KOREA KASKAZINI YASHINDWA KUFYATUA MAKOMBORA YAKE YA MASAFA YA WASTANI.


Jaribio la Korea Kaskazini kufyatua kombora la masafa ya wastani kwa jina “Musudan” katika pwani yake ya mashariki, limeshindwa, hayo ni kulingana na, maafisa wa Marekani na Korea Kusini

Shughuli hiyo ilikuwa ikifanyika siku ambayo ni ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa taifa la Korea Kaskazini Kim Il-sung.

Shirika la habari la Korea Kusini Yonhap, likinukuu duru za serikali, limesema kombora hilo lilikuwa aina ya kombora la Musudan, ambalo kitaalamu hujulikana kama BM-25.

Makombora hayo yanaweza kufika umbali wa kilomita 3,000 na kufikia kambi ya majeshi ya Marekani iliyopo kisiwa cha Guam katika bahari ya Pasifiki. Hata hivyo hayawezi kufika Marekani bara.

Hayo ni makombora ya masafa ya wastani, makombora yake ya masafa marefu yanaweza kufika Marekani, hii ina maanisha Korea Kaskazini inaweza kumchapa Mmarekani bila kuhitaji msaada wa uwanja au bahari ya nchi yeyote na Marekani.

Kama mtakumbuka, Marekani ilipigana vita Iraq kwa msaada wa nchi kama Jordan ambazo zilitoa anga na viwanja kwaajili ya matumizi ya kijeshi kwa wamarekani, kama si msaada huo vita ya Iraq isingekuwa nyepesi kwa Marekani.

Marekani na Korea Kusini ndio wanasema hilo Jaribio la Kaskazini limefeli, lakini huwez jua, bado hatuna taarifa kutoka kaskazini, sababu hii huenda ni propaganda tu za Marekani Korea Kusini.

Tusubiri Tuone.


AFIKISHWA KIZIMBANI KWA KUMTUKANA RAIS MAGUFULI FACEBOOK.




KUMAMOTO HALI BADO MBAYA.

KUMAMOTO HALI BADO MBAYA.

Watu tisa wamefariki baada ya tetemeko kubwa la ardhi kuukumba mkoa wa Kumamoto kusini magharibi mwa Japan, huku zaidi ya watu 400 wakiwa wamekimbizwa hospitalini.

Tetemeko hilo lilikuwa na kipimo cha 6.4 katika vipimo vya Richter. Habari zinasema takriban watu 23,000 walitafuta hifadhi kwenye maeneo 350 mkoani humo.

NIGERIA YASISITIZA UDHARULA WA KUPAMBANA NA UGAIDI.

NIGERIA YASISITIZA UDHARULA WA KUPAMBANA NA UGAIDI.

Wizara ya Mambo ya Nje ya Nigeria imesisitiza udharura wa kuzidishwa ushirikiano unaohitajika kati ya nchi za eneo la magharibi mwa Afrika kwa ajili ya kupambana na kundi la Boko Haram.
Taarifa iliyotolewa na wizara hiyo imesema kuwa, kundi la Boko Haram katika kipindi cha miezi iliyopita limepata pigo kubwa kutoka vikosi vya majeshi ya nchi za eneo la magharibi mwa Afrika lakini inasikitisha kuona kuwa, kundi hilo lingali linaendeleza hujuma za kigaidi.

Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Nigeria imeongeza kuwa, maafisa usalama wa Nigeria, Chad na Niger hadi sasa wameshindwa kuratibu oparesheni za majeshi ya nchi hizo dhidi ya Boko Haram katika eneo hilo na hivyo kundi hilo limetumia vibaya nukta hiyo ya udhaifu.

Maafisa usalama wa nchi hizo tatu walikutana mwaka jana huko Abuja, Nigeria kwa lengo la kutathmini oparesheni zao za pamoja dhidi ya kundi la Boko Haram. Japokuwa kituo kikuu cha kundi la Boko Haram kiko huko kaskazini mashariki mwa Nigeria lakini kundi hilo limekuwa pia likifanya mashambulizi ya kigaidi katika nchi jirani.

