XI JINPING:MAKUBALIANO YA KIMATAIFA YAHITAJI HAKI NA USAWA.

Rais Xi Jinping wa China amesema usawa na haki ni msingi wa makubaliano yoyote ya kimataifa.
Rais Xi amesema hayo alipohudhuria mkutano wa wakuu wa nchi 6 kuhusu suala la nyuklia la Iran mjini Washington.
Rais Xi amesema, utatuzi wa suala la nyuklia la Iran umetoa funzo kubwa, kuwa makubaliano yoyote ya kimataifa yanatakiwa kufikiwa kwenye msingi wa haki na usawa, ambapo ufuatiliaji wa haki ya kila nchi unatakiwa kuzingatiwa.

Amesisitiza kuwa, mazungumzo ni njia yenye ufanisi zaidi ya kutatua masuala makubwa, ambapo nia ya kisiasa inahitajika huku ikisaidiwa na uratibu na ushirikiano kati ya nchi kubwa duniani.

JINSI WANAFUNZI WA YESU WALIVYOKUFA.!

JINSI WANAFUNZI WA YESU WALIVYOKUFA.!

1. #Mathayo.
Huyu aliuawa kwa upanga huko Uhabeshi (Ethiopia ya leo) baada ya kuonyesha imani kali dhidi ya kanisa la Kristo. Alijeruhiwa kwa upanga na kidonda chake hakikupona hadi umauti ulipomfika.

2. #Marko
Huyu alifariki huko Alexandria Misri ya sasa baada ya kuangushwa na farasi barabarani, aliangushwa vibaya na hakupata msada. Mwishowe akafariki.

3. #Luka
Alinyongwa huko Ugiriki, hii ni kutokana na msimamo wake mkali aliouonesha dhidi ya Kristo.

4. #Yohana
Huyu alitumbukizwa katika pipa lenye mafuta yanayochemka huko Roma, (Italia ya sasa). Hata hivyo kwa miujiza hakuungua na  alitolewa akiwa mzima kabisa.

Alipelekwa katika gereza lililokuwa katika migodi huko kisiwa cha Patmos. Na huko ndiko alipofunuliwa na mwenyezi Mungu na kuandika kitabu cha "Ufunuo wa Yohana". Baadae aliachiwa huru na kwenda kutumika kama Askofu huko Edessa (Uturuki ya sasa). Alifariki akiwa mzee sana. Na ni mtume pekee aliuefariki bila mateso.

5. #Petro
Huyu alipata adhabu ya kifo cha msalaba. Ila yeye alisulubiwa tofauti na Yesu kristo. Kusulubiwa kwa Petro ilikuwa kichwa chini miguu juu katika msalaba wenye nembo ya "X". Petro mwenyewe aliomba asulubiwa kwa namna hii kwani hakutaka kusulubiwa kama Yesu (Yohana 21:18).

6.#Yakobo
Alikuwa Kiongozi wa kanisa huko Jerusalemu Israel ya sasa. Yeye alitupwa kutoka juu kabisa ya mnara wa hekalu wenye urefu wa meta 100 baada ya kugoma kumpinga Kristo. Mnara huo ni ule ambao Shetani aliutumia kumjaribu Yesu kwa kumwambia kama yeye ni mwana wa Mungu ajirushe.  Walipogundua kuwa hajafa baada ya kumdondosha tokea juu ya mnara, walimpiga na mawe mpaka akafa.

7. #Yakobo (mwana wa Zebedayo)
Alikuwa ni mvuvi kabla Yesu hajamteua kuwa mwanafunzi wake. Akiwa kiongozi mkubwa wa kanisa Yakobo alichinjwa huko Jerusalemu kwa kukatwa kichwa kwa amri ya Herode (Matendo 12:2).

8. #Batholomayo
Pia alijulikana kama Nathanieli. Alikuwa ni mmisionari huko Armeni (Asia ya sasa). Alimshuhudia Yesu Kristo huko Uturuki. Yeye aliuawa kwa kupigwa fimbo baada ya kugoma kuacha mafundisho yake dhidi ya Kristo.

