Showing posts with label Mashairi. Show all posts
Showing posts with label Mashairi. Show all posts

NIMETAFAKARI SANA.

Kumekucha ni salama, ahsante mungu wangu,
Japo dede nasimama, na tete hatua zangu,
Nina kuomba Karima, nifike safari yangu
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Jana sikupe hasira, leo sipate karaha,
Tena sifanye harara, kesho upate furaha,
Kiumbe fanya subira, kama wazitaka raha.
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Aliyeumba kinyonga, ndiye kaumba farasi,
Lumbwi siwezi jinyonga, kulilia kwenda kasi,
Karima ndiye hupanga, ndogo nyingi na kiasi,
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Namtazama jongoo, kunako miguu yake,
Ilivyo kama pongoo, ajabu ni mwendo wake
Kamzidi kangaroo, lakini si mbio zake,
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Sijaona uwaridi, lisilo kuwa na miba,
Ama jambo maridadi, baya liwate kubeba,
Jua kuna kujirudi, ndio ikawepo toba,
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Mja usiwe bahili, pia usifanye ria,
Ila sianguke chali, asama kusaidia,
Moyo usizidi hali, Mola alokujalia,
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Kaditama namaliza, hapa natia kikomo,
Shika nilo yawaza, huenda tapata somo,
Kuuliza unaweza, zingatia yaliyomo,
Nimezama fikirani, nawaza mie nawaza.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
Whatspp/call 0622845394 Morogoro

KISO CHAKO HUKISHIKI

Ufanye uende mbio, kaskazi mashariki,
Ubebe na kuku kwio, kwa ndumba unihiliki,
Yote yawa kifagio, kwa uwezo wa Maliki,
Jalali sio babio, elewa sihadhiriki.
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Mja kalisha kalio, hazina pato shiriki,
Fanya uweke fungio, huta zuia riziki
Waja angua kilio, useme na hizo chuki,
Mola wangu kimbilio, wallahi sifedheheki,
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Nimegundua mwenzio, tabasamu lako feki,
Watia kinukajio, kwa chips na mishikaki,
Umepaka kipambio, sumu nipate fariki,
Rabi kahuluku "sio" ndio mana sianguki
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Ulo nalo kusudio, fahamu halisomeki,
Uweke na kikingio, kiso chako hukishiki,
Ingia kwa kitubio, umrudie Razaki,
Jalali kaumba "ndio" kwahivyo sitetereki.
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Wanisema kwa wenzio, vile isivyo stahiki,
Mithili ya kisusio, mdomoni sikutoki,
Neno mwenziwe sikio, halichomi si mkuki,
Mungu tanipa tulio, hakika sibabaiki.
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Umeshika mchinjio, na bado haushutuki,
Chakughuri kilalio, kiumbe hauzinduki,
Punguza matamanio, dunia haibebeki,
Rabi nipe kifutio, nifute zako falaki
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Alokupa mtwangio, na kinu simdhihaki,
Kuna siku ya chungio, kiumbe huiepuki,
Hivyo situpe dekio, kesho haitabiriki,
Hapa pana zingatio, wajibu nduguye haki,
Kiso chako hukishiki, hata kwa lake shikio.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
0622845394 Morogoro

MSUKUMA HABARI YAKO.


