SIASA MJUE NJIA, MAAMUZI KUFIKIA.
SIASA MJUE NJIA, MAAMUZI KUFIKIA.
1
Nimezama mwituni, kumtafuta mnyama,
Mwenye nguvu duniani, leo na kesho kiama,
Atajwa msikitini, kanisani wa msema,
Haliwi jambo mwituni, bila ya huyo mnyama.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
2
Naanzia shuleni, watoto wanaposoma,
Wanao soma vyuoni, na shahada za heshima,
Ngumbaru ipo kundini, unyago akina mama,
Elimu yetu nchini, huongozwa na mnyama.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
3
Uende sipitalini, na walipo wakulima,
Kwenye sekta ya madini, na kwa wapiga ngoma,
Utalii wa mbugani, uchezaji wa sinema,
Kote huko tambueni, mratibu ni mnyama.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
4
Siasa ndio mnyama, Lutumbo katuambia,
Siasa ni kitu chema, katika yetu dunia,
Siasa njia ya umma, maamuzi kufikia,
Siasa si kama sima, bali maji nawaambia.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
5
Siasa kitu lazima, katu huwezi kimbia,
Waweza ikacha sima, maji huwezi susia,
Hata ngazi ya boma, siasa waitumia,
Siasa ukiitema, jua umeangamia.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
6
Kuna siasa ya chama, kimoja nawaambia,
Kila shauri la umma, chama hujiamulia,
Bunge huwa maamuma, muhuri hushikilia,
Jambo lipite kwa Chama, bunge lalishadidia.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
7
Zipo za demokrasia, vyama vingi nawambia,
Mfano za Tanzania, na uingereza pia,
Vyama hushindania, magogoni kuingia,
Rais kwa Tanzania, waziri kwa malikia
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
8
Siasa ndani ya vyama, huko hazikuanzia,
Ilianza toka zama, kabla ya hino dunia,
Furkani nimeisoma, sikuiacha biblia,
Malaika na Karima, pia wanaitumia,
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
9
Siasa za huko ahera, kiongozi ni Jalia,
Huongoza msafara, waja wakafuatia,
Mwenye kufanya harara, jeuri akajitia,
Atakuwa ni asira, wa shetani nawambia.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
10
Muumba ndio kinara, wa mbinguni na dunia,
Maisha huyachora, na njia hutupangia,
Hupata njema ijara, mwenye kumsujudia,
Hupata kubwa hasara, mwenye kupuuzia.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
11
Nani alipiga kura? Munguwe kumchagua,
Mjibu pasi kufura, kweli mpate ijua,
Hapana si masihara, si punde mtagundua,
Tena sifanye papara, siasa kuchambua.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
12
Siasa za kifalme, mfano za Saudia,
Mwana hasa wa kiume, kiti ndio hukalia,
Koo iloshika kome, dola huishikilia,
Mfalme ndio sime, na pia huwa pazia.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
13
Zipo za kidikteta, kama zile za Mobutu,
Wengine panga hufuta, pia wapo wa mtutu,
Umma wote hufyata, mbele ya miungu watu,
Kila mwenye kutukuta, ni mbwa mbele ya chatu.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
14
Dikteta awe katili, mbona mtaumwa sana,
Siombe awe jahili, mtapoteza amana,
Tena akiwa bahili, wananchi hukondeana,
Kiongozi bahaluli, asiaminiwe tena.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
15
Samaki awape nyoka, mkate awape mawe,
Nani kashindwa ondoka, kisa halina mauwe?
Ya msingi wanataka, viongozi waelewe,
Wakichoka kuboboka, watawapopoa mawe.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
16
Dikteta awe rahimu, ndipo mtanufaika,
Rasini awe timamu, na tena mshaurika,
Mtakula keki tamu, mafurushi mtashika,
Tripoli yajilaumu, Gaddafi kudondoka.
Siasa mjue njia, maamuzi kufikia.
