MAPENZI, NDOA, ROHO, MAJINI NA BINADAMU.

Ndoa nyingi huvunjika, na wapenzi wengi huachana kabla hata hawajafunga ndoa. Kabla ya ndoa kuvunjika na wapenzi kuachana hutokea visa vingi vya usaliti, ukigeugeu na chuki.

Mapenzi nini? Mahala pake hasa ni wapi? Asili yake wapi?Wakati gani usaliti hutokea? Wakati gani mtu anakuwa kigeugeu? Nini hasa chanzo cha chuki kwa wapenzi?

Hakuna maana moja ya mapenzi, ila vyovyote iwavyo mapenzi ni ile hali ya kuvumilia na kukubali mapungufu, udhaifu na karaha za mtu yoyote au hali yeyote au kitu chochote.

Mapungufu, udhaifu na karaha zinapokuwa za kiwango kikubwa na bado ile hali ya uvumilivu na kukubali ikaendelea kuwepo,basi hapo ujue kuwa kiwango cha mapenzi kiko juu sana, na kinyume chake ni kweli. Ukiona mtu yuko na mapungufu na mbaya zaidi ni kero kwako lakini bado wampenda basi ujue kuwa uko na mapenzina huyo mtu.

Mapenzi mahala pake ni moyoni; ambapo si lile pande la nyama lenye vyumba na mishipa ya kutoa na kuingiza damu, bali ni ile roho ambayo ndio asili ya nguvu zote zinazopatikana ndani ya mwili wa mwanadamu. Mwili wa mwanadamu tunaweza kufananisha na kompyuta.

Kopyuta imeundwa na mifumo miwili yenye kutegemeana ambavyo ni hardware na software. Vile vitu tunavyoweza kuvishika na kuviona ndio hardware na vile ambavyo hatuwezi kuviona wala kuvishika ni software. Software ndio huilazimisha hardware nini ifanye, na hardaware hupokea command toka kwa software.

Kwa upande wa mwanadamu kuna roho na mwili. Roho ndio huamuru kitu cha kufanya na katu mwili hauwezi kuiamuru roho kitu cha kufanya. Roho ni kama OS[Operating System] kwa kompyuta.

Kwa mujibu wa mapokeo ya dini za kikristo na kiislamu, mwili wa mwanadamu umeumbwa kutokana udongo, kisha mungu akupulizia pumzi yake kwenye hilo dongo hata likawa mwanadamu mwenye uhai.

Kama nilivyosema awali kuwa roho ni kama OS, na ndani ya OS huweza kuongezwa programu mbalimbali kulingana na uhitaji wa mtumiaji wa kompyuta, pia kwa mwanadamu pia huwa kuna viprogramu vidogodogo vinavyopatikana ndani ya ROHO.

Viproglamu hivyo vidogo vidogo ni kama vile vya kucheka,kununa, kuchukia, kutamani, kupenda, nk, Kila ROHO si lazima iwe na viprogramu hivi vyote, bali zingine huwa na hizi na hukosa zile na zingine hupata zile na hukosa hizi.

Kikubwa cha kufahamu ni kuwa mwanadamu hawezi kucheka kama hana hicho kiprogramu cha kumuwezesha kucheka, kama vile huwezi kuchezesha video kwenye kompyuta yako kama hauna programu ya kukuwezesha kuchezesha video. Watu wengine hawajui kununa na wengine hawajui kucheka pia, hiyo ni kwasababu hakuna kitu hicho cha kununa au kucheka kwenye roho zao. Upendo na chuki ni moja kati ya viprogramu vilivyopo kwenye roho.

SOUL MATE? Class mate humaanisha ni mtu ambaye umesoma naye darasa moja, naam, mlikutana huko darasani. Nini maana ya SOUL MATE? Hivi roho hukutana? Kwa mujibu wa dini ya kiislamu M/Mungu alianza kuziumba roho za viumbe vyote kabla hata ya kuumbwa ulimwengu na ziliishi miaka mingi kabla hata hazijatiwa au kupuliziwa kwenye miili ya viumbe hivyo. Hivyo basi huenda hizo roho zilikutana huko kwa mara ya kwanza.

