USAWA WA BAHARI HUKO NEW ZEALAND UTAINUKA KWA MM 30 KATIKA KARNE HII.

Usawa wa bahari kando ya New Zealand utainuka kwa milimita 30 hata mita moja ndani ya karne hii

Ripoti iliyotolewa na taasisi ya New Zealand inaonesha kuwa, kama utoaji wa hewa inayosababisha kuongezeka kwa joto duniani hakutapungua kwa kiasi kikubwa, joto litaendelea kuongezeka, na usawa wa bahari kando ya New Zealand utainuka kwa milimita 30 hata mita moja ndani ya karne hii.

Kuinuka kwa usawa wa bahari kutasababisha maji ya bahari kuingia kwenye fukwe nchini humo, na hivyo mafuriko yatatokea mara kwa mara wakati wa mvua kubwa. Hivi sasa watu wengi wanaishi pwani, na theluthi mbili ya watu wanaishi katika maeneo yaliyo kwenye hatari zaidi ya kukumbwa na mafuriko.

Mfano pwani ya Otago iliyoko kisiwa cha kusini cha nchi hiyo, tofauti kati ya urefu wa mawimbi yanayosababishwa na tufani yanayotokea kila baada ya miaka miwili na mawimbi makubwa yanayotokea kila miaka mia moja ni milimita 32 tu, hii inamaanisha kuwa kama usawa wa bahari ukiinuka kwa milimita 30, maafa ya mafuriko yaliyotokea kila miaka mia moja huenda yatatokea kila mwaka.

Licha ya hayo, wakati joto linapoendelea kuongezeka, mvua itapungua, kazi za ujenzi, uzalishaji viwandani na utoaji wa maji baridi zitakabiliwa na shinikizo kubwa. Wanyama na mimea ambayo sasa iko hatarini huenda vitatoweka.

Ingawa kuongezeka kwa joto duniani kutasababisha kupanda kwa bei ya bidhaa duniani, na kunufaisha maendeleo ya kilimo nchini humo, lakini pia kutaleta athari nyingi mbaya, na kuhatarisha usalama wa chakula.

TFDA YANASA VIPODOZI HARAMU TANI 15.

Mamlaka ya Chakula na Dawa nchini TFDA imenasa vipodozi vya magendo tani 15 vyenye thamani ya shilingi milioni 400 mjini Dar es Salaam.
Bidhaa hizo  zilikuwa zimehifadhiwa kwenye ghorofa mbili zilizoko eneo la Karioakoo mjini humo.

Meneja wa TFDA Emmanuel Alphone amesema vipodozi hivyo vimeingizwa bila ya idhidi ya mamlaka husika.
Watu wanane wamekamatwa na kuhojiwa kuhusiana na bidhaa hizo na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani.

SOMALIA NA AU WAJIPANGA KUPAMBANA NA UGAIDI.

Somalia na Umoja wa Afrika wanapanga kuwa na mikakati mipya ya usalama ili kuzuia matishio ya ugaidi nchini Somalia.

Mwakilishi maalum wa mwenyekiti wa Kamati ya Umoja wa Afrika nchini Somalia Bw Francisco Madeira amefanya mazungumzo na naibu waziri mkuu wa Somalia Bw Mohamed Omar Arte kuhusu mambo muhimu ya operesheni za usalama.

Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Africa imesema, kwenye mkutano huo, maofisa hao wawili walijadili kuhusu jinsi majeshi ya serikali ya Somalia na tume ya Umoja wa Afrika nchini humo AMISOM yanavyoweza kuratibu na kushirikiana kulishinda kundi la Al Shabaab.

RIYAD MAHREZ AWA MWAFRIKA WA KWANZA KUSHINDA TUZO YA PFA.

Mshambuliaji wa kimataifa wa Algeria anayeichezea klabu ya Leicester City ya Uingereza Riyad Mahrez ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya PFA 2015/2016 (Professional Footballers Association).

Riyad Mahrez ametangazwa kushinda tuzo hiyo mbele ya wachezaji kama Mesut Ozil wa Arsenal, Jamie Vardy wa Leicester City, Harry Kane wa Totenham Hot Spurs, N’golo Kante wa Leicester City na Dimitri Payet wa West Ham United.
PFA ni tuzo za wachezaji bora wa kulipwa.

CRYSGAL PALACE IYAKUTANA NA MANCHESTER KOMBE LA FA.

Crystal Palace itakutana na Manchester United katika fainali ya kombe la FA mwaka 2016, kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Watford City.

Yannick Bolasie aliongoza Palace kabla ya Troy Deeney kusawazisha kunako dakika ya 55, lakini Conor Wickham alifunga bao la pili na la ushindi kwenye dakika ya 61.

WABUNGE TISA WAPEWA SIKU 30 KUICHUNGUZA LUGUMI.


















WABUNGE TISA WAPEWA SIKU 30 KUICHUNGUZA LUGUMI.

