrasia.

JIMMY CARTER: MAREKANI NI NCHI AMBAYO DAIMA IKO VITANI.

JIMMY CARTER: MAREKANI NI NCHI AMBAYO DAIMA IKO VITANI.

Sera za kijeshi na za kupenda vita za Marekani zinakosolewa kote duniani na hivi sasa hata wakuu wa nchi hiyo wameanza kukosoa sera hizo.

Jimmy Carter, rais wa 39 wa Marekani kutoka mwaka 1977 hadi 1981, katika mahojiano na jarida la Time amesema tokea kuanzishwa Umoja wa Mataifa baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia hadi sasa, Marekani daima imekuwa vitani.

Rais huyo wa zamani wa Marekani ambaye aliwahi kushinda Tuzo ya Amani ya Nobel, amesema tangu kumalizika Vita Vikuu Vya Pili vya Dunia Marekani imeanzisha vita katika nchi 30 duniani.

Matamshi ya rais wa zamani wa Marekani ni dalili ya wazi kuwa nchi hiyo haiwezi kutekeleza mipango yake ya kiuchumi na kisiasa pasina kuwepo vita.

Kwa hakika, Marekani katika muundo wake wa sasa iliibuka katika nusu ya pili ya karne ya 18 baada ya kupigana vita vya uhuru na Ufalme wa Uingereza. Tokea wakati huo nchi hiyo kimsingi imekuwa vitani. Marekani ilipigana vita na Uingereza mwaka 1812, kisha ikaingia vitani na Mexico mwaka 1846 na vita na Uhispania mwaka 1898. Kisha iliingia katika Vita Vikuu vya Kwanza vya Dunia mwaka 1917 na baada ya hapo ikaingia katika Vita Vikuu vya Pili vya Dunia vilivyoanza mwaka 1941.

Baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, Marekani iliendeleza sera zake za kichokozi na vita kwa kisingizio cha kutetea kile inachodai kuwa ni uhuru duniani. Hapa tunaweza kutaja baadhi ya vita ambavyo Marekani imejihusisha navyo tokea wakati huo ambavyo ni, Vita vya

MKUTANO JUU YA NJIA IPI LIPITE BOMBA LA MAFUTA UNAFANYIKA UGANDA.

MKUTANO JUU YA NJIA IPI LIPITE BOMBA LA MAFUTA UNAFANYIKA UGANDA.

Mkutano unaohusu ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta kutoka Uganda hadi Bahari ya Hindi ulianza jana katika mji mkuu wa Uganda Kampala.

Taarifa zaidi kutoka Uganda zinasema kuwa, mkutano huo unayashirikisha mataifa waanzilishi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaani Kenya, Uganda na Tanzania- ambapo baada ya siku tatu maafisa wa serikali kutoka mataifa hayo wataamua iwapo bomba hilo linafaa kutoka Uganda na kupitia nchini Tanzania hadi Bandari ya Tanga au kupitia Kenya hadi Bandari ya Lamu au Bandari ya Mombasa.

Bomba la mafuta kutoka Tanga hadi Uganda litakuwa na urefu wa kilometa 1,410 na litasafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima eneo la ziwa Albert nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Bomba la kutoka Hoima na kwenda Lokichar kisha hadi Lamu litakuwa na urefu wa kilomita 1,476.

Bomba la kutoa mafuta Lokichar kisha kupitia Hoima nchini Uganda na kufika Tanga litakuwa na urefu wa kilomita 2,028.

Hivi karibuni Wizara ya Nishati na Madini ya Tanzania iliwahakikishia Watanzania kuwa serikali ya nchi hiyo ina uhakika wa asilimia 98 wa kupata mradi wa ujenzi wa bomba hilo la mafuta kutoka Uganda kuelekea bandari ya Tanga, mradi ambao unapiganiwa pia na nchi jirani ya Kenya.

WAZIRI MKUU WA ITALY YUKO JIJINI TEHRAN.

WAZIRI MKUU WA ITALY YUKO JIJINI TEHRAN.

Waziri Mkuu wa Italia Matteo Renzi amewasili mjini Tehran mapema leo akiongoza ujumbe wa ngazi za juu wa kisiasa na kiuchumi wa nchi yake.
Katika uwanja wa ndege, Waziri Mkuu wa Italia alilakiwa na Waziri wa Viwanda, Madini na Biashara Muhammad Reza Neematzadeh.

Katika safari yake hiyo inayolenga kuinua na kustawisha kiwango cha uhusiano baina ya pande mbili baada ya kipindi cha vikwazo dhidi ya Iran, Matteo Renzi ameandamana na ujumbe wa watu 250 unaojumuisha maafisa wa kisiasa na kiuchumi wa nchi yake.

Imeelezwa kuwa kukutana na kufanya mazungumzo na Rais Hassan Rouhani pamoja na viongozi wengine wa ngazi za juu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kustawisha ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara wa nchi mbili pamoja na kushiriki mashirika na wawekezaji wa Italia katika sekta ya uchumi na biashara ya Iran, ni miongoni mwa malengo ya safari ya Waziri Mkuu wa Italia hapa nchini.

Kabla ya safari yake hiyo, Matteo Renzi alisisitiza kuwa Italia imedhamiria kustawisha uhusiano wa pande mbili katika nyanja zote na kufidia fursa yake iliyopoteza ya biashara na Iran katika kipindi cha vikwazo vilivyowekwa na Magharibi.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo Italia inakusudia kurejesha kiwango cha mabadilishano ya kibiashara na Iran cha mwaka 2010, ambacho ni cha yuro bilioni saba kwa mwaka.