1
Mpemba sabalheri, unaionaje hali,
Kwangu mie ni buheri, namshukuru Jalali,
Usiwe na munkari, lijibu langu suali,
Kwanini wapenda shari, kama vile hauswali?
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
2
Mgogo habari yako, salamu zangu pokea,
Hapa nina swali lako, lile ulilo zoea,
Kuomba silika yako? jibu ninalingojea,
Lini unarudi kwako? Dom ulipotokea?
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
3
Mtumbatu nampenda, wenzangu naweka wazi,
Mtu huyu hana inda, tena hana utalazi,
Mwaminifu kama kunda, akiwa na laazizi,
Sishangae akikonda, sababu ya mkumbazi.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
4
Mmakunduchi mpole, si mwepesi kuchukia,
Tena hapendi kelele, na fujo kuzisikia,
Aenda huku na kule, kuti ajitafutia,
Ila mvivu kwa shule, umande aukimbia,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
5
Mzaramo sikupati, zinduka silale doro,
Uwate tupu kibeti, isifike yako soro,
Wapenda kichenipati, watoto wakosa karo,
Unalitunza kabati, nguo waweka kwa poro,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
6
Msukuma simsemi, ila ukweli nampa,
Sio kwamba hajitumi, tatizo ni zake pupa,
Pombe ageuza maji, huku nguo azitupa,
Akifika kwenye lami, anayavua malapa.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
7
Mnyakyusa kwa vioja, hakuna wa kumpata,
Fulusi anazifuja, kama vile aokota,
Aagizia mapaja, jikoni yalo tokota,
Anywa supu kwa mrija,soda kwake tarumbeta,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
8
Mhaya apenda sifa, tena kupita kiasi,
Aweza lalia fafa, kibanda chake cha nyasi,
Pia asiwe na sofa, masikini si mkwasi,
Atatamba sio lofa, ana kasri Parisi
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
9
Mhehe si mchokoze, hasa yule wa Kalenga,
Tena simgombeze, usimfanyie ngenga,
Hujui na nikujuze, mwepesi wa kujinyonga,
Kosa lake mueleze, maneno ukiyachunga.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
10
Mkuriya ana nini, leo nataka ukweli,
Kila siku gazetini, mara lile mara hili,
Kumwaga damu mwilini, kwake yeye ni sahali,
Ana tatizo rasini, kiasi aitwe nduli,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
11
Mluguru kwa kulima, mwenzenu nampongeza,
Gimbimaji na mlima, kuchemsha anaweza,
Wali wake kama sima, wallahi hutaongeza,
Atasema kwa heshima, mkono umeteleza,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
12
Mchaga toka Machame, aongoza ubahili,
Yu tayari akuchome, kikubwa apate dili,
Asemwa ni gumegume, ati ni yake asili,
Kama mate umteme, kiumbe huyu katili,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
13
Mha atege sikio, nisemalo asikie,
Anajua kwenda mbio, lengo lake litimie,
Afanye watu fagio, njia wamsafishie
Apate mafanikio, awaacha wajifie.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
14
Mkwere ana maneno, huyasema rejareja,
Kwa mithali na mifano, huzichanganya lahaja,
Kesha maliza matano, weye huna hata moja,
Vile bila ndoano, ajipatia kangaja,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
15
Mnyamwezi kwa ushamba, nadhani atia fora,
Avae apige pamba, utacheka kama jura,
Akiwa alima shamba, anaruka kama chura,
BASATA wakimbamba, 'taungana na Snura.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
16
Mdigo yule wa Tanga, asifika kwa kupika,
Uchungu wote wa chunga, kirahisi inalika,
Kwa mapenzi ndio nanga, ukizama hutatoka,
Ukikutoka ujinga, nguo anaziloweka,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
17
Mpare wa milimani, analima tangawizi,
Anashangaza jamani, chai yake ya mluzi,
Haipiki na majani, yaani hata mizizi,
Wanayo fikira gani, mjue sijamaizi,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
18
Mfipa kwake Mpanda, Mpimbwe na Sumbawanga,
Kibeku anakipanda, anapaa akiwanga,
Hufanya analopenda, kwa tunguri na usinga,
Akitaka kukuwinda, anakuchinjia ninga.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
19
Mmakonde mla panya, ati samaki mchanga,
Leo mimi nakukanya, ndugu yangu wa Nambunga,
Hebu jaribu kufanya, uvue japo mkunga,
Rohoni nimekusinya, natamani kukutenga.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
20.
Kaditama samahani, nyie nilio wakwaza,
Mimi ni wenu mtani, sio yule wa Vigwaza,
Natokea undambani, Ifakara si Muheza,
Msiweke mtimani, lengo si kuwachokoza.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
whatspp/call 0622845394 Morogoro.

MSUKUMA HABARI YAKO.


