17
Nikitazama chupani, sioni kitu jamani,
Wino wangu wa thamani, ya manjano zafarani,
Niko mengi rasini, wino umetufitini,
Mwenye nao sinihini, naomba niuzieni
Mmeshindwa nidhamini, kwa kifupi kwaherini.
Dotto Chamchua Rangimoto (Njano5)
mzalendo.njano5@gmail.com
0715845394/0784845394/0762845394
Morogoro Tanzania.
BREAKING NEWZ, MAWAZO RUKSA KUAGWA.
Polisi waangukia meno ya mbele Mahakamani...wao na waliowatuma kuzuia Mawazo asiagwe!
Alphonce Mawazo ataagwa kishujaa Jijini Mwanza kama ilivyooangwa na familia na Chadema baada ya Mahakama kuridhika kuwa wanahaki ya Kikatiba kumuaga mpendwa wao. Polisi inajukumu la kulinda amani na utulivu wakati wa shughuli hiyo.
NDESAMBURO ATOA MASHARTI MAGUMU CHADEMA.
NDESAMBURO ATOA MASHARTI MAGUMU CHADEMA.
Mdhamini mkubwa wa CHADEMA mh. Ndesamburo atoa masharti magumu kwa chadema baada ya Binti yake Lucy Owenya kukosa Ubunge wa viti maalum.
Mpashaji wetu ameieleza Kisima kuwa Ndesamburo alimwita Mbowe Moshi na kumpa masharti makali kuwa kama Binti yake Lucy Owenya hatapata Ubunge atasitisha misaada na kuipeleka kwa kwa chama cha ACT wazalendo kumuongezea nguvu Zitto Kabwe, na kutangaza rasmi Vita na chadema.
Hata hivyo Mbowe aliomba radhi na akamwambia mchakato wa viti maalum haufanywi na mtu mmoja, bali kuna taratibu ndani ya chama na NEC pia. Hata hivyo inaonekana nia ya Mbowe ilikuwa kuwatupia zigo Tume ya Uchaguzi, jambo ambalo sio kweli.
Baada ya mazungumzo yote walihitimisha kwa kukubaliana. Mbowe aliomba radhi na kukubali kuyatekeleza masharti, kwa kuanza kumtoa Lucy Owenya nafasi ya 39 na kumshusha hadi nafasi ya 37 ya orodha ya mpangilio wao wa viti maalum . Nafasi ya 37 inamfanya Lucy kuwa mtu wa Kwanza katika viti maalum vipya watakavopata chadema baada ya kumalizika uchaguzi huu unaoendelea desemba 20. Kama tutakumbuka tume ya Uchaguzi walibakiza viti vitatu kutovigawa ndio hivyo ambavyo wanategemea kimoja wampe Lucy endapo wataongeza asilimia za kura za kupata sifa kupata viti maalum hivyo.
Pamoja na hayo inasemekana sababu iliyo sababisha Lucy Owenya akose nafasi ya kiti maalum ni ukaribu wake na mwanasiasa machachari Zitto Kabwe, hongera yake Lucy Owenya kwa kupewa matumaini na poleni madada wa CHADEMA ambao mlikuwa nafasi ya 37 na 38. Lucy Owenya kachukua nafasi yenu, midhali ni maamuzi ya chama, hamna budi ya kuyakubali na kuongeza juhudi zenu katika ujenzi wa chama.
Kisima Cha Jangwani.
Baada ya mazungumzo yote walihitimisha kwa kukubaliana. Mbowe aliomba radhi na kukubali kuyatekeleza masharti, kwa kuanza kumtoa Lucy Owenya nafasi ya 39 na kumshusha hadi nafasi ya 37 ya orodha ya mpangilio wao wa viti maalum . Nafasi ya 37 inamfanya Lucy kuwa mtu wa Kwanza katika viti maalum vipya watakavopata chadema baada ya kumalizika uchaguzi huu unaoendelea desemba 20. Kama tutakumbuka tume ya Uchaguzi walibakiza viti vitatu kutovigawa ndio hivyo ambavyo wanategemea kimoja wampe Lucy endapo wataongeza asilimia za kura za kupata sifa kupata viti maalum hivyo.
