MAONI YA KIGWANGALA JUU YA HOTUBA YA RAIS

MAONI YA KIGWANGALA JUU YA HOTUBA YA RAIS



Huu ni ‪#‎WakatiWaKazi‬ , hotuba ya Rais ya jana imedhihirisha hilo. Kilichonifurahisha jana mimi ni ukweli kwamba kama Taifa tumepata Rais ambaye ataweza kutukimbiza kuelekea kuyafikia matamanio na matarajio yetu. Hotuba ya Rais inadhihirisha kuwa huu kwa hakika ni #WakatiWaKazi.
Sisi sote ni lazima tuamke tujue kuwa ‪#‎TunaKazi‬ ya kufanya mbele yetu, na tuifanye. Tumepata mtu wa kutusukuma kufanya kazi, basi tufanye kazi, tusimuangushe. Na sisi wabunge tumuunge mkono, 'tusimshike' mkono, tumsaidie afanye kazi. Maana kwa hakika ‪#‎MabadilikoYaKweli‬ yamefika. Tuyapokee!

Kuna sheria 21, kwa mujibu wa Katibu Mkuu, Ndg. Kinana, zinazokwamisha wananchi ama zinazowakandamiza, ama zinachelewesha harakati za kuleta maendeleo, zinapaswa kufutwa ama kufanyiwa marekebisho kwa haraka, basi ziletwe Bungeni zirekebishwe kwa haraka, nchi ianze kukimbia sasa.

Tuna changamoto mbalimbali zinazosababishwa na muundo wa serikali, mahusiano na muingiliano wa wizara moja na nyingine, taasisi moja na nyingine, haya nayo yanapaswa kushughulikiwa kabla Rais wetu hajafika mbali. Namna ya kuratibu uwekezaji - kuondoa mindset potofu kwamba wawekezaji ni lazima wawe watu wa kutoka nje tu, kuwa na taasisi ya EPZA, TIC, Wizara ya uwekezaji na uwezeshaji, viwanda na biashara, kilimo na mifugo (ukizingatia uwekezaji mkubwa tunaohitaji kwa sasa ni unaohusiana na sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi ili kuwagusa wananchi walio wengi kwa haraka) yote haya yanachanganya na kuifanya process ya uwekezaji nchini mwetu iwe ndefu na complex kuliko kuwa ya haraka na rahisi n.k.

Tuna mkanganyiko mkubwa sana kwenye mahusiano kiutendaji kati ya wizara ya TAMISEMI na wizara za kisekta...