MSUKUMA HABARI YAKO.
1
Mpemba sabalheri, unaionaje hali,
Kwangu mie ni buheri, namshukuru Jalali,
Usiwe na munkari, lijibu langu suali,
Kwanini wapenda shari, kama vile hauswali?
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
2
Mgogo habari yako, salamu zangu pokea,
Hapa nina swali lako, lile ulilo zoea,
Kuomba silika yako? jibu ninalingojea,
Lini unarudi kwako? Dom ulipotokea?
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
3
Mtumbatu nampenda, wenzangu naweka wazi,
Mtu huyu hana inda, tena hana utalazi,
Mwaminifu kama kunda, akiwa na laazizi,
Sishangae akikonda, sababu ya mkumbazi.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
4
Mmakunduchi mpole, si mwepesi kuchukia,
Tena hapendi kelele, na fujo kuzisikia,
Aenda huku na kule, kuti ajitafutia,
Ila mvivu kwa shule, umande aukimbia,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
5
Mzaramo sikupati, zinduka silale doro,
Uwate tupu kibeti, isifike yako soro,
Wapenda kichenipati, watoto wakosa karo,
Unalitunza kabati, nguo waweka kwa poro,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
6
Msukuma simsemi, ila ukweli nampa,
Sio kwamba hajitumi, tatizo ni zake pupa,
Pombe ageuza maji, huku nguo azitupa,
Akifika kwenye lami, anayavua malapa.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
7
Mnyakyusa kwa vioja, hakuna wa kumpata,
Fulusi anazifuja, kama vile aokota,
Aagizia mapaja, jikoni yalo tokota,
Anywa supu kwa mrija,soda kwake tarumbeta,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
8
Mhaya apenda sifa, tena kupita kiasi,
Aweza lalia fafa, kibanda chake cha nyasi,
Pia asiwe na sofa, masikini si mkwasi,
Atatamba sio lofa, ana kasri Parisi
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
9
Mhehe si mchokoze, hasa yule wa Kalenga,
Tena simgombeze, usimfanyie ngenga,
Hujui na nikujuze, mwepesi wa kujinyonga,
Kosa lake mueleze, maneno ukiyachunga.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
10
Mkuriya ana nini, leo nataka ukweli,
Kila siku gazetini, mara lile mara hili,
Kumwaga damu mwilini, kwake yeye ni sahali,
Ana tatizo rasini, kiasi aitwe nduli,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
11
Mluguru kwa kulima, mwenzenu nampongeza,
Gimbimaji na mlima, kuchemsha anaweza,
Wali wake kama sima, wallahi hutaongeza,
Atasema kwa heshima, mkono umeteleza,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
12
Mchaga toka Machame, aongoza ubahili,
Yu tayari akuchome, kikubwa apate dili,
Asemwa ni gumegume, ati ni yake asili,
Kama mate umteme, kiumbe huyu katili,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
13
Mha atege sikio, nisemalo asikie,
Anajua kwenda mbio, lengo lake litimie,
Afanye watu fagio, njia wamsafishie
Apate mafanikio, awaacha wajifie.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
14
Mkwere ana maneno, huyasema rejareja,
Kwa mithali na mifano, huzichanganya lahaja,
Kesha maliza matano, weye huna hata moja,
Vile bila ndoano, ajipatia kangaja,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
15
Mnyamwezi kwa ushamba, nadhani atia fora,
Avae apige pamba, utacheka kama jura,
Akiwa alima shamba, anaruka kama chura,
BASATA wakimbamba, 'taungana na Snura.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
16
Mdigo yule wa Tanga, asifika kwa kupika,
Uchungu wote wa chunga, kirahisi inalika,
Kwa mapenzi ndio nanga, ukizama hutatoka,
Ukikutoka ujinga, nguo anaziloweka,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
17
Mpare wa milimani, analima tangawizi,
Anashangaza jamani, chai yake ya mluzi,
Haipiki na majani, yaani hata mizizi,
Wanayo fikira gani, mjue sijamaizi,
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
18
Mfipa kwake Mpanda, Mpimbwe na Sumbawanga,
Kibeku anakipanda, anapaa akiwanga,
Hufanya analopenda, kwa tunguri na usinga,
Akitaka kukuwinda, anakuchinjia ninga.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
19
Mmakonde mla panya, ati samaki mchanga,
Leo mimi nakukanya, ndugu yangu wa Nambunga,
Hebu jaribu kufanya, uvue japo mkunga,
Rohoni nimekusinya, natamani kukutenga.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.
20.
Kaditama samahani, nyie nilio wakwaza,
Mimi ni wenu mtani, sio yule wa Vigwaza,
Natokea undambani, Ifakara si Muheza,
Msiweke mtimani, lengo si kuwachokoza.
Nang'ata na kupuliza, utani nawatania.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
whatspp/call 0622845394 Morogoro.