Pamoja na hayo inasemekana sababu iliyo sababisha Lucy Owenya akose nafasi ya kiti maalum ni ukaribu wake na mwanasiasa machachari Zitto Kabwe, hongera yake Lucy Owenya kwa kupewa matumaini na poleni madada wa CHADEMA ambao mlikuwa nafasi ya 37 na 38. Lucy Owenya kachukua nafasi yenu, midhali ni maamuzi ya chama, hamna budi ya kuyakubali na kuongeza juhudi zenu katika ujenzi wa chama.
Kisima Cha Jangwani.
LOWASSA AWAPIGA CHENGA P0LISI.
LOWASSA AWAPIGA CHENGA P0LISI.
Hivi karibuni aliyekuwa mgombea wa UKAWA, Lowassa aliwaambia Polisi Jijini Mwanza kuwa Chadema haihitaji ulinzi wao kufanya matukio yake kuwa salama. Rekodi zote za vurugu huanzishwa na Polisi wenyewe...
Jana alithibitisha hilo mjini Kahama baada ya kuwapiga chenga ya mwili na kwenda hospitali bila escot yao kwake kama Waziri Mkuu mstaafu.
Baadae Polisi wakamfuatilia nyuma nyuma akiwa anarudi.. Msafara wake ukatoka nduki na kuwaacha maboya tena polisi hao.
***
Nipashe lina stori zaidi.
BRAKING NEWZ, EXPLOTION KILS KDF GARISSA
#BreakingNews: IED explosion kills KDF soldier, wounds six others in #Garissa County.
Habari kamili na picha baadae,
WAZIRI MKUU AANZA KAZI KWA MKWARA
WAZIRI MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amewataka wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu watambue jukumu walilonalo la kuwahudumia wananchi kutokana na majukumu ya ofisi hiyo ambayo yanagusa maisha ya kila siku ya Watanzania.
“Ofisi ya Waziri Mkuu ni kubwa na pana sana na inahusika na shughuli za kila siku za Watanzania. Kwa hiyo tuna kazi kubwa ya kukidhi matarajio yao,” alisema.
Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumatatu, Novemba 23, 2015) wakati akizungumza na wakuu wa taasisi, wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye mkutano uliofanyika ofisini kwake, Magogoni, jijini Dar es Salaam. Leo ndiyo ameripoti kwa mara ya kwanza tangu alipoapishwa Ijumaa iliyopita kwenye Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma.
Pamoja na
kazi nyingine tunayo majukumu makubwa ambayo ni udhibiti, usimamizi na
ufuatiliaji wa masuala mbalimbali humu Serikalini. Ninataraji kupata
mpango kazi kutoka kwa Mkuu wa kila idara na kila taasisi zilizo chini
ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Nitakwenda pia ofisi za TAMISEMI ili kuweka
vipaumbele vyetu sawa,” alisema.
Aliwataka watumishi hao wawe tayari kutekeleza kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ ambayo imekuwa ikisisitizwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ili kuweza kumudu kasi ya utendaji kazi Serikali ambayo anaihimiza hivi sasa.
Alisema ana imani kuwa watumishi hao watampa ushirikiano kama ambavyo walikuwa wakiutoa kwa mtangulizi wake, Mhe. Mizengo Pinda ambaye amestaafu hivi karibuni.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMATATU, NOVEMBA 23, 2015.
Aliwataka watumishi hao wawe tayari kutekeleza kaulimbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ ambayo imekuwa ikisisitizwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli ili kuweza kumudu kasi ya utendaji kazi Serikali ambayo anaihimiza hivi sasa.
Alisema ana imani kuwa watumishi hao watampa ushirikiano kama ambavyo walikuwa wakiutoa kwa mtangulizi wake, Mhe. Mizengo Pinda ambaye amestaafu hivi karibuni.