Katika filamu ya kihindi inayoitwa Dil To Pagal Hai mtunzi ametueleza kuwa roho zimeumbwa katika jozi, yaani mbili mbli huku zikiwa zimenatana. Wakati wa kutiwa kwenye miili ya viumbe zikatenganishwa, moja ikatiwa kwa mwanaume na nyingine ikatiwa kwa mwanamke. Hizi roho mbili lazima zikutane, na kukutana kwenyewe ni kwa watu waliobeba roho hizo kuoana, na ndoa iliyofungwa na watu wenye hizi roho mbili[soulmate] katu hawawezi kuachana.

Usaliti? Kigeugeu? Mara baada ya M/mungu kupulizia pumzi yake kwenye mwili wa mwanadamu, baadaye na hii mara baada ya kutokea uasi mbinguni zikaingia pumzi zingine ngeni kwenye miili ya wanadamu. Pumzi hizi ni majini, au mashetani au mapepo. Hizi pumzi hufanya kazi kama roho ndani ya mwili. Nilisema huko juu kuwa roho huamuru mwili cha kufanya, hivyo na haya majini pia huamuru mwili cha kufanya.

Mkumbuke Hawa na Adamu hawakuwahi kufikiria japo kuusogelea ule mti wa kati, lakini baada ya pumzi mpya kumuingia hawa, si kwamba waliusogolea tu, lakini pia wakala na lile tunda. Roho ya mtu iliumbwa kwa mfano wa Mungu, na kiasilika haiwezi kutenda dhambi au kuacha kumtii Mungu, ila roho ngeni zilizo muingia ndio humfanya atende dhambi, ndio maana twaambiwa kuna pepo la uzinifu, uongo, wizi, na kubwa zaidi roho zetu halaumiwi kwa kutenda dhambi bali zinalaumiwa kwa kushindwa vita na shetani.

Kwakuwa ndani ya mwili tayari kuna roho, na kwakuwa hizi roho ngeni[majini] nazo huamrisha mwili, hivyo basi huwa panatokea mashindano mengi ya kiroho ndani ya mwili wa mwanadamu. Vita???

Mwili siku zote hutii ile roho iliyoshinda haijalishi hiyo roho ni ngeni au ile aloumbiwa mwanadamu. Mfano mwanadamu waweza kutoka kuoga kisha ukajikuta uko katika mtihani wa kuchagua nguo ya kuvaa, wakati mwingine waweza kuvaa nguo kabisa kisha ukajikuta waivua na kuivaa nyingine, ila hali ya kuchagua nivae hii au ile ni matokeo ya mashindano ya kiroho ndani ya mwili, Vita?

Hata katika kuchagua mpenzi pia hutokea mashindano ya kiroho ndani ya mwili. Unapochagua mpenzi na kuamua kuishi naye jua kuwa kuna roho imekushinikiza kufanya hivyo na si vinginevyo. Kwakuwa watu wote tuko na roho ngeni nyingi kwenye miili yetu, kwakuwa hizi roho hutofautiana nguvu kulinganana nyakati, na kwakuwa roho yenye nguvu kwenye wakati fulani ndio hutawala kipindi hicho, hivyo basi kiwango cha “mapenzi” ya mwanadamu kwa mwenza wake hubadilika kadiri roho zinazotawala mwili wa mwanadamu huyo zinavyobadilika;hapa ndipo usaliti na kigeugeu vinapozaliwa.

Wakati wampenda mwajuma elewa kuna kiprogramu[roho] ndani ya mwili wako kimekufanya umpende huyo mwajuma, hiyo roho ikizidiwa nguvu hata ikaingia roho ya kumpenda Asha lazima utamuacha mwajuma na kuanza kumpenda Asha. Hizi roho ngeni ndio hupelekea “soulmate” wakati mwingine zisikutane. Kama ile roho ya inayompenda Asha ikiendelea kutawala kwa muda mrefu hata mauti, basi huyo mtu atendelea kumpenda Asha hadi kifo chake.