9. #Andrea
Aliuawa kama Petro huko Ugiriki kwa kusulubiwa kwenye msalaba wenye umbo la "X" miguu juu kichwa chini sawa na Petro Petro. Ila baada ya kuwambwa msalabani aliendelea kupaza sauti akihubiri neno la Mungu mpaka mauti ilipomchukua. Akiwa msalabani aliwaambia wafuasi wake "nilikua naisubiri saa kama hii"

10. #Tomaso
Aliuwa kwa kupigwa na mshale huko Chennai (India ya sasa) katika moja ya safari zake kama Mmisionari kwenda kuanzisha Kanisa huko.

11. #Yuda (Thadei)
Aliuawa kwa kupigwa na mshale ubavuni.

12. #Yuda (Iskariote)
Huyu alijiua kwa kujinyonga baada ya kumuuza Yesu kwa vipande 30 vya fedha.

NOTE:
13. #Thadayo (au Mathia) ni Mwanafunzi aliyeteuliwa na Yesu kuziba nafasi ya Yuda Iskariote (msaliti). Huyu alipigwa na mawe  hadi kufa na baada ya hapo walimkata kichwa.

14. #Paulo
Hakuwa mmoja wa wale wanafunzi 12 wa Yesu. Lakini huhesabika kuwa mfuasi wa Kristo na mtetezi wa mwanzo wa Kanisa. Huyu aliteswa na baadaye akachinjwa na Emperor Nero huko Roma mwaka (A.D).

Kabla ya kuchinjwa Paulo aliishi muda mrefu sana gerezani ambapo akiwa huko aliandika barua (nyaraka) nyingi kwa makanisa mbalimbali. Ndio hizi ambazo zinafundisha misingi ya ukristo katika agano jipya, kama vile Waraka wa Paulo mtume kwa Warumi, Wakoritho, Waefeso, Wakolosai, Wathesalonike, Timotheo etc.

NB: Si muhimu kujua ni namna gani mitume walikufa, ila ni muhimu kujua kuwa mitume wote walikufa wakitetea imani yao. Walikua tayari kuchukiwa na kufa vifo vya mateso kwa ajili ya kumtetea na kumshuhudia Kristo.

Biblia imesema, "Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu, lakini mwenye kuvumilia mpaka mwisho, ndiye atakayeokoka." Mathayo Mtakatifu 10:23

Nakutakia pasaka njema.!

Malisa Godlisten GJ.!

WAJUE MAADUI WA NYOKA.

WAJUE MAADUI WA NYOKA.

Nyoka wenye sumu ni hatari sana, lakini wao pia wana maadui. Maadui zao ni pamoja na karani tamba, tai wanaokula nyoka (crested serpent eagle), vicheche na mamba. Baadhi ya nyoka wanakula nyoka, kwa mfano King Cobra anaweza kumla cobra. Hivyo nyoka wenye sumu wanahitaji kuchukua hatua mbalimbali Ili kujilinda katika mazingira yenye maadui wengi.

Hatua ya kwanza ni kujifanya aonekane kuwa mkubwa na hatari. Nyoka aina ya Death Adder wanaoishi huko Australia ni moja kati ya nyoka wenye sumu kali zaidi duniani, Lakini hawawezi kushinda tai wanaokula nyoka. Death Adder akikutana na tai, anatulia, kupanusha mwili wake ili ionekane kama tai hataweza kumeza. Kama tai hana maarifa ya kutosha, atamwacha na kuondoka.

Hatua ya Pili ni kujificha. Nyoka aina ya Western diamondback rattlesnake anaweza kujificha vizuri. Kutokana na madoa ya rangi ya kijivu kwenye ngozi yake, anaonekana kama changarawe. Kwa nyoka huyu anayetembea polepole, anaweza kupumzika bila ya kugunduliwa na maadui.

Hatua ya tatu ni kutoa onyo.
Nyoka aina ya rattlesnake anaweza kupiga kelele kwa kutikisika mkia wake ili kuwaonya wanyama wengine wasiingie eneo lake. Na nyoka aina ya Gaboon viper anatoa mlio wa ‘sss’ ili kutoa onyo.

SHIRIKA LA KIJASUSI LA ISRAELI HUMTUMIA MWANAMKE KAMA SILAHA.