Baadhi wa wachambuzi wa mambo wanasema kuwa, mapigano na mivutano ya ndani katika baadhi ya nchi za magharibi mwa Afrika kwa upande mmoja, na kutokuwepo uratibu baina ya nchi za eneo hilo kwa ajili ya kupambana kwa pamoja na magaidi hao ni miongoni mwa sababu za kutofanikiwa mapambano ya kuliangamiza kundi hilo.

Sisitizo la Nigeria juu ya udharura wa kuzidishwa ushirikiano baina ya nchi za magharibi mwa Afrika limetolewa huku kundi la Boko Haram likizidisha mashambulizi ya kigaidi katika nchi za eneo hilo licha ya jitihada zinazofanywa na najeshi ya nchi hizo za kukabiliana na wahalifu hao.

Katika kampeni zake za uchaguzi, Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria aliahidi kuwa atakomesha uasi wa kundi la Boko Haram. Hata hivyo hadi sasa jeshi la Nigeria halijapata mafanikio makubwa katika mapambano dhidi ya kundi hilo la kigaidi. Ni kutokana na hali hiyo ndipo weledi wa mambo wanaposisitiza kuwa, kuna udharura wa kuwepo ushirikiano na uratibu wa pamoja kati ya nchi zote za magharibi mwa Afrika kwa ajili ya kung'oa mzizi wa kundi hilo la kigaidi.

Kundi la Boko Haram linaendelea kuwashikia mateka mamia ya wasichana wa shule waliochukuliwa na kundi hilo miaka miwili iliyopita. Jana Jumatano wataalamu wa Umoja wa Mataifa na wataalamu wa haki za binadamu wa Afrika walitoa taarifa ya pamoja wakiashiria suala na kusema kuwa:

Imepita miaka miwili sasa ambapo wapiganaji wa kundi la Boko Haram wanaendelea kuwashikilia mateka wanafunzi wa kike wa shule ya Chibok na hadi sasa hakuna maendeleo ya aina yoyote ya kuweka wazi hali ya wanafunzi hao. Wataalamu hao wameitaka serikali ya Nigeria kuzidisha juhudi za kukomboa wasichana hao.

Kuongezeka kwa mashambulizi ya kigaidi katika maeneo mbalimbali ya dunia na kuimarika na kupanuka zaidi harakati za makundi ya kigaidi hususan katika bara la Afrika lenye utajiri wa maliasili, maeneo ya kistratijia na hitilafu nyingi za kikabila na kikaumu kumeyafanya mataifa na nchi hizo zikabiliwe na tishio kubwa la makundi kama Boko Haram na al Shabab.

Ukweli ni kwamba makundi ya kigaidi yanatishia usalama wa kimataifa na si bara la Afrika pekee, kwa msingi huo kuna udharura wa kuchukuliwa hatua za kimataifa za kukabiliana na janga hilo lisilojua mipaka ya nchi au bara makhsusi.

HUKO BURUNDI AFISA WA CNDD-FDD AUAWA

HUKO BURUNDI AFISA WA CNDD-FDD AUAWA

Afisa wa chama tawala nchini Burundi ameuawa kwa kupigwa risasi, katika kile kinachoonekana ni wimbi la makabiliano ya kulipiza kisasi dhidi ya serikali.

Damien Barindambi, mshirikishi wa wilaya katika eneo la Mutimbuza amesema Phocas Bakaza, mwanachama wa chama tawala CNDD-FDD aliuawa kwa kufyatuliwa risasi jana jioni viungani mwa mji mkuu Bujumbura. Amesema kuwa, watu wawili wamekamatwa kutokana na hujuma hizo zinazoaminika ni za kulipiza kisasi.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 400 wamekwishauawa hadi sasa, tokea Burundi itumbukie kwenye mgorogoro wa wenye kwa wenyewe Aprili mwaka jana. Wizara ya Usalama wa Umma nchini Burundi imetangaza kuendelea machafuko katika maeneo tofauti ya nchi, ambapo watu 46 wameuawa tokea mwanzoni mwa mwaka huu wa 2016 pekee.