Cha kuzingatia, ile roho inayomfanya John ampende Asha haiwezi kufaulu hadi Asha awe na roho inayompenda John. Ikiwa roho hizi ni "SOULMATE" basi mapenzi ya Asha na John hudumu daima, kama hizi roho si "soulmate" na hivyo mapenzi yao ni matokeo ya roho ngeni[majini] zilizopendana, kwa hivyo mapenzi hayo yatachuja na kupotea kabisa mara baada ya roho hizo kutolewa kwenye utawala na roho zingine.

Roho ngeni namaanisha majini au mapepo. Kila mwanadamu ana majini wengi na kila jini kuna mambo anapenda na kuna mambo anachukia, na kila jina kuna siku yake, mwaka wake na hata muongo wake wa kutawala. Pia kila jini ana nguvu zake za kikawaida alizoumbwa nazo na kuna majini wengine wana nguvu za ziada(uchawi)

MWISHO:
katika yote hayo juu, naomba rejea kitendo cha Kefa kumkana Yesu mara tatu, rejea usaliti wa Yuda Iskariote kwa Yesu, rejea vita vya maswahaba baada kifo cha Mtume Muhammad(s.a.w), pia rejea maisha yako kila siku. Utabaini bila jelezi kuwa usaliti, kigeugeu, mapenzi, urafiki, nk vinatawaliwa na majini na roho, na kwasababu hiyo miili yetu haina hiyari hata kidogo.

Siku nyingine nitafafanua uhusiano kati ya majina yetu na mahusiano mapenzi na ndoa. Kwanini watu wengine huchezesha herufi za majina yao au hubadili majina kabisa kwa lengo la kuimarisha ndoa na mahusiano.

PENZI JINI HATARI.
1
Penzi ni jini hatari, wa kutesa na kuua,
Huzibeba zote shari, za kiangazi na mvua,
Nina kuomba Qahari, miye asije niua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
2
Penzi mganga mzuri, huponya wanougua,
Hukusanya nyingi heri, za mwezi hata za jua,
Kwa idhini Ya Jabari, aponye changu kifua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
3
Mapenzi istiimari, hakika nimetambua
Baridi naona hari, meli mwenzenu mashua,
Asali kwangu shubiri, ninajuta kuyajua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
4
Mapenzi ni zingifuri, kwa mja anayejua,
Narauka Alfajiri, naswali naomba dua,
Yarabi penzi la siri, lisije kuniumbua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
5
Penzi si kama johari, huwezi kulinunua,
Si mchanga wa bahari, bure ukalichukua,
Thamaniye si mahari, mkaja hata jazua.
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
6
Penzi halina jabari, si chuma la kuinua,
Uwe bondia hodari, pia laweza sumbua,
Huba zataka sukari, moyo upate kutua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
7
Mapenzi jua qadari, uwaze na kuwazua
Alo lipanga Ghafuri, hakuna wa kupangua,
Hivyo hatuna hiyari, hata kama twaamua
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
8
Mapenzi si kibatari, ni mshumaa tambua,
Nyonda apate fahari, mwenyewe unaungua,
Yengekuwa samsuri, wallahi ningeyavua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
Whatspp/call 0622845394

BINT WA DESMOND TUTU AVULIWA UKASISI KWA KUOA MWANAMKE MWENZAKE.

Binti wa Desmond Tutu, kiongozi mashuhuri wa Kikristo wa Afrika Kusini amevuliwa joho la Ukasisi baada ya kuoa mwanamke mwenzake.