SHIRIKA LA KIJASUSI LA ISRAELI HUMTUMIA MWANAMKE KAMA SILAHA.

Mtandao wa Intaneti wa "Sauti ya Israel" umefichua kuwa, silaha ya hatari zaidi inayotumiwa na shirika la kijasusi la utawala wa Kizayuni MOSSAD ni mwili wa mwanamke wa Kiyahudi.

Televisheni ya al Alam imeunukuu mtandao wa habari wa Alsumaria News ukiripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, mwili wa mwanamke wa Kiisraeli unahesabiwa kuwa moja ya silaha muhimu sana za kufanikishia malengo ya MOSSAD kiasi kwamba watu wenye ushawishi ndani ya utawala wa Kizayuni wanawashawishi wanawake wa Kiyahudi kutofungwa na maadili yoyote yale na wapewe uhuru kamili wa kutumia wanavyotaka miili yao kwa ajili ya utawala wa Kizayuni.

Mtandao huo umemnukuu kuhani mmoja wa Kiyahudi akisema: Ingawa jamii yetu imeshikamana na dini, lakini tuna wajibu wa kuwashawishi wanawake wa Kiyahudi kujichanganya na watu wa jamii nyingine ili kuenea ukafiri na ufisadi na kudhoofisha misingi muhimu ya jamii hizo, ili iwe rahisi kuzidhibiti.

Mtandao huo umeongeza kuwa, mwanamke wa Kiisraeli anahesabiwa kuwa nguzo moja muhimu sana ya Shirika la Kijasusi la Israel, MOSSAD na wanahesabiwa kuwa ni silaha ya nne muhimu zaidi ya utawala wa Kizayuni baada ya jeshi la majini, jeshi la anga na jeshi la nchi kavu la Israel.

Mtandao huo wa Intaneti umeongeza kuwa, kila mwaka maelfu ya wanawake wa Kiyahudi wanajiunga na MOSSAD na moja ya kazi zao kubwa ni kuuza miili yao, kuua na maovu mengineyo kwa ajili ya kuulinda utawala wa Kizayuni wa Israel.

WATU ZAIDI 69 WAMEKUFA KATIKA MLIPUKO PAKISTAN.

WATU ZAIDI 69 WAMEKUFA KATIKA MLIPUKO PAKISTAN.

Zaidi ya watu sitini na tisa wamekufa na wengine kujeruhiwa katika mlipuko uliotokea kwenye eneo la wazi la kupumzikia lenye shughuli nyingi katika mji wa Lahore nchini Pakistan.

Polisi wanasema mlipuaji mwenye kujitoa mhanga alijilipua karibu na eneo la kuchezea watoto mahali wazazi walipokuwa wamejikusanya ambao baadhi yao walikuwa wakisherehekea siku kuu ya Pasaka.

Wengi ya waliokufa na kujeruhiwa katika tukio hilo ni watoto. Tayari kundi la Talbani la Pakistan la Jamaat ul Ahrar limekiri kuwa ndilo linalohusika na shambulizi hilo. Msemaji wa kundi hilo amesema walikusudia kuwalenga jamii ya wakristo waliopo katika mji huo.

Afzal ni mmoja ya wakazi wa mji wa Lahore yeye alikuwa ni miongoni mwa waliosaidia kuwasaidia majeruhi baada ya mlipuko kutokea.

" Nimewabeba zaidi ya watoto ishirini ambao walipelekwa hosptalini. Nilisaidia kubebe miili mitatu na kupakia kwenye gari la polisi. Wakati mlipuko ulipokuwa unatokea watoto walikuwa wakicheza kwenye uwanja huo wa wazi. Leo jamii ya wakristo walimaliza mfungo na kusherehekea Pasaka. Wakristo wengi walifika hapa katika tukio hili. Siwezi kuelezea jinsi tukio hilo la kusikitisha lilivyokuwa."

Naye Tariq Fatimi ambaye ni mshauri wa Waziri Mkuu wa Pakistani ameiambia BBC kuwa tukio hilo ni la kinyama bila kujali ni nchi gani imelengwa.

