ROBOTI LENYE HISIA ZA KIBINADAMU LATENGENEZWA CHINA.


Je unaweza tambua roboti kati ya hawa watu kwa hizi picha ? Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia ya China katika mji mkuu wa Hefei, mashariki mwa China  kimezindua roboti kwa jina "Jiajia" ambayo ina uwezo wa mwingiliano na binadamu.

Jiajia ni huyo mwenye mwanamke mwenye nguo nyekundu, anaweza kila kitu ambacho mwanamke anaweza kasoro kubeba mimba tu, lakini hisia za kupenda na kuchukia, hisia za kulala na mwanaume na mengi kama hayo.

Roboti hizo zinauwezo wa kutongoza au kutongozeka, zinaweza kukataa au kukubali inategemea na uwezo wako wa kushawishi.

Bado bei yake haijapangwa, na yapo yanayotengenezwa maalum kwaajili ya Afrika, je yakija Tanzania utanunua?? yakiume pia yatatengenezwa kwaajili ya kazi mbalimbali kama kulima nk.

Watu watabisha lakini mbona wanakula mayai kizungu, kuku za kizungu, sasa kuna ubaya gani mkila na nyapu/zakari za kichina? Au wachina hamuwaamini?

TANZANIA NI YA PILI KWA UZALISHAJI BANGI KWA WINGI AFRIKA.


Polisi nchini Tanzania wameendeleza oparesheni dhidi ya ukuzaji wa bangi pamoja na biashara yake kwenye eneo la Arusha.

Oparesheni hiyo inaendelezwa huku ripoti ya Umoja wa Mataifa ikionyesha kuwa Tanzania ndio mzalishaji mkuu wa pili wa bangi barani Afrika.

Kamanda wa polisi kwenye eneo la Arusha Charlse Mkumbo amesema oparesheni hiyo italenga biashara na ukuzaji wa bangi na miraa.

TETEMEKO LINGINE LIMETOKEA JAPANI.

TETEMEKO LINGINE LIMETOKEA JAPANI.

Tetemeko lignine la ardhi lenye nguvu ya 7.3 kwenye vipimo vya Richter limetokea nchini Japan na kuuwa watu 19 na kusababisha uharibifu mkubwa hayo ni kwa mujibu wa mamlaka nchini humo.  

Tetemeko hilo  lilikukumba kisiwa cha Kyushu ndani ya siku mbili, na kusa sababisha kuporomoka kwa majengo, barabara, mifumo ya maji na umeme.
Wanajeshi 20,000 wametumwa kusaidia juhudi za uokoaji lakini jitihada za uokoaji zimetatizwa na mitetemeko mingine midogo midogo.

Hivi majuzi lilitokea tetemeko Kumamoto hukohuko Japan na kuleta uharibufu na kuua watu, hili sasa lingine, nchi ya Japan inakumbwa na majanga haya kwa mara na kupelekea nchi hiyo kuwa na sheria kali za ujenzi.

GAVANA HUKO MAREKANI ALIGIZA HELKOPTA KUBEBA WALLETI YAKE.


Helikopta ya polisi ilitumwa kuchukua pochi ya gavana wa jimbo moja nchini Marekani, safari iliyogharimu $4,000 (£2,800), uchunguzi umebaini.

Kisa hicho kilitokea mwishoni mwa 2014.
Gavana wa Alabama Robert Bentley aliondoka Tuscaloosa kuelekea kwenye nyumba yake ya ufukweni, mwendo wa saa tano hivi ukitumia gari, lakini akasahau pochi yake.

Aliwataka maafisa wake wa usalama kwenda kuchukua pochi hiyo. Maafisa hao walitumia helikopta hiyo ya polisi, rekodi za safari za ndege zimeonesha.
Bw Bentley anakabiliwa na shinikizo za kumtaka ajiuzulu kutokana na sakata ya unyanyasaji wa kingono.

Lakini anasema hakuagiza ndege itumiwe kwenda kuchukua pochi.
"Niliwaomba tu waende wakachukue pochi yangu, sikuwaambia watumie njia gani,” gavana huyo ameambia mtandao wa AL.com.