Uongozi wa Kanisa la Anglikana nchini humo umesema, Mchungaji Mpho Tutu-van Furth, Padri wa kanisa hilo amepokonywa leseni ya kuendesha shughuli za kanisa hilo ikiwemo misa, ubatizaji, ndoa na maziko kwa kuwa kanuni za kanisa hilo haziruhusu ndoa za jinsia moja.

Binti huyo amesema babake Desmond Tutu, aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Angilkana nchini humo na pia mwanamapambano mashuhuri wa sera za kibaguzi hajashangazwa na habari hizo ingawa hazijafurahia.

Mpho Tutu alifunga ndoa na raia wa Uholanzi kwa jina Marceline, ambaye ni Profesa wa Tiba ya Watoto huko jijini Amsterdam Disemba mwaka jana, huku sherehe za harusi zikifanyika mjini Cape Town nchini Afrika Kusini mapema mwezi huu. Wanandoa hao waliwahi kuolewa huku nyuma na wote wana watoto.

Ni vyema kuashiria hapa kuwa, licha ya kuwa Kanisa la Angilikana linapinga liwati na usagaji, lakini Afrika Kusini iliidhinisha ndoa za jinsia moja mwaka 2006.

NDEGE YA MISRI ILIDUNGULIWA NA ISRAELI?

Uwezekano kuwa ndege ya abiria ya Misri iliyotoweka hivi karibuni ilitunguliwa na ndege za kivita za Israel, umezidi kupata nguvu.

Gazeti la al Misri al Yaum limeandika kuwa, uchunguzi unaonesha kwamba, kuna uwezekano mkubwa ndege ya abiria ya Egypt Air ilitunguliwa na ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel.

Matamshi rasmi ya viongozi wa Ugiriki kuhusiana na ajali ya ndege ya abiria ya Misri na sababu zake, yamekwepa kwa makusudi kutaja mazoezi ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni yaliyokuwa yanafanyika kusini mwa kisiwa cha Crete cha Ugiriki.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mazoezi hayo ya kijeshi yalifanyika katika kalibu ya mpango wa mafunzo ya ndege za kivita za Israel kwa kutumia mipaka ya angani ya Ugiriki na katika mpaka wa Misri na Libya. Israel iliiomba pia Uturuki iruhusu kutumia anga yake, lakini Uturuki ilikataa.

Gazeti hilo la Misri limeongeza kuwa, ramani ya eneo la mazoezi hayo ya ndege za Israel inaonesha kuwa, ndege hiyo ya Misri ilipita katika eneo hilo wakati mazoezi yakiwa yanaendelea na ilitoweka katika rada dakika 27 baada ya kuanza mazoezi hayo ya kijeshi ya Israel.

KUVURUGA KWA SIMBA, MO ATOA YA MOYONI.


Michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imemalizika hapo jana na Simba SC ikijikuta ikiangukia nafasi ya tatu baada ya kupokea kichapo cha goli 2-1 kutoka kwa JKT Ruvu na hivyo kusalia na alama 62 huku Azam wakifikisha alama 64 na kushika nafasi ya pili baada ya kutoa sare ya goli 1-1 na Mgambo JKT,

Shabiki wa damu wa Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ ameamua kufunguka yaliyo moyoni mwake kutokana na matokeo hayo.

Mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Simba na JKT Ruvu, MO ambaye pia ni Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL Group) alitoa yaliyo moyoni kwake kuhusu Simba kupitia ukurasa wake wa Twitter, ujumbe ambao ulionekana kuwagusa mashabiki wa Simba na wadau wengine wa michezo nchini.

MO aliandika

“#Simba mnatunyima raha, tumechoka kutaniwa na kutukanwa mitaani”

BREAKING NEWS: KITWANGA ATUMBULIWA


Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Charles Kitwanga kwa kosa la kuingia Bungeni akiwa amelewa

ALIYEANDIKA MWANYANGE APINDUE NCHI ATIWA MBARONI.

Jeshi la polisi mkoa wa Arusha linamshikilia mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru aliyejulikana kwa jina la Harold Mmbando (23) kwa kosa la kutoa taarifa za uchochezi dhidi ya Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Mkuu wa majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo alisema kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Mei 17 mwaka huu saa 09:00 asubuhi .
Ameeleza kuwa mtuhumiwa alaindika haya katika mtandao wa Facebook

“Mwamunyange pindua nchi haiwezekani wote wawe nje halafu hakuna aliyepewa mamlaka ya kukalia kile kiti.”

Aidha mtuhumiwa aliandika ujumbe mwingine kuwa

,”Dkt Shein akiuawa kama Karume sitashangaa wala kushtuka naomba Mungu mauaji ya kisiasa yaliyotokea Zanzibar yawe kwa viongozi wa kisasa hasa watawala na sio wananchi wa kawaida”.

Kamanda wa Polisi alisema kuwa, ni vyema wananchi wakatumia mitandao kwa njia iyakayolisaidia taifa badaala ya kutumia kusambaza jumbe za matusi au uchochezi kwani watajikutaka katika mazingira magumu.  

WEMA SEPETU: ALI KIBA WANGU MUMUACHE TU.

Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote

"Ila huyu bichwa wangu mimi ananikoshaga sana. Na mumuachage tu kwakweli. Bichwa una sifa lakini maana si kwa Vocal hizi. Halafu mimi siwezi kukubania namba bana. Naupenda sana huu wimbo jamani. Wajua kutukunaga mashabiki wako. Good work Bichwa wangu Officialalikiba did it again ladiez & Gentlemen"  aliandika Wema Sepetu

Mbali na hilo Wema Sepetu amempa pongezi msanii Alikiba kwa kuweza kusaini mkataba chini ya kampuni ya muziki ya 'Sony Music' na kusema kuwa alistahili hilo na zaidi ya hilo kwani anakipaji kikubwa.

" God Grants accordingly... Congrats Bichwa wangu for that Big Contract... You deserve it & more... Time Heals all wounds... The Sky remains to be the only Limit for u baba..." 

NDEGE YA MISRI YASEMEKANA ILIDUNGULIWA NA MAGAIDI.


Maafisa nchini Uigiriki wanasema vipande viwili “vinavyodhaniwa kuwa mabaki ya ndege ya iliotoweka ya Misri

"yameonekanayakielea katika bahari ya Mediterranean", bado haijabainika kama kweli ni ya ndege hiyo.

Waziri wa uchukuzi wa Misri r Sharif Fathi anasema kuna uwezekano mkubwa kwamba ndege hiyo “iliangushwa na magaidi”, lakini hakuna uwezekano mkubwa wa matatizo ya kiufundi.

Maafisa nchini Uigiriki wanasema ndege hiyo Airbus A320, iligeuka “ nyuzi 90 kushoto na kisha nyuzi 360 kulia kabla ya kutumbukia baharini kutoka umbali wa futi 27, 000.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema ndege hiyo nambari MS804, ilianguka.

HATIMAYE, NDEGE YA MISRI IMEANGUKA BAHARINI.

Hatimaye imethibitika ndege ya Misri imeanguka baharin,juhud za kusaka mabak zaendelea huku kukiwa na hisia za kigaidi.

Ndege hiyo aina ya Airbus A320 ya shirika la ndege la Misri la EgyptAir, iliyokuwa ikitoka mji mkuu wa Ufaransa Paris hadi Cairo awali iliripotiwa kutoweka kutoka kwenye mitambo ya rada.

Ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria 66,na miongoni mwao kulikuwa na watoto 3,wafanyakazi watatu wa usalama na wahudumu saba.

Ndege hiyo ilipaa angani saa 11:09 usiku na ilitoweka ikiwa kilomita 16 ndani ya anga ya Misri na kupoteza mitambo ya rada saa 2:45 asubuhi,afisa mmoja katika shirika hilo la ndege alisema.

Sasa imethibitika ndega hiyo kuanguka bagarini na Operesheni ya kutafuta ndege hiyo imeanzishwa.