" Hata kama shambulizi hilo limetokea Peshawar au Lahore au Brussels au Paris au London, Sisi sote tunapaswa kuwa pamoja kwa sababu huu ni uhalifu ambao hauathiri nchi moja pekee, au jamii moja lakini inaathiri wanadamu wote."

PADRI ATIMULIWA KWA KULAWITI VIJANA ITALIA.

Padri wa Kikatoliki atimuliwa kwa kuwalawiti vijana Italia 

Padri mmoja wa Kanisa Katoliki mjini Milan nchini Italia amesimamishwa kazi baada ya kubainika kuwa amekuwa akimhonga kijana mmoja barobaro ili afanye naye ulawiti.

Askofu Mkuu wa Kanisa hilo katika eneo la Muggiano mjini Milan, Kadinali Angelo Scola amesema kuwa amemsimamisha kazi Padri Alberto Paolo Lesmo wa kanisa hilo, kwa tuhuma za kumhadaa kijana aliyekuwa mraibu wa mihadarati kati ya mwaka 2009 na 2011 na kisha kufanya naye tendo la liwati.

Kadinali huyo amesema: “Ni majuzi tu tumegundua kuwa Padri Lesmo alikuwa anafanyiwa uchunguzi na vyombo vya dola kuhusu uozo huo tangu mwaka 2013; hata hivyo tumeanzisha uchunguzi wetu juu ya tuhuma hizo, lakini kwa sasa tumemvua Upadri na kumsimamisha kazi.”

Madai ya liwati na visa vya kushiriki ngono na watoto wadogo sio mapya kwa Kanisa Katoliki, na katika miaka ya hivi karibuni, waathiriwa wa vitendo hivyo vichafu wamekuwa wakijitokeza hadharani na kufichua kashfa hizo.

Licha ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis kutoa dikrii ya kutaka kuchukuliwa hatua za kinidhamu maaskofu wanaoficha kashfa za kulawitiwa watoto wadogo na mapadri wa kanisa hilo, lakini visa hivyo vimekuwa vikiripotiwa kila uchao.

Miongoni mwa nchi ambazo zimerekodi idadi kubwa ya wakuu wa Kanisa Katoliki kugunduliwa kuwa wanawalawiti wavulana wadogo ni Marekani, Ireland, Uholanzi, Australia, Ufaransa, Ujerumani, Austria, Ubelgiji, Canada, Mexico na Poland.

ISRAELI KUSHIRIKIANA FBI KUDUKUA SIMU.

ISRAELI KUSHIRIKIANA FBI KUDUKUA SIMU.

Baada ya Shirika la Simu za Apple kukataa kushirikiana na Idara ya Polisi ya Upelelezi Marekani FBI katika kuifungua simu aina ya iPhone iliyotumiwa na mtu anayedaiwa kutekeleza mauaji San Bernardino, California mwaka jana, shirika moja la Kizayuni limepewa jukumu la kuifungua simu hiyo.

FBI imesema kuwa imepata njia ya kuifungua simu hiyo ambayo imefungwa na nywila ya siri. Shirika la mitandao ya intaneti la Cellebrite ambalo huunda programu za kiusalama za simu za mkononi, limesema linashirikiana na FBI kuidukua simu hiyo.

Shirika la Cellebrite ambalo ni tawi la shirika la Sun Corp la Japan limesema linaweza kuunda programu mpya itakayowezesha kufunguliwa simu hiyo ya iPhone na hivyo kuhitimisha mvutano baina ya FBI na Apple.

FBI imekuwa ikilishinikiza shirika la Apple kufungua simu ya iPhone iliyokuwa ikitumiwa na mmoja kati ya waliotekeleza mauaji ya San Bernardino lakini Apple imekataa kufanya hivyo kwani huo utakuwa mwanzo wa kudukuliwa taarifa katika simu za watumiaji wa simu za iPhone.