„Sikuwaambia watumie helikopta. Ni lazima uwe na pochi yako kwa sababu za kiusalama. Mimi ni gavana. Na ni lazima niwe na pesa. Ni lazima ningenunua kitu cha kula. Na nilihitaji vitambulisho vyangu.”

Tovuti ya AL.com inasema safari hiyo ya helikopta iligharimu mlipa kodi takriban $4,000 (£2,800).

IRAN YAJITAMBA KUWA NA JESHI IMARA NA LENYE NGUVU.

IRAN YAJITAMBA KUWA NA JESHI IMARA NA LENYE NGUVU.

Luteni Kamanda wa Jeshi la Nchi Kavu la Iran amesema kuwa, jeshi hilo liko imara katika kuyalinda Mapinduzi ya Kiislamu na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
Shirika la habari la IRNA limemnukuu Brigedia Jenerali Kiumars Heidari akisema hayo wakati huu wa kukaribia Siku ya Jeshi nchini Iran.

Ameongeza kuwa, jeshi la Iran halizembea hata sekunde moja kuulinda Uislamu na Mapinduzi ya Kiislamu na kwamba kusimama kwake huko imara kunathibitishwa na jinsi jeshi hilo lilivyo na fakhari ya kutoa mashahidi 48 elfu katika njia ya haki.

Brigedia Jenerali Kiumars Heidari ameongeza kuwa, jeshi la Iran lina tofauti kubwa na majeshi ya nchi nyingine duniani na kusisitiza kuwa, leo hii jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limekuwa mtetezi mkubwa wa wanyonge na watu wanaodhulumiwa duniani na limesimama imara kukabiliana na waistikbari na mabeberu na ndio maana linapendwa na linakubalika.

Ikumbukwe kuwa kesho Jumapili inayosadifiana na tarehe 17 Aprili ni siku ya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, siku ambayo huadhimishwa kila mwaka kwa ratiba tofauti.

MALALAMIKO YA WAZIMBABWE KWA SIASA ZA MUGABE.


Wananchi wa Zimbabwe wamefanya maandamano kulalamikia siasa za Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo.
Karibu wafuasi elfu mbili wa chama cha upinzani cha MDC cha Morgan Tsvangirai wamefanya maandamano mjini Harare kulalamikia siasa za Rais Robert Mugabe. Akizungumza mbele ya wafuasi wake Tsvangirai amesisitiza kuwa, Mugabe ameshindwa kutatua mgogoro wa nchi hiyo na kwamba wananchi wa Zimbabwe wanaamini kuwa, serikali yake haina njia nyingine ila kuporomoka tu.

Robert Mugabe ambaye hivi sasa ana umri wa miaka 92, amekuwa rais wa Zimbabwe tangu mwaka 1980. Hali yake tete ya kiafya imepelekea kuzuka maneno mengi kuhusu mtu wa kurithi kiti chake. Kumekuwa na dhana kuwa, Mugabe anafanya mpango wa kumrithisha kiti hicho mkewe, Grace Mugabe. Hata hivyo mwanzoni mwa mwezi uliopita wa Machi, Mugabe alikanusha uvumi huo na kusisitiza kuwa, rais ajaye wa Zimbabwe lazima achaguliwe kwa njia za kidemokrasia.

Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, matamshi hayo ya Mugabe yanaashiria azma yake ya kuendelea kuwa rais wa Zimbabwe hadi mwisho wa maisha yake. Katika hali ambayo duru za kisiasa za nchi hiyo zinafuatilia kwa karibu sana hali ya kiafya ya Mugabe, baadhi ya duru hizo zinaamini kuwa, hatua ya Mugabe ya kushindwa kuainisha mrithi wake itazidi kuitumbukiza katika mgogoro nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.

Hivi sasa hali ya kiuchumi ya Zimbabwe ni ya mgogoro kiasi kwamba baadhi ya ripoti zinaonesha kuwa Zimbabwe ndiyo nchi maskini zai

MAKUMI YA RAIA WAMETIWA MBARONI KWA MAANDAMANO KUMPINGA RAIS WA GAMBIA.


Makumi ya raia wametiwa mbaroni nchini Gambia katika maandamano yaliyofanyika jana ya kumpinga Rais Yahya Jammeh wa nchi hiyo.
Jana maelfu ya wananchi wa Gambia walifanya maandamano wakimpinga Rais wa nchi hiyo Yahya Jammeh.

