WAKRISTO WAJIFUNZA UISLAMU KATIKA MAKANISA HUKO MAREKANI.


Licha ya kuongezeka vitendo vya chuki dhidi ya Waislamu nchini Marekani, baadhi ya makanisa ya nchi hiyo yameamua kuitisha vikao mbalimbali vya kujifunza na kuutambua vizuri Uislamu.
Shirika la habari la RASA liliripoti jana Jumatatu kwamba, makanisa ya mji wa Albuquerque katika jimbo la New Mexico huko Marekani, wameandaa ratiba maalumu za kuutambulishwa Uislamu kwa wafuasi wa dini nyinginezo hususan Wakristo.

Ratiba hizo ambazo zimepata umaarufu wa jina la Hotuba za Wanawake Waislamu, wanawake wa tamaduni na dini tofauti wameamua kukusanyika katika makanisa na kujifunza, kuuliza maswali na kujadiliana mambo mbalimbali kuhusu Uislamu ikiwa ni pamoja na kuhusiana na maisha ya Waislamu hususan wanawake Waislamu wa Marekani.

Imepangwa kuwa, ratiba kama hizo zifanyike pia katika makanisa mengine matatu ya jimbo hilo.

Chuki dhidi ya Uislamu zimeongezeka sana huko Marekani, suala ambalo limewafanya wafuasi wa dini nyinginezo hasa Wakristo wadadisi na wapate hamu ya kuujua zaidi Uislamu kutoka kwa Waislamu wenyewe.

WATU 38 WAFA KWA MAFURIKO HUKO AFGHANISTAN.


Watu wasiopungua 38 wamefariki dunia kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kali iliyonyesha maeneo ya kaskazini mwa Afghanistan.

Maafisa wa serikali ya Afghanistan wamesema vifo hivyo vimeripotiwa katika mikoa ya kaskazini ya Takhar, Badghis na Samangan katika mafuriko yaliyoanza Jumapili usiku.

Mkurugenzi wa majanga ya kimaumbile katika mkoa wa Takhar, Abdul Razaq Zinda, amesema watu 13 wakiwemo watoto walifariki katika wilaya za Kalafgan na Bangi.

Aidha amesema, nyumba kadhaa hasa zile zilizojengwa kwa matofali ya udongo ziliharibiwa na mvua kali.

Msemaji wa polisi ya mkoa wa Badghis amesema watu 19 walifariki wilayani Muqur.

Mafuriko yameua pia watu wengine sita ambao ni wanawake watatu na watoto watatu mkoani Samangan na kubomoa nyumba zipatazo 20 na ekari zisizopungua tano za kilimo.

Mvua kali zimeukumba mji mkuu wa Afghanistan, Kabul lakini hakuna maafa makubwa yaliyoripotiwa.

ISRAELI YATETEA KITENDO CHAKE CHA KUKALIA MIUNUKO YA GOLAN YA SYRIA.


Licha ya kuweko upinzani wa jamii ya kimataifa dhidi ya umiliki wa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa eneo la miinuko ya Golan ya Syria unayoikalia kwa mabavu, lakini Waziri Mkuu wa utawala huo, Benjamin Netanyahu amedai kuwa, miinuko hiyo ya Golan daima itakuwa sehemu isiyotenganishika na utawala huo.

Akizungumza siku ya Jumapili katika kikao cha baraza la mawaziri kilichofanyika kwa mara ya kwanza katika eneo la miinuko ya Golan, Benjamin Netanyahu sanjari na kusisitiza juu ya mamlaka ya utawala huo kwa eneo hilo la Syria amesema kuwa, katu Israel haitasalimu amri mbele ya mashinikizo ya kimataifa.

Akiendelea na matamshi yake ya kichochezi kuhusiana na miinuko ya Golan inayokaliwa kwa mabavu na Israel Netanyahu ameitaka jamii ya kimataifa iutambue rasmi umiliki wa Israel kwa miinuko hiyo.

Utawala ghasibu wa Israel uliikalia kwa mabavu sehemu ya miinuko ya Golan ya Syria mwaka 1967 katika vita vyake na Waarabu. Mwaka 1981, utawala huo wa kimabavu uliiunganisha sehemu hiyo na ardhi unazozikalia kwa mabavu, hatua ambayo hakuna wakati ilitambuliwa rasmi na jamii ya kimataifa.

