BINT WA DESMOND TUTU AVULIWA UKASISI KWA KUOA MWANAMKE MWENZAKE.

Binti wa Desmond Tutu, kiongozi mashuhuri wa Kikristo wa Afrika Kusini amevuliwa joho la Ukasisi baada ya kuoa mwanamke mwenzake.

Uongozi wa Kanisa la Anglikana nchini humo umesema, Mchungaji Mpho Tutu-van Furth, Padri wa kanisa hilo amepokonywa leseni ya kuendesha shughuli za kanisa hilo ikiwemo misa, ubatizaji, ndoa na maziko kwa kuwa kanuni za kanisa hilo haziruhusu ndoa za jinsia moja.

Binti huyo amesema babake Desmond Tutu, aliyekuwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Angilkana nchini humo na pia mwanamapambano mashuhuri wa sera za kibaguzi hajashangazwa na habari hizo ingawa hazijafurahia.

Mpho Tutu alifunga ndoa na raia wa Uholanzi kwa jina Marceline, ambaye ni Profesa wa Tiba ya Watoto huko jijini Amsterdam Disemba mwaka jana, huku sherehe za harusi zikifanyika mjini Cape Town nchini Afrika Kusini mapema mwezi huu. Wanandoa hao waliwahi kuolewa huku nyuma na wote wana watoto.

Ni vyema kuashiria hapa kuwa, licha ya kuwa Kanisa la Angilikana linapinga liwati na usagaji, lakini Afrika Kusini iliidhinisha ndoa za jinsia moja mwaka 2006.

NDEGE YA MISRI ILIDUNGULIWA NA ISRAELI?

Uwezekano kuwa ndege ya abiria ya Misri iliyotoweka hivi karibuni ilitunguliwa na ndege za kivita za Israel, umezidi kupata nguvu.

Gazeti la al Misri al Yaum limeandika kuwa, uchunguzi unaonesha kwamba, kuna uwezekano mkubwa ndege ya abiria ya Egypt Air ilitunguliwa na ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel.

Matamshi rasmi ya viongozi wa Ugiriki kuhusiana na ajali ya ndege ya abiria ya Misri na sababu zake, yamekwepa kwa makusudi kutaja mazoezi ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni yaliyokuwa yanafanyika kusini mwa kisiwa cha Crete cha Ugiriki.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mazoezi hayo ya kijeshi yalifanyika katika kalibu ya mpango wa mafunzo ya ndege za kivita za Israel kwa kutumia mipaka ya angani ya Ugiriki na katika mpaka wa Misri na Libya. Israel iliiomba pia Uturuki iruhusu kutumia anga yake, lakini Uturuki ilikataa.

Gazeti hilo la Misri limeongeza kuwa, ramani ya eneo la mazoezi hayo ya ndege za Israel inaonesha kuwa, ndege hiyo ya Misri ilipita katika eneo hilo wakati mazoezi yakiwa yanaendelea na ilitoweka katika rada dakika 27 baada ya kuanza mazoezi hayo ya kijeshi ya Israel.

KUVURUGA KWA SIMBA, MO ATOA YA MOYONI.


Michezo ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) imemalizika hapo jana na Simba SC ikijikuta ikiangukia nafasi ya tatu baada ya kupokea kichapo cha goli 2-1 kutoka kwa JKT Ruvu na hivyo kusalia na alama 62 huku Azam wakifikisha alama 64 na kushika nafasi ya pili baada ya kutoa sare ya goli 1-1 na Mgambo JKT,

Shabiki wa damu wa Simba, Mohammed Dewji ‘MO’ ameamua kufunguka yaliyo moyoni mwake kutokana na matokeo hayo.

Mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa Simba na JKT Ruvu, MO ambaye pia ni Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Limited (METL Group) alitoa yaliyo moyoni kwake kuhusu Simba kupitia ukurasa wake wa Twitter, ujumbe ambao ulionekana kuwagusa mashabiki wa Simba na wadau wengine wa michezo nchini.

MO aliandika

“#Simba mnatunyima raha, tumechoka kutaniwa na kutukanwa mitaani”

BREAKING NEWS: KITWANGA ATUMBULIWA


Rais Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani Mh. Charles Kitwanga kwa kosa la kuingia Bungeni akiwa amelewa

ALIYEANDIKA MWANYANGE APINDUE NCHI ATIWA MBARONI.

Jeshi la polisi mkoa wa Arusha linamshikilia mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru aliyejulikana kwa jina la Harold Mmbando (23) kwa kosa la kutoa taarifa za uchochezi dhidi ya Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein na Mkuu wa majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Charles Mkumbo alisema kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo Mei 17 mwaka huu saa 09:00 asubuhi .
Ameeleza kuwa mtuhumiwa alaindika haya katika mtandao wa Facebook

“Mwamunyange pindua nchi haiwezekani wote wawe nje halafu hakuna aliyepewa mamlaka ya kukalia kile kiti.”