Akizungumza na waandishi wa habari hapo jana mjini Dodoma baada ya kikao cha kamati hiyo, Kaimu Mwenyekiti wa PAC Mh.Aeshy Hilary amesema uamuzi wa kuundwa kamati hiyo umekuja kufuatia kutoridhishwa na ripoti hiyo pamoja na kuwepo kwa changamoto katika taarifa ya utekelezaji wa mradi huo iliyowasilishwa na Jeshi la Polisi.

Mh. Hilary alisema kuwa majukumu ya kamati hiyo yatakayoongozwa na Mwenyekiti wake Mh. Josephat Asunga ni k...uwa kamati hiyo ndogo itafanya uchunguzi kwa muda wa siku 30 sambamba na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Ameongeza kuwa uchunguzi huo utafanywa kwa mtindo wa kikachero na ule wa kushtukiza, ili kukwepa hali ya kuandaliwa kwa mazingira ya kuficha ukweli.

GAIDI MWANDAMIZI WA AHRAR AL SHAM AUAWA HUKO SYRIA.











GAIDI MWANDAMIZI WA AHRAR AL SHAM AUAWA HUKO SYRIA.

Kamanda mwandamizi wa kundi la kigaidi la Ahrar al-Sham lenye mafungamano na mtandao wa kimataifa wa al-Qaeda ameuawa katika hujuma ya bomu iliyolenga ngome za kundi hilo katika mkoa wa Idlib, kaskazini magharibi mwa Syria.
Majid Hussein al-Sadeq pamoja na magaidi wengine watatu waliuawa katika shambulio la jana Jumamosi dhidi ya mji wa Binnish, unaohesabiwa kuwa moja ya ngome za magaidi hao, yapata kilomita 10 kaskazini mashariki mwa mkoa wa Idlib.
Julai mwaka jana, kamanda mwingine mkuu wa kundi la kigaidi la Ahrar al-Sham kwa jina Abu Abdu Rahman Salqin aliuawa katika shambulio jingine la bomu katika eneo la Abu Talha, mkoani Idlib.
Kwa muda mrefu sasa serikali ya Syria imekuwa ikisisitiza kuwa magaidi nchini humo wanapata misaada ya fedha na silaha kutoka nchi za Magharibi hasa Marekani na waitifaki wake katika eneo hili ambao ni Saudi Arabia, Qatar, Uturuki na utawala haramu wa Israel. Karibu watu nusu milioni wameshapoteza maisha tokea magaidi waanzishe kampeni ya kumuondoa madarakani Rais Bashar al Assad wa Syria mwaka 2011.
Hii ni katika hali ambayo, Steffan de Mistura, Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Syria amesema watu wapatao laki nne wamepoteza maisha kutokana na vita vya zaidi ya miaka mitano vilivyoikumba nchi hiyo ya Kiarabu.

ALIYEMTUSI MTUME MUHAMMAD(S.A.W) AUHUKUMIWA KIFO MAURITANIA.


Mahakama ya Rufaa ya Mauritania imepasisha hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi aliyemvunjia heshima Mtume Muhammad (saw).

Shirika la Habari la Kimataifa la Qur'ani (IQNA) limeripoti kuwa, Mahakama ya Rufaa ya mji wa Nawadibo huko kaskazini magharibi mwa Mauritania imepasisha hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi Muhammad Sheikh Ould Amkhtir wa nchi hiyo kwa sababu ya kuandika makala iliyomvunjia heshima na kumtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad (saw) hapo mwaka 2014.

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mauritania ambaye aliomba kutolewe hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi huyo amesema kuwa kunyongwa kwake kutakuwa somo kwa wale wote wanaothubutu kumvunjia heshima Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Kuchapishwa kwa makala ya mandishi Muhammad Sheikh Ould Amkhtir hapo mwaka 2014 kulisababisha maandamano makubwa kote Mauritania ambayo hayakutulia ila baada ya kutolewa hukumu ya kifo dhidi ya mwandishi huyo.

UMOJA WA ULAYA HAUTAMBUI UMILIKI WA ISRAELI KWA MIINUKO YA GOLAN.


Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa, umoja huo hauutambui rasmi umiliki na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa miinuko ya Golan ya Syria.

Federica Mogherini amesisitiza kuwa, Umoja wea Ulaya hautambui ukaliaji mabavu wa Israel dhidi ya ardhi za Palestina baada ya vita vya mwaka 1967 na kuongeza kuwa, huu ni msimamo wa Umoja wa Ulaya na nchi wanachama wa umoja huo.

Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema hayo siku chache baada ya utawala wa Kizayuni wa Israel kudai kwamba, miinuko ya Golan ya Syria ni sehemu ya ardhi ya utawala huo.

Waziri Mkuu wa utawala huo, Benjamin Netanyahu alinukuliwa hivi karibuni akidai kwamba, miinuko hiyo ya Golan daima itakuwa sehemu isiyotenganishika na utawala huo.

Utawala ghasibu wa Israel uliikalia kwa mabavu sehemu ya miinuko ya Golan ya Syria mwaka 1967 katika vita vyake na Waarabu. Mwaka 1981, utawala huo wa kimabavu uliiunganisha sehemu hiyo na ardhi unazozikalia kwa mabavu, hatua ambayo hakuna wakati ilitambuliwa rasmi na jamii ya kimataifa.