Matamshi hayo ya Netanyahu anayatoa katika hali ambayo, hivi karibuni vyombo vya habari vya Israel vimeripoti mara kadhaa kuhusiana na kihoro na wasiwasi wa viongozi wa utawala huo juu ya kurejea eneo hilo katika milki ya Syria.

Sambamba na duru mpya ya njama za Israel za kutaka kujitanua na kuzikalia kwa mabavu ardhi za Mashariki ya Kati, Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Syria imemwandikia barua Katibu

ROBOTI LENYE HISIA ZA KIBINADAMU LATENGENEZWA CHINA.


Je unaweza tambua roboti kati ya hawa watu kwa hizi picha ? Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia ya China katika mji mkuu wa Hefei, mashariki mwa China  kimezindua roboti kwa jina "Jiajia" ambayo ina uwezo wa mwingiliano na binadamu.

Jiajia ni huyo mwenye mwanamke mwenye nguo nyekundu, anaweza kila kitu ambacho mwanamke anaweza kasoro kubeba mimba tu, lakini hisia za kupenda na kuchukia, hisia za kulala na mwanaume na mengi kama hayo.

Roboti hizo zinauwezo wa kutongoza au kutongozeka, zinaweza kukataa au kukubali inategemea na uwezo wako wa kushawishi.

Bado bei yake haijapangwa, na yapo yanayotengenezwa maalum kwaajili ya Afrika, je yakija Tanzania utanunua?? yakiume pia yatatengenezwa kwaajili ya kazi mbalimbali kama kulima nk.

Watu watabisha lakini mbona wanakula mayai kizungu, kuku za kizungu, sasa kuna ubaya gani mkila na nyapu/zakari za kichina? Au wachina hamuwaamini?

TANZANIA NI YA PILI KWA UZALISHAJI BANGI KWA WINGI AFRIKA.


Polisi nchini Tanzania wameendeleza oparesheni dhidi ya ukuzaji wa bangi pamoja na biashara yake kwenye eneo la Arusha.

Oparesheni hiyo inaendelezwa huku ripoti ya Umoja wa Mataifa ikionyesha kuwa Tanzania ndio mzalishaji mkuu wa pili wa bangi barani Afrika.

Kamanda wa polisi kwenye eneo la Arusha Charlse Mkumbo amesema oparesheni hiyo italenga biashara na ukuzaji wa bangi na miraa.

TETEMEKO LINGINE LIMETOKEA JAPANI.

TETEMEKO LINGINE LIMETOKEA JAPANI.

Tetemeko lignine la ardhi lenye nguvu ya 7.3 kwenye vipimo vya Richter limetokea nchini Japan na kuuwa watu 19 na kusababisha uharibifu mkubwa hayo ni kwa mujibu wa mamlaka nchini humo.  

Tetemeko hilo  lilikukumba kisiwa cha Kyushu ndani ya siku mbili, na kusa sababisha kuporomoka kwa majengo, barabara, mifumo ya maji na umeme.
Wanajeshi 20,000 wametumwa kusaidia juhudi za uokoaji lakini jitihada za uokoaji zimetatizwa na mitetemeko mingine midogo midogo.

Hivi majuzi lilitokea tetemeko Kumamoto hukohuko Japan na kuleta uharibufu na kuua watu, hili sasa lingine, nchi ya Japan inakumbwa na majanga haya kwa mara na kupelekea nchi hiyo kuwa na sheria kali za ujenzi.

GAVANA HUKO MAREKANI ALIGIZA HELKOPTA KUBEBA WALLETI YAKE.


Helikopta ya polisi ilitumwa kuchukua pochi ya gavana wa jimbo moja nchini Marekani, safari iliyogharimu $4,000 (£2,800), uchunguzi umebaini.

Kisa hicho kilitokea mwishoni mwa 2014.
Gavana wa Alabama Robert Bentley aliondoka Tuscaloosa kuelekea kwenye nyumba yake ya ufukweni, mwendo wa saa tano hivi ukitumia gari, lakini akasahau pochi yake.

Aliwataka maafisa wake wa usalama kwenda kuchukua pochi hiyo. Maafisa hao walitumia helikopta hiyo ya polisi, rekodi za safari za ndege zimeonesha.
Bw Bentley anakabiliwa na shinikizo za kumtaka ajiuzulu kutokana na sakata ya unyanyasaji wa kingono.

Lakini anasema hakuagiza ndege itumiwe kwenda kuchukua pochi.
"Niliwaomba tu waende wakachukue pochi yangu, sikuwaambia watumie njia gani,” gavana huyo ameambia mtandao wa AL.com.

„Sikuwaambia watumie helikopta. Ni lazima uwe na pochi yako kwa sababu za kiusalama. Mimi ni gavana. Na ni lazima niwe na pesa. Ni lazima ningenunua kitu cha kula. Na nilihitaji vitambulisho vyangu.”

Tovuti ya AL.com inasema safari hiyo ya helikopta iligharimu mlipa kodi takriban $4,000 (£2,800).

IRAN YAJITAMBA KUWA NA JESHI IMARA NA LENYE NGUVU.

IRAN YAJITAMBA KUWA NA JESHI IMARA NA LENYE NGUVU.

Luteni Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu la Iran amesema kuwa, jeshi hilo liko imara katika kuyalinda Mapinduzi ya Kiislamu na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
Shirika la habari la IRNA limemnukuu Brigedia Jenerali Kiumars Heidari akisema hayo wakati huu wa kukaribia Siku ya Jeshi nchini Iran.

Ameongeza kuwa, jeshi la Iran halizembea hata sekunde moja kuulinda Uislamu na Mapinduzi ya Kiislamu na kwamba kusimama kwake huko imara kunathibitishwa na jinsi jeshi hilo lilivyo na fakhari ya kutoa mashahidi 48 elfu katika njia ya haki.

Brigedia Jenerali Kiumars Heidari ameongeza kuwa, jeshi la Iran lina tofauti kubwa na majeshi ya nchi nyingine duniani na kusisitiza kuwa, leo hii jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limekuwa mtetezi mkubwa wa wanyonge na watu wanaodhulumiwa duniani na limesimama imara kukabiliana na waistikbari na mabeberu na ndio maana linapendwa na linakubalika.

Ikumbukwe kuwa kesho Jumapili inayosadifiana na tarehe 17 Aprili ni siku ya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka kwa ratiba tofauti.

MALALAMIKO YA WAZIMBABWE KWA SIASA ZA MUGABE.


Wananchi wa Zimbabwe wamefanya maandamano kulalamikia siasa za Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo.
Karibu wafuasi elfu mbili wa chama cha upinzani cha MDC cha Morgan Tsvangirai wamefanya maandamano mjini Harare kulalamikia siasa za Rais Robert Mugabe. Akizungumza mbele ya wafuasi wake Tsvangirai amesisitiza kuwa, Mugabe ameshindwa kutatua mgogoro wa nchi hiyo na kwamba wananchi wa Zimbabwe wanaamini kuwa, serikali yake haina njia nyingine ila kuporomoka tu.

Robert Mugabe ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 92, amekuwa rais wa Zimbabwe tangu mwaka 1980. Hali yake tete ya kiafya imepelekea kuzuka maneno mengi kuhusu mtu wa kurithi kiti chake. Kumekuwa na dhana kuwa, Mugabe anafanya mpango wa kumrithisha kiti hicho mkewe, Grace Mugabe. Hata hivyo mwanzoni mwa mwezi uliopita wa Machi, Mugabe alikanusha uvumi huo na kusisitiza kuwa, rais ajaye wa Zimbabwe lazima achaguliwe kwa njia za kidemokrasia.

Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, matamshi hayo ya Mugabe yanaashiria azma yake ya kuendelea kuwa rais wa Zimbabwe hadi mwisho wa maisha yake. Katika hali ambayo duru za kisiasa za nchi hiyo zinafuatilia kwa karibu sana hali ya kiafya ya Mugabe, baadhi ya duru hizo zinaamini kuwa, hatua ya Mugabe ya kushindwa kuainisha mrithi wake itazidi kuitumbukiza katika mgogoro nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.

Hivi sasa hali ya kiuchumi ya Zimbabwe ni ya mgogoro kiasi kwamba baadhi ya ripoti zinaonesha kuwa Zimbabwe ndiyo nchi maskini zai