Mwaka mmoja umetimia tangu Burundi itumbukie katika hali ya mchafukoge mwezi Aprili mwaka jana, kufuatia hatua ya chama tawala cha CNDD-FDD kumuidhinisha Rais Pierre Nkurunziza kugombea tena urais katika uchaguzi uliopita nchini humo.

MAREKANI NA NCHI ZINAZO MILIKI SILAHA ZA NYUKULIA WAPOKONYWE KUKIDHI TAKWA LA KILIMWENGU.

MAREKANI NA NCHI ZINAZO MILIKI SILAHA ZA NYUKULIA WAPOKONYWE KUKIDHI TAKWA LA KILIMWENGU.

Kupokonywa silaha za nyuklia Marekani na nchi nyingine zinazomiliki sialha hizo ni takwa na hitajio kuu la fikra za waliowengi ulimwenguni.

Gazeti la Resalat linalochapishwa mjini Tehran limeandika leo katika uchambuzi wake kuwa, kupokonywa silaha za nyuklia ni takwa ambalo nchi zinazomiliki silaha za aina hiyo, zikiongozwa na Marekani; zina hofu kubwa kuhusiana na mpango wa kutaka kutekelezwa hatua hiyo.

Gazeti la Resalat limeandika kuwa, kuwepo mamia ya vichwa vya nyuklia ni hatari kwa maisha ya mamilioni ya watu duniani na kwamba suala la kupokonya silaha za nyuklia linapasa kuwekwa katika ajenda ya kazi ya nchi mbalimbali duniani ili kudhamini usalama wa kimataifa.

Gazeti hilo linalochapishwa hapa Tehran limeendelea kuandika kuwa, nchi zinazomiliki silaha haribifu na zilizopigwa marufuku katika hatua yao inayokinzana waziwazi katika kikao cha hivi karibuni cha G-7 huko Hiroshima Japan, zimetaka kuwepo dunia pasina na silaha za nyuklia, katika hali ambayo nchi hizo hazistahiki kuzungumzia suala la kupokonywa silaha za nyuklia ulimwenguni.

Gazeti la Resalat limeongeza kuwa, hatua ya madola yanayomiliki silaha za nyuklia ya kutekelezwa miamala ya kindumakuwili kwa kupuuza maghala ya silaha za nyuklia yanayomilikiwa na utawala wa Kizayuni wa Israel, imeutia kiburi utawala huo na hivyo kutoheshimu taasisi yoyote ya kimataifa ukiwemo Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).

WAASI WA UGANDA WASHAMBULIA MASHARIKI YA DRC.

WAASI WA UGANDA WASHAMBULIA MASHARIKI YA DRC.

Watu kadhaa wameuawa na kujeruhiwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya waasi wa Uganda kufanya mashambulizi kwenye maeneo hayo.

Mtandao wa habari wa Africa Time umezinukuu duru za kijeshi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zikitangaza kuwa, wanajeshi wawili wa nchi hiyo waliuawa jana Jumanne baada ya waasi wa ADF wa Uganda kufanya mashambulizi katika mji wa Opita, kaskazini mwa mkoa wa Kivu Kaskazini, mashariki mwa Kongo na wanajeshi wengine wanne wamejeruhiwa. Hata hivyo duru hizo hazikusema chochote kuhusu hasara walizopata waasi katika mapigano hayo.

Waasi wa Uganda wanaoipinga serikali ya Rais Yoweri Museveni wako mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo tangu mwaka 1995 hadi hivi sasa. Askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa huko Kongo pamoja na serikali ya nchi hiyo wanaamini kuwa waasi hao wa Uganda wamefanya mauaji ya raia 550 katika eneo la Beni huko Kivu Kaskazini tangu mwezi Oktoba 2014 hadi hivi sasa.

Eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetumbukia kwenye machafuko na mashambulio ya waasi kwa miaka 20 sasa. Jeshi la Kongo pamoja na askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa hadi sasa wameshindwa kudhibiti vitendo hivyo vya waasi na kuwaletea amani na usalama wakazi wa maeneo hayo.

KABURI LA PAMOJA LA WATU 350 LAGUNDULIKA KASKAZIN MWA NIGERIA.

KABURI LA PAMOJA LA WATU 350 LAGUNDULIKA KASKAZIN MWA NIGERIA.

Karibu miili 350 ya Waislamu imepatikana ikiwa imezikwa kwa siri katika kaburi la umati kaskazini mwa Nigeria.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Kano, Muhammad Namadi Musa, Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Wafuasi wa Dini Mbalimbali amesema kugunduliwa kaburi hili la umati ni ushahidi wa wazi kuwa mamia ya Waislamu waliuawa Desemba mwaka jana wakati jeshi la Nigeria lilipowashambulia Waislamu wafuasi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria katika jimbo la Zaria.

Katika tukio hilo, jeshi la Nigeria liliwafyatulia risasa wafuasi wa harakati hiyo inayoongozwa na Sheikh Ibrahim Zakzaky ambaye sasa anashikiliwa na jeshi la nchi hiyo akiwa na majeraha na risasi mwilini.

Siku ya Jumatatu mwanaharakati mmoja maarufu wa nchini Uingereza alikosoa vikali ukimya wa jamii ya kimataifa juu ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu nchini Nigeria.

Masoud Shajareh mkuu wa Tume ya Kiislamu ya Haki za Binadamu (IHRC) yenye makao yake London amesema ni miezi kadhaa sasa imepita tangu kujiri mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu nchini Nigeria ambapo hadi sasa ukatili huo haujachunguzwa.

IRAN YASEMA UWEZO WAKE MKUBWA WA KIJESHI SIO TISHIO, BALI WA KIJIHAMI NA FYOKOFYOKO ZA AINA YOYOTE.

IRAN YASEMA UWEZO WAKE MKUBWA WA KIJESHI SIO TISHIO, BALI WA KIJIHAMI NA FYOKOFYOKO ZA AINA YOYOTE.

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) linaendelea na mazoezi makubwa ya kijeshi katika eneo la kusini mashariki mwa nchi.

Luteka hiyo iliyopewa jina la Mtume Mtukufu SAW imeanza Jumanne katika mkoa wa Sistan na Baluchestan ambapo pia kumezinduliwa ndege mpya isiyo na rubani au drone ilioyotengenezwa hapa nchini na yenye uwezo mkubwa.

Drone hiyo ijulikanayo kama Hamasa inatumika kwa mara ya kwanza katika mazoezi ya jeshi baada ya uundwaji wake kutangazwa miaka miwili iliyopita. Drone hiyo ina uwezo mkubwa wa kazi za upelelezi na kurusha makombora mbali na kuwa na uwezo wa kuruka juu sana. Drone zingine zilizotengenezwa nchini Iran zinazotumika katika luteka hiyo ni pamoja na Mohajer, Ababil na Shahed.

Kamanda wa Kikosi cha Nchi Kavu cha IRGC Brigedia Jenerali Mohammad Pakpour amesema mazoezi hayo ya siku tatu yatafanyika pia katika mikoa ya Kerman, Khorasan Kusini na Hormozgan.

Hivi karibuni pia vikosi vya ulinzi vya Iran vilifanya mazoezi na kufanyia majaribio zana za kisasa za kujihami. Machi 9 IRGC ilifanyia majaribio yaliyofana makombora mawili ya balistiki ya Qader-H na Qader-F. Machi nane pia Iran ilifanya majaribio yaliyofana ya kombora la Qiam.

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inasisitiza kuwa uwezo wake mkubwa wa kijeshi si tishio kwa nchi yoyote bali ni kwa ajili ya kujihami.