Shirika la Apple limeishtaki FBI katika mahakama nchini Marekani lakini kesi hiyo ambayo ilikuwa imepangwa kusikilizwa Jumamosi iliyopita imeakhirishwa kufuatia ombi la serikali ya Marekani. Watetezi wa haki za binadamu wamelalamikia hatua ya kuakhirishwa kesi hiyo. Wiki mbili zilizopita pia, Rais Obama wa Marekani alisema anapinga kuundwa simu za mkononi ambazo maafisa wa serikali hawataweza kupata maelezo yaliyo ndani kila wanapotaka. Kwa m

VIONGOZI WA UPINZANI CONGO BRAZZAVILLE WAITISHIA KUANDAMANA NCHI NZIMA.

VIONGOZI WA UPINZANI CONGO BRAZZAVILLE WAITISHIA KUANDAMANA NCHI NZIMA.

Viongozi wa upinzani nchini Kongo Brazzaville wameitisha maandamano ya nchi nzima kupinga kuchaguliwa tena Rais Denis Sassou Nguesso mwenye umri wa miaka 72.

Viongozi watano wa upinzani nchini humo walioshindwa katika uchaguzi rais wa Jumapili iliyopita akiwemo Guy-Brice Parfit Kolelas aliyeibuka wa pili kwa kupata asilimia 15 ya kura na Jean-Marie Mokoko ambaye alishika nafasi ya tatu kwa asilimia 14 wamewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maandamano ya nchi nzima mnamo Machi 29, kulaani kile walichokitaja kuwa ‘wizi wa kura na utumizi mbaya wa mamlaka.’

Wamewaasa wananchi kujitokeza kwa wingi katika kila mji kupigania kile walichokiita kuhujumiwa haki zao za kidemokrasia na kushinikiza kuheshimiwa katiba.

Tume ya Uchaguzi nchini Kongo Brazzaville ilimtangaza Denis Sasso Nguesso kuwa mshindi wa kiti cha urais katika uchaguzi wa Machi 20 kwa kupata asilimia 60 ya kura zote halali zilizopigwa.

Nguesso ambaye ameiongoza nchi hiyo kwa zaidi ya miaka 30, Oktoba mwaka jana alibadilisha katiba na kuondoa kipengee kinachoweka ukomo wa vipindi viwili kwa Rais na kujiandalia mazingira ya kubakia madarakani.

RAIS ASSAD ALIPONGEZA JESHI LA SYRIA KWA KUUKOMBOA MJI WA PALMYRA.

RAIS ASSAD ALIPONGEZA JESHI LA SYRIA KWA KUUKOMBOA MJI WA PALMYRA.

Rais Bashar al-Assad wa Syria amelipongeza jeshi la nchi hiyo kwa kuukomboa mji wa kihistoria wa Palmyra kutoka mikononi mwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh.

Rais Assad ameyasema hayo leo wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na wabunge wa Ufaransa mjini Damascus na kuongeza kuwa, kukombolewa mji huo ni mafanikio makubwa sana kwa taifa la Syria na kunaonyesha namna jeshi la nchi hiyo likishirikiana na makundi ya wananchi linavyoendelea kupata mafanikio na kuzidi kukomboa miji mbali mbali ambayo ilikuwa chini ya udhibiti wa matakfiri wa Daesh.

Wakati huo huo, jeshi la Syria limesema kuwa, baada ya kuukomboa na kuudhibiti mji wa Palmyra, sasa linajiandaa kusonga mbele kwa ajili ya kuikomboa mikoa ya Raqqah na Deir al-Zawr. Kamandi Kuu ya jeshi la Syria imepongeza kukombolewa mji huo wa kihistoria na kusema kuwa, huu ndio mwanzo wa kuporomoka kwa harakati za kundi la kigaidi na kitaifiri la Daesh nchini humo.

Itakumbukwa kuwa, Juni mwaka jana 2015, wanachama wa kundi la kitakfiri la Daesh walibomoa makaburi mawili ya kale ya Mawalii wa Allah katika mji wa kihistoria wa Palmyra mkoani Homs nchini Syria. Mkurugenzi wa Turathi za Kale nchini Syria, Maamoun Abdulkarim, alisema kuwa magaidi hao wa kitakfiri walilipua mabomu ndani ya majengo ya makaburi ya Mohammad bin Ali wa kizazi cha binamu yake Mtume Muhammad SAW na Nizar Abu Bahaaeddine, msomi mtajika wa Kiislamu kutoka Palmyra.