Maandamano hahayo yalikandamizwa na vikosi vya usalama huku makumi ya waandamanaji wakitiwa mbaroni. Habari kutoka Gambia zinasema kuwa, maandamano hayo ni makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa nchini humo.

Waandamanaji wakiwa wamebeba mabango na maberamu walipiga nara wakipinga sera za Rais huyo na kutoa wito wa kufanyika mageuzi ya kisiasa.

"Wananchi wa Gambia Wanataka Mageuzi ya Kisiasa" ni moja ya maandishi yaliyoonekana katika maberamu yaliyokuwa yamebebwa na waandamanaji hao. Baadhi ya waandamanaji hao wamesema kuwa, Rais jammeh ndio sababu ya hali mbaya ya kiuchumi inayoikabili nchi hiyo.

Baadhi ya waandamaji waliotiwa mbaroni wanaripotiwa kupigwa na kuteswa na vikosi vya usalama baada ya kutiwa mbaroni.

Baadhi ya ripoti zinasema kuwa, Rais Yahya Jammeh aliyekuwa nchini Uturuki kushiriki mkutano wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC amekatisha safari yake yake hiyo na kurejea Gambia.

Rais Jammeh amekuwa akiongoza Gambia kwa mkono wa chuma tangu mwaka 1994.

UNICEF: BOKOHARAM INAWATUMIA KINGONO WASICHANA WA CHIBOK

Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, anayehusika na masuala ya magharibi na katikati mwa Afrika amesema kuwa, wasichana wanaoshikiliwa na kundi la Boko Haram wanabakwa na kudhalilishwa kijinsia na wanamgambo wa kundi hilo.

Manuel Fontaine amesema hayo leo na kuongeza kuwa, wanawake na wasichana wanaotoroka kutoka mikononi mwa kundi hilo maarufu kwa kutenda jinai dhidi ya binaadamu, wameelezea namna wanachama wa kundi hilo walivyokuwa wakiwabaka na kuwalazimisha kutenda vitendo vya ngono bila ya wao kupenda. Kwa mujibu wa wasichana hao, makamanda wa genge hilo walikuwa pia wakiwapatia mafunzo ya kujiripua kwa mabomu. Hii ni katika hali ambayo, ripoti zilizotolewa mwezi Mei mwaka jana zilieleza kuwa, robo tatu ya mashambulio yaliyofanywa na kundi la Boko Haram kuanzia mwaka 2014, yalifanywa na watoto wadogo waliopatiwa mafunzo na magaidi hao.

Ni miaka miwili sasa imepita tangu magaidi hao walipowateka nyara wasichana wa shule moja ya serikali katika mji wa Chibok, kaskazini mashariki mwa Nigeria, huku jamii ya kimataifa ikitaka kuachiliwa huru mara moja wasichana hao.

WAPELISTINA WAANDAMANA KUPINGA UKATILI WA ISRAELI.


Wapalestina wa maeneo tofauti ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan wamefanya maandamano makubwa ya kulaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.

Mwandishi wa shirika la habari la IRIB ameripoti kuwa, jana Ijumaa mamia ya wananchi wa Palestina walifanya maandamano katika maeneo tofauti ya Ukingo wa Magharibi wakiutaka utawala wa Kizayuni wa Israel ukomeshe mara moja ujenzi wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi wanazoporwa Wapalestina.

Waandamanaji hao walipiga nara dhidi ya ya Israel na wametangaza uungaji mkono wao kwa muqawama na Intifadha ya kupambana na utawala wa Kizayuni.

Wanajeshi wa Israel waliwavamia na kuwashambulia kwa risasi waandamanaji hao na kujeruhi Wapalestina kadhaa.

Wakati huo huo mamia ya Wapalestina wamekusanyika mbele ya jengo la Shirika la Msalaba Mwekundu katika Ukanda wa Ghaza wakitaka kuachiliwa huru Wapalestina wenzao wanaoshikiliwa mateka na utawala wa Kizayuni.

Hivi sasa kuna karibu Wapalestina elfu saba wanaoshikiliwa mateka na utawala wa Kizayuni wa Israel katika jela za kuogofya za utawala huo dhalimu.