Aidha mtuhumiwa aliandika ujumbe mwingine kuwa

,”Dkt Shein akiuawa kama Karume sitashangaa wala kushtuka naomba Mungu mauaji ya kisiasa yaliyotokea Zanzibar yawe kwa viongozi wa kisasa hasa watawala na sio wananchi wa kawaida”.

Kamanda wa Polisi alisema kuwa, ni vyema wananchi wakatumia mitandao kwa njia iyakayolisaidia taifa badaala ya kutumia kusambaza jumbe za matusi au uchochezi kwani watajikutaka katika mazingira magumu.  

WEMA SEPETU: ALI KIBA WANGU MUMUACHE TU.

Wema Sepetu amezidi kuonyesha mapenzi aliyonayo kwenye kazi za msanii Alikiba na kusema huwa zinamkosha sana na kudai hajawahi kumuangusha siku zote

"Ila huyu bichwa wangu mimi ananikoshaga sana. Na mumuachage tu kwakweli. Bichwa una sifa lakini maana si kwa Vocal hizi. Halafu mimi siwezi kukubania namba bana. Naupenda sana huu wimbo jamani. Wajua kutukunaga mashabiki wako. Good work Bichwa wangu Officialalikiba did it again ladiez & Gentlemen"  aliandika Wema Sepetu

Mbali na hilo Wema Sepetu amempa pongezi msanii Alikiba kwa kuweza kusaini mkataba chini ya kampuni ya muziki ya 'Sony Music' na kusema kuwa alistahili hilo na zaidi ya hilo kwani anakipaji kikubwa.

" God Grants accordingly... Congrats Bichwa wangu for that Big Contract... You deserve it & more... Time Heals all wounds... The Sky remains to be the only Limit for u baba..." 

NDEGE YA MISRI YASEMEKANA ILIDUNGULIWA NA MAGAIDI.


Maafisa nchini Uigiriki wanasema vipande viwili “vinavyodhaniwa kuwa mabaki ya ndege ya iliotoweka ya Misri

"yameonekanayakielea katika bahari ya Mediterranean", bado haijabainika kama kweli ni ya ndege hiyo.

Waziri wa uchukuzi wa Misri r Sharif Fathi anasema kuna uwezekano mkubwa kwamba ndege hiyo “iliangushwa na magaidi”, lakini hakuna uwezekano mkubwa wa matatizo ya kiufundi.

Maafisa nchini Uigiriki wanasema ndege hiyo Airbus A320, iligeuka “ nyuzi 90 kushoto na kisha nyuzi 360 kulia kabla ya kutumbukia baharini kutoka umbali wa futi 27, 000.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande amesema ndege hiyo nambari MS804, ilianguka.

HATIMAYE, NDEGE YA MISRI IMEANGUKA BAHARINI.

Hatimaye imethibitika ndege ya Misri imeanguka baharin,juhud za kusaka mabak zaendelea huku kukiwa na hisia za kigaidi.

Ndege hiyo aina ya Airbus A320 ya shirika la ndege la Misri la EgyptAir, iliyokuwa ikitoka mji mkuu wa Ufaransa Paris hadi Cairo awali iliripotiwa kutoweka kutoka kwenye mitambo ya rada.

Ndege hiyo ilikuwa imebeba abiria 66,na miongoni mwao kulikuwa na watoto 3,wafanyakazi watatu wa usalama na wahudumu saba.

Ndege hiyo ilipaa angani saa 11:09 usiku na ilitoweka ikiwa kilomita 16 ndani ya anga ya Misri na kupoteza mitambo ya rada saa 2:45 asubuhi,afisa mmoja katika shirika hilo la ndege alisema.

Sasa imethibitika ndega hiyo kuanguka bagarini na Operesheni ya kutafuta ndege hiyo imeanzishwa.

TAARIFA ZA SASA KUHUSU NDEGE YA MISRI ILOPOTEA.


Wanajeshi wa Misri na maafisa wa Uigiriki wanatafuta ndege ya shirika la EgyptAir iliotoweka ikitoka mjini Paris Ufaransa kuelekea Cairo Misri ikiwa na abiria 66.

Ugiriki imetuma ndege mbili na pia itatuma meli moja eneo hilo ili kusaidia utafutaji kwenye bahari ya Mediterranean ambako inaaminika huenda ndege hiyo ilianguka.

Nchini Ufaransa mamlaka zinaandaa mkutano wa dharura kujadili kutoweka kwa ndege hiyo.

Waliokuwemo kwenye ndege hiyo aina ya Airbus A320, ni pamoja na Wamisri 30 Wafaransa 15, Mwingereza 1, Mbelgiji 1,Wairaqi 2, Mkuwait 1, Msaudi 1, Msudan 1,Raia wa Chad 1,Mreno 1,Raia wa Algeria 1, na raia wa Canada 1.

Ilikuwa ikisafiri kutoka Ufaransa kwenda Misri na kutoweka kwenye mtambo wa rada kilomita 280 hivi kabla ya kufika pwani ya Misri.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande na mwenzake wa Misri Abdul Fattah al-Sisi wamewasiliana na kuahidi kushirikiana katika uchunguzi, hayo ni kwa mujibu wa shirika la Reuters .