PENZI JINI HATARI.

PENZI JINI HATARI.
1
Penzi ni jini hatari, wa kutesa na kuua,
Huzibeba zote shari, za kiangazi na mvua,
Nina kuomba Qahari, miye asije niua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
2
Penzi mganga mzuri, huponya wanougua,
Hukusanya nyingi heri, za mwezi hata za jua,
Kwa idhini Ya Jabari, aponye changu kifua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
3
Mapenzi istiimari, hakika nimetambua
Baridi naona hari, meli mwenzenu mashua,
Asali kwangu shubiri, ninajuta kuyajua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
4
Mapenzi ni zingifuri, kwa mja anayejua,
Narauka Alfajiri, naswali naomba dua,
Yarabi penzi la siri, lisije kuniumbua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
5
Penzi si kama johari, huwezi kulinunua,
Si mchanga wa bahari, bure ukalichukua,
Thamaniye si mahari, mkaja hata jazua.
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
6
Penzi halina jabari, si chuma la kuinua,
Uwe bondia hodari, pia laweza sumbua,
Huba zataka sukari, moyo upate kutua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
7
Mapenzi jua qadari, uwaze na kuwazua
Alo lipanga Ghafuri, hakuna wa kupangua,
Hivyo hatuna hiyari, hata kama twaamua
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.
8
Mapenzi si kibatari, ni mshumaa tambua,
Nyonda apate fahari, mwenyewe unaungua,
Yengekuwa samsuri, wallahi ningeyavua,
Mahaba yanizuzua, mtima wata ghururi.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
0622845394

MWANANGU SEMA AMINI.














MWANANGU SEMA AMINI.
1
Mwana ninaye kupenda, naomba sema amini,
Mungu anaye tulinda, akukinge na majini,
Wale wanao kuwinda, Rabi awabwage chini.
Namuomba Rahmani, akupe walau shinda.
2
Uvune ulichopanda, shuke moja themanini,
Kama ni nyavu watanda, uwe kingi baharini,
Iwe unafuga kunda, watotoe ishirini,
Namuomba Rahmani, akupe walau shinda.
3
Wanotaka kukuponda, wasiweze abadani,
Viumbe wafanya inda, hasa wale mafatani,
Mwanangu utawashinda, kwa uwezo wa Manani,
Namuomba Rahmani, akupe walau shinda.
4
Tazama unavyoenda, sema na wayo njiani,
Njia ni sawa kupinda, isikutoe imani,
Allah atakulinda, uishinde mitihani,
Namuomba Rahmani, akupe walau shinda.
5
Kiti usije kukonda, kwa kudekeza lohani
Yote unayoyatenda, yakufae maishani,
Usije ukawa punda, faida ya Baniani,
Namuomba Rahmani, akupe walau shinda.


Dotto Chamchua Rangimoto(Njano5)
0622845394/0784845394 Morogoro
MWANANGU SEMA AMINI

NAMPENDA MMOJA, NAYE ANAJUA.


















NAMPENDA MMOJA, NAYE ANAJUA.

Kiumbe silete hoja, sikiza nakuambia,
Nimpendaye mmoja, moyoni alonitia,
Hao unao wataja, si wangu wanizushia.
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Apendeza bila koja, wallahi ametimia,
Si usoni hata paja, kila kitu avutia
Nikimuita yuaja, mtiifu wa tabia,
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Hili jambo lina tija, mimi nilo kusudia,
Nimeshatoa mkaja, mahari yafuatia,
Nimeuchoka useja, wa mito kukumbatia,
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Muogope sana mja, mama aliniusia
Haishiwi na harija, mapenzi kukuvunjia
Hatimaye huwa chaja, muhibu awe nokia,
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Kwahivyo sioni haja, ya jina kukutajia,
Kutotaja sikuroja, ni mafunzo ya nabia,
Naomba sikose kuja, hiyo siku kiwadia,
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Ukome kutajataja, njia ni'zo zipitia,
Hayo unayo bwabwaja, yasije kumfikia,
Tungule iwe tunguja, iso faa kupikia,
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Naapa sitakufuja, ulipo nyonda sikia,
Mahaba hayatachuja, kama safi zetu nia,
Lije vumba la kangaja, jua nitavumilia,
Jina sitakutajia, nimpendaye mmoja.