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
2 MTAA WA MAGOGONI,
S. L. P. 3021,
11410 DAR ES SALAAM
JUMATATU, NOVEMBA 23, 2015.
SHEREHE ZA UHURU ZAFUTWA MWAKA HUU.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kwa mujibu wa Sheria ya Sikukuu za Kitaifa (The Public Holidays Act, Cap 35) pamoja na Sheria zingine zinazompa mamlaka Rais kutangaza siku yoyote kuwa sikukuu au mapumziko, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ameamua kuwa maadhimisho ya Sherehe za Uhuru na Jamhuri zitakazofanyika tarehe 9 Desemba, 2015, yatumike kwa kufanya kazi. Kwamba maadhimisho ya Uhuru ya mwaka huu (2015) yatatumika kama kichocheo cha kujenga tabia ya kufanya kazi (Uhuru na Kazi) katika Taifa letu.
Mheshimiwa Rais ameelekeza Watanzania wote siku hiyo waitumie kwa
kufanya kazi mbalimbali kama vile, mashambani, maofisini, sokoni,
viwandani na usafi wa miji yao katika kutimiza dhana ya Uhuru na Kazi
kwa vitendo.
Aidha, kwa kuwa Sherehe za Uhuru na Jamhuri huendana na Maandalizi mbalimbali ambayo yanatumia fedha, kwa kuzingatia kuwa siku hiyo itaadhimishwa kwa kufanya kazi, fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe hiyo sasa zitumike kwa shughuli zingine za kijamii ikiwa ni pamoja na kupambana na maradhi hasa kipindupindu, kununulia dawa za hospitali, vitanda vya hospitali n.k. kadri kamati za maandalizi zitakavyoamua.
Ieleweke kuwa sherehe za Uhuru na Jamhuri ni muhimu katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa nchi yetu. Hivyo, sherehe hizi zitaendelea kuadhimishwa kila mwaka kama kawaida kuanzia mwaka 2016.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
23 Novemba, 2015
Aidha, kwa kuwa Sherehe za Uhuru na Jamhuri huendana na Maandalizi mbalimbali ambayo yanatumia fedha, kwa kuzingatia kuwa siku hiyo itaadhimishwa kwa kufanya kazi, fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya sherehe hiyo sasa zitumike kwa shughuli zingine za kijamii ikiwa ni pamoja na kupambana na maradhi hasa kipindupindu, kununulia dawa za hospitali, vitanda vya hospitali n.k. kadri kamati za maandalizi zitakavyoamua.
Ieleweke kuwa sherehe za Uhuru na Jamhuri ni muhimu katika kuadhimisha kumbukumbu ya uhuru wa nchi yetu. Hivyo, sherehe hizi zitaendelea kuadhimishwa kila mwaka kama kawaida kuanzia mwaka 2016.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
23 Novemba, 2015
KATIBU MKUU KIONGOZI AAGIZA WATUMISHI WA UMMA WAVAE SARE.
KATIBU MKUU KIONGOZI AAGIZA WATUMISHI WA UMMA WAVAE SARE.
Katibu mkuu kiongozi Ombeni Sefue ameagiza watumishi umma kuvaa sare maalum wanapokuwa kazini, lengo kubwa wapate kujulikana kwa urais na wateja wao.
MAGUFULI ABATILISHA HATI ZA UMILIKI WA ARDHI ZISIZO ENDELEZWA
Taarifa inatolewa kwa umma kwamba, Miliki za viwanja na mashamba zilizoorodheshwa katika jedwali, zimebatilishwa kutokana na ukiukwaji wa kumiliki ardhi.
Inasemekana wale wote ambao wanamiliki viwanja kwa muda mrefu na hawajaviendeleza, kuna mpango wa kunyang'anywa. Taarifa hii inatolewa kwa mujibu wa fungu la 49(1) la sheria ya ardhi sura
(113)
Subscribe to:
Posts (Atom)