Dotto Rangimoto Chamchua(Njano5)
0622845394
Morogoro.

TANZANIA NAKUPENDA SANA.



















TANZANIA NAKUPENDA SANA.
Mama Tanzania, nakupenda sana,
Nakupigania, usiku mtana,
Zitaangamia, husuda fitina,
Za walo pania, watu kuchinjana
Nakupenda sana, wangu Tanzania.


Siwati kulia, tunapo zozana,
Huomba Jalia, tupate patana,
Tusiwape ndia, wafanya hiyana,
Wapate kimbia, wasirudi tena.
Nakupenda sana, wangu Tanzania.

Siasa ni njia, ya kuongozana,
Katu si jambia, roho kutoana,
Yataka sikia, kushauriana,
Mambo hutimia, kwa kusikizana.
Nakupenda sana, wangu Tanzania.

Ninajivunia, kuwa wako mwana,
Katika Dunia, hata kwa Rabana,
Mi husimulia, Ulaya na China,
Mola kajalia, vitu vingi sana.
Nakupenda sana, wangu Tanzania.

Dotto Rangimoto Chamchua (Njano5)
0622845394/0784845394 Morogoro.

UKIONACHO NDOTONI.








  






        


UKIONACHO NDOTONI.

Kiona choo ndotoni, kiumbe sikitumie,
Haja iwe mlangoni, kazana ishikilie,
Tena fanya hukioni, shukani siyaachie.
Yataka uzingatie, uyaonayo ndotoni.

Kiona kiza ndotoni, mwenzangu usiumie,
Mfano mwanga uoni, pambana ukufikie,
Swali utoke shimoni, Rabi akuangazie
Yataka uzingatie, uyaonayo ndotoni.

Kiona simba ndotoni, naomba simkimbie,
Mrukie mgongoni, kipando ujifanyie,
Uwatazame usoni, maadui wazimie,
Yataka uzingatie, uyaonayo ndotoni.

Kiona swala ndotoni, kichale umnyatie,
Sije zama mtegoni, kijanja mkaribie
Mtazame pasi soni, asiwe chui ulie,
Yataka uzingatie, uyaonayo ndotoni.

Dotto Rangimoto Chamchua.(Njano5)
mzalendo.njano5@gmail.com
0762845394/0784845394
Morogoro Tanzania

NDUGU ZANGU NAWAJUA, SITAKI KUKUMBUSHWA.





                 NDUGU ZANGU NAWAJUA.
1.     Nimejifunza si haba, natambua ndugu zangu,
Kuna dhahabu na shaba, najua tamu na chungu,
Hasidi nimpe huba, sitathubutu wenzangu,
Sihitaji kukumbushwa, ndugu zangu nawajua.

2.     Nasema ninawajua, kwa marefu na mapana,
Nao pia wanijua, kwa usiku na machana,
Iwe mvua ama jua, wenyewe tunashikana,
Sihitaji kukumbushwa, somo zangu nawajua.

3.     Simung’unyi nawajua, leo niwape yakini,
Muwache kujizuzua, suhuba pake moyoni,
Mkome kujifutua, sifa zitawaueni
Sihitaji kukumbushwa, ndugu zangu nawajua

4.     Mjue vitendo vyenu, vizuri mseme navyo,
Tegeni sikio zenu, msikie msemwavyo,
Naogopa kula chenu, sitaki kusemwa ovyo,
Sihitaji kukumbushwa, ndugu zangu nawajua

5.     Wa kushoto usijue, kuvuli katoa nini,
Hino ibada mjue, kwa mola wetu Manani,
Ushetani mtambue, kutangaza hadharani,
Sihitaji kukumbushwa, ndugu zangu nawajua

6.     Mtoa kitu kwa ria, huvaa vazi la mungu,
Adhabu tamshukia, aja lia kwa uchungu,
Hapa kikomo natia, nafunga kitabu changu,
Sihitaji kukumbushwa, ndugu zangu nawajua

          Dotto Chamchua Rangimoto(Njano5
          Mzalendo.njano5@gmail.com
          0784845394/0762845394
          